Chalamila: Sijaona Rais Samia ukielekeza Ukatoliki au Ulutherani wa mtu kufanya mambo unayoyataka

Chalamila: Sijaona Rais Samia ukielekeza Ukatoliki au Ulutherani wa mtu kufanya mambo unayoyataka

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa Kikao kazi cha Maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi, Oystebay, leo Septemba 4, 2023.


CHALAMILA: SIJAONA RAIS UKIELEKEZA UKATOLIKI AU ULUTHERANI WA MTU KUFANYA MAMBO UNAYOYATAKA
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema “Sijawahi kuona Rais ukielekeza Ukatoliki wetu au Ulutherani wa mtu mwingine kufanya mambo ambayo unayataka, ungesimama na kuanza kutuelekeza tungekuwa tumepoteza mwelekeo.

Kama kuna mtu yeyote atasimama kukuelekeza wewe na Serikali yako kufanya vitu ambavyo wanataka iwe hivyo, naomba usimame na unyooshe kamba kwa kuwa utapimwa kwa matokeo.

Simama katika mstari, hatuko tayari kuona Rais ukitukanwa na kurushiwa mawe, Polisi wameimba wakikuvaa tutawavaa, na mimi kama Mkuu wa Mkoa wa Dar naahidi wakikuvaa nitawavaa.

Rais Samia anazungumza
Rais Samia amepongeza jeshi la polisi kwa kupunguza uhalifu nchini, amewaomba kuimarisha dhana ya ulinzi shirikishi, wananchi wawe huru kufanya shughuli zao bila hofu ya kuvamiwa na majambazi.

Kumbe huyu naye ni chawa!
 
Asiyemfahamu huyo CHAWA na bendera fuata upepo, ndiye pekee atakayepata shida. Huyo jamaa akili yake siku zote huwa anaihifadhi tumboni, badala ya kichwani.
Afadhali tumboni, ubongo umekuwa embedded katika large intestine Kwenye mavi
 
Kauli za wateule wa mama mbona huwa zina ukakasi sana;
I. Huwa wanatumwa kusema hivyo badala ya yy mwenyw?
Ii. Kuna watu mpka wanamkosoa Mungu hapa duniani sembuse Rais wa nchi
Iii.Kutoa maoni, kukataa jambo lolote kwa ajili ya nchi sio jambo baya kwa sababu Rais anaongoza wanachi na sio wanyama ambao wao hawana uelewa wowote..
Iv. Njaaa mbaya sana kwa viongoz wetu katika kutetea nafasi zao, mm nisingependa wananchi wang wapewe maneno magumu na kutishwa kias hicho.
V. Ifke mahala sisi wanachi tuheshimiwe na viongoz wetu, mbona sisi tunawaheshimu sana tuu. Mbona sisi huwa hatuwatishi, mbona sisi huwa hatuwakalipii wakat wanaishi kwa kodi zetu.
 
Kauli za wateule wa mama mbona huwa zina ukakasi sana;
I. Huwa wanatumwa kusema hivyo badala ya yy mwenyw?
Ii. Kuna watu mpka wanamkosoa Mungu hapa duniani sembuse Rais wa nchi
Iii.Kutoa maoni, kukataa jambo lolote kwa ajili ya nchi sio jambo baya kwa sababu Rais anaongoza wanachi na sio wanyama ambao wao hawana uelewa wowote..
Iv. Njaaa mbaya sana kwa viongoz wetu katika kutetea nafasi zao, mm nisingependa wananchi wang wapewe maneno magumu na kutishwa kias hicho.
V. Ifke mahala sisi wanachi tuheshimiwe na viongoz wetu, mbona sisi tunawaheshimu sana tuu. Mbona sisi huwa hatuwatishi, mbona sisi huwa hatuwakalipii wakat wanaishi kwa kodi zetu.
Wapo hapo kumsifia maza kulinda vibarua vyao
 
Rais Samia anazungumza
Rais Samia amepongeza jeshi la polisi kwa kupunguza uhalifu nchini, amewaomba kuimarisha dhana ya ulinzi shirikishi, wananchi wawe huru kufanya shughuli zao bila hofu ya kuvamiwa na majambazi.
Kuna baadhi Wana mdanganya, ama wanamficha!

Kwa uchache, Raia wa Tanzania ambao wanafanya kazi za uvuvi Ziwa Victoria (Maarufu Ziwa Rwelu/Lwelu) hawako huru kufanya shughuli Yao Hii adhimu bila hofu.

Wavuvi wenye mitumbwi, na Mashine(injini za mitumbwi) Wana hofu sana. Wanafanya kazi kwa hofu na wasiwasi kwa sababu wanavamiwa na majambazi na kuporwa zana zao za uvuvi zikiwemo Mashine za uvuvi, na Simu. Wakati, mwingine wanakatwa mapanga ama kutoswa majini na Hata kuuwawa.

Kwenye Ziwa hilo Kuna boti ya polisi kwa ajili ya "patrolling". Inasemwa, hawa wanafanya kazi ya kukimbizana wafanya magendo tu lakini hawajihusishi namna ya kukabili wahalifu wanaowatia hofu wavuvi hawa ambao wanasaidia kukuza Uchumi wa nchi kwa kulipa Kodi, ada, tozo, na ushuru wa aina mbalimbali.

Matukio ya kuumizwa na kuporwa kwa wavuvi kwenye Ziwa Victoria inasisitizwa kuwa si ya kufikirika Bali ni matukio ya ukweli.

Rai kwa Mheshimiwa Rais Dr Samia Suluhu Hassan atamke neno la Faraja kwa wavuvi hawa wa Ziwa Victoria na maziwa mengine, mito na bahari wanao kabiliwa na tishio la ujambazi katika maeneo Yao ya kazi. Kisha wale ambao hawatimizi wajibu wao kurahisisha shughuli hii muhimu ya kiuchumi kwa nchi yetu wawajibishwe inavyostahili kwa mujibu wa sheria.

Asante kwa kusoma bandiko hili.

Kazi Iendelee.
 
Gharama Kwa Mkuu wa nchi Kwa nchi yoyote ile duniani na ulimwenguni kiujumla haiepukiki hata Kama Wananchi wanakula nyasi!!
ohooo! umenikumbusha mwaka 47 eti ndege ya rais itanunuliwa hata wananchi wakila nyasi! Sawa tu! ila 2024 mtaua raia 1000000 ili kujipitisha bure bure kama kawaida yenu stupid
 
Gharama Kwa Mkuu wa nchi Kwa nchi yoyote ile duniani na ulimwenguni kiujumla haiepukiki hata Kama Wananchi wanakula nyasi!!
Mkuu wa nchi aliye madarakani kwa wizi wa kura anapataje matumizi yote hayo?
 
Back
Top Bottom