Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Chapinga kushirikishwa katika Mchakato Mzima wa Maoni ya "Bima Ya Afya kwa wote" Kama serikali ilivyosema

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Chapinga kushirikishwa katika Mchakato Mzima wa Maoni ya "Bima Ya Afya kwa wote" Kama serikali ilivyosema

Chama cha Madaktari Nchini Tanzania (MAT) kimepinga na kusema kuwa hakikushirikishwa kwenye mchakato wowote wa kuandaa,Kutoa maoni au Kushiriki katika njia yoyote ile ya mchakato huo.

kinyume cha serikali inavyojinasibu kuwa Chama hicho kilishirikishwa kama Mdau Rasmi wa Afya..

Aidha Dr. Deusdedit Ndilanha, ambaye ni Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT)

ametangaza ya kuwa ameshitushwa na
taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionesha kuwa chama kilishiriki kwenye mapendekezo ya Kitita cha Mafao Cha Mwaka 2023 cha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)

"Chama kinakanusha kushiriki au kushirikishwa kwenye mchakato huu ,Hatua zilizopitiwa wakati wa mchakato" anasema Dr ndilanha..

"Chama kinawaomba wanachama na wadau wa afya kuwa na subira, Chama kitatoa tamko rasmi na msimamo wake mara baada ya kikao na kamati tendaji kukaa" anamalizia Dr Deusdedit Ndilanha

View attachment 2847744
View attachment 2847743

View attachment 2847759
Washirikishwe wasishirikishwe wangesaidia nini
 
Nahisi Serkali inataka kukusanya mapato zaidi ila sheria hii ni Ngumu kumeza kwakweli..

Subri ianze kazi utaona kilio cha wananchi..

Japo wengine kupinga ni Vigumu.."Kuona wadau kama viongozi wa dini wakipinga hiyo sahau" pia vivo hivyo kwa Wamiliki wa Hospitali na Vituo vya afya
Umeisoma? We ni nyumbu tu
 
Ile kamati iloundwa ya wataalam kuassess feasibility ilikuja na majibu yasiyo na furaha kwa wanasiasa, ndiyo sababu ya kuondolewa kwa Makubi sababu hakutaka siasa kwenye jambo serious kama hili...

Ukiona MAT wanakuwa na guts za kuikana serikali ujue wana uhakika na wanachokifanya..

Hakuna mtaalamu wa afya anaielewa serikali inachofanya kwenye hii bima kwa wote..

Iwapo NHIF tu inapumulia mipira, hii bima kwa wote itawezekanaje?
Hao MAT ni mapoyo tu wanaangalia maslahi yao. MAT ni kakikundi kadogo sana na hawahusiki na afya za watanzania.
 
Mabadiliko yapi hayo unazungumzia Sheria ya bima ya Afya imeshasainiwa Rasmi na Rais mwaka huu na ilisitishwa kwa sababu haikukidhi vigezo na walioirudisha ni Wabunge..

Wewe aliekudanganga Kuhusu haya yote unayoongea ni nani?

Sheria mara ya kwanza ilupelekwa mwaka 2022 na ilikataliwa na kamati ya bunge na Bunge wakasema bado inaukakasi kuhusu Mapato na baadhi ya sehemu!..

Miongozo yote Hutoka baada ya Sheria kupita wewe unazungumzia sheria zipi?
Na miongozo ipi?

Sio kila mara Tutetee Vitu hata kama havina uhalisia unafikri Chama cha madaktari hawana akili kutoa Maelezo bila wao kusoma?

Nimeisoma bima ya afya ikiwa mswada tangu mwaka 2022 na hata marekebisho yake na kuwa sheria mwaka 2023 na nilianzisha uzi humu!

AU unataka tuchambue makosa ya Miongozo na Bima hadharani?
😂😂😂 humjui kila mtu humu so usikariri, mswada ulishatika mbona mapema sana na uliwekwa pending ila kuhusu pricelist kijana huwezi kuyajua yaliyomo ndani kwasababu hujui hata mchakato gani unafanyika kutengeneza pricelist mpya. Miongozo gani inatumika hivyo acha kubashiri vitu, I bet unajua STG tu ndio inayotumika. Acha wenge boss.
 
Watu wanachanganya UHI (Universal Health Insurance) na NHIF. Msimamizi wa UHI ni TIRA sio NHIF hivyo implementation ya UHI bado hayajaanza kwakuwa UHI lazima makubaliane yafanyike na kila insurance scheme kwa pamoja kutenfeneza kitita cha mafao cha basic yaani chakila mwananchi ila yaziada ni mpaka scheme iyaongeze yenyewe kutokana na operation cost yao. Hii iliyotoka ni kitita cha mafao cha NHIF kwawatoa huduma nasi UHI tuache kuweka propaganda.
 
Umeisoma? We ni nyumbu tu
Nimeisoma kipengele kwa kipengele. Tangunikiwa mswada wa kwanza mwaka 2022..
Na hii ya mwaka 2023 mpaka ikawa sheria..
Sasa
Kati yangu mimi na wewe nani nyumbu?
Maana mimi sifati mkumbo nafata facts..
 
😂😂😂 humjui kila mtu humu so usikariri, mswada ulishatika mbona mapema sana na uliwekwa pending ila kuhusu pricelist kijana huwezi kuyajua yaliyomo ndani kwasababu hujui hata mchakato gani unafanyika kutengeneza pricelist mpya. Miongozo gani inatumika hivyo acha kubashiri vitu, I bet unajua STG tu ndio inayotumika. Acha wenge boss.
By the way kama ulivyosema humjui mtu humu..
Mimi sio kijana hicho ni cha kwanza..
Sheria imepita tarehe 01 December 2023..

Kiufupi mchakato mzima naujua kuanzia ulivyoanza mpaka ulipofikia kufikia hatua ya mwanzo mpaka unakuwa sheria..

Kingine usichanganye kati ya Pricelists ambayo ni just ambayo ni just a schedule package for claimaint in NHIF schemes.. Na sheria ya Bima kwa ujumla wake tatizo vijana mnakurupuka na mambo na kuhisi mnayajua...
Hakuna nilichobashiri nachokiongea ni 100%
 
Mambo ya Afya za binadamu wanakaa watu wachache kuamua afya zao Nchi ngumu sana hii mambo ya mikataba hata hicho chama cha Wanasheria hawapewi nafasi tunaenda enda tu kama gari la Mkaa..
Wanasiasa ndio wafanya maamuzi makubwa hapa nchini
 
Watu wanachanganya UHI (Universal Health Insurance) na NHIF. Msimamizi wa UHI ni TIRA sio NHIF hivyo implementation ya UHI bado hayajaanza kwakuwa UHI lazima makubaliane yafanyike na kila insurance scheme kwa pamoja kutenfeneza kitita cha mafao cha basic yaani chakila mwananchi ila yaziada ni mpaka scheme iyaongeze yenyewe kutokana na operation cost yao. Hii iliyotoka ni kitita cha mafao cha NHIF kwawatoa huduma nasi UHI tuache kuweka propaganda.
This is 100% sasa ulichokuwa unabisha ni nini
 
By the way kama ulivyosema humjui mtu humu..
Mimi sio kijana hicho ni cha kwanza..
Sheria imepita tarehe 01 December 2023..

Kiufupi mchakato mzima naujua kuanzia ulivyoanza mpaka ulipofikia kufikia hatua ya mwanzo mpaka unakuwa sheria..

Kingine usichanganye kati ya Pricelists ambayo ni just ambayo ni just a schedule package for claimaint in NHIF schemes.. Na sheria ya Bima kwa ujumla wake tatizo vijana mnakurupuka na mambo na kuhisi mnayajua...
Hakuna nilichobashiri nachokiongea ni 100%
Sasa nikuulize 😂😂😂😂 iliyotolewa na NHIF ni nini, pricelist au kitu gani au hujui kitita cha mafao ni nini? Watanzania ni shida sana. Pricelist au kitita cha mafao cha 2016/2017 kinafutwa kinaanza kutumika cha 2023/2024 mnamo January. Sasa UHI hapo unaileta na inaingia wapi😂😂😂
 
Huyo Rais wa MAT hajui wenzake wanatafuta Kura kwaajili ya Uchaguzi 2025.

Amuulize Dokta Ulimboka alichofanywa na hiyo hiyo Serikali alipojaribu kwenda kinyume nao.

Ajue anaishi na kufanya kazi Nchi ya Giza hii [emoji847]
solution ni kumkatisha tamaa kwenye ukwel au mimi na ww kuungana nae kuonesha nguvu ya umma?

Sent from my HUAWEI NXT-L29 using JamiiForums mobile app
 
Kisheria hivi ni vuama viwili tofauti. Medical Association of TANZANIA wakae watulie. Hakuna mtu aliyewataja kwenye report ya Wizara. Waliotajwa kuhusishwa ni Medical Association of TANGANYIKA.

Medical Association of TANGANYIKA wakiamua kuwaburuza Wizara mahakamani serikali kwa kutowashirikisha, watashinda kesi misa ya kwanza tu.

1703086060090.png
 
Sio tunakoelekea nadhani tulipo na nikiangalia vijana wetu hawa sijui watafanya nini huko mbele maana kila sehemu ni password tena zile ngumu na mazingira ya kuwaandalia maisha yao bado pia ni magumu tunabaki kwenye mduara wa Umasikini tuu..
Umeongea ukweli mtupu. Vijana tunao enda kua watu wazima 10years from now kazi tunayo. Mazingira yanazidi kua wagumu.

Naombea tu wasiiguse ardhi. Maana wakigusa na hapa tu. Kama babu yako hakutunza hata eka10 huko mmekwisha
 
Hahahaha.........wale watu wanatisha Mkuu, hata Msanii Roma hadi leo hii hakuwahi kusema waliomteka na kumtesa ni akina nani?

Nenda umuulize hata Tajiri Mo Dewji kama naye aliweza kuwataja

Hatari [emoji119]
Niliiona ile interview ya Moo baada ya kutoka matekani nikajua hapa ni usaniii tu.

Wazee wakibana pumbu vizuri unakaa kimya tu.
 
Kisheria hivi ni vuama viwili tofauti. Medical Association of TANZANIA wakae watulie. Hakuna mtu aliyewataja kwenye report ya Wizara. Waliotajwa kuhusishwa ni Medical Association of TANGANYIKA.

Medical Association of TANGANYIKA wakiamua kuwaburuza Wizara mahakamani serikali kwa kutowashirikisha, watashinda kesi misa ya kwanza tu.

View attachment 2848306
na MAT wakiamua
 
na MAT wakiamua
Medical Association of TANZANIA (MAT) wakienda mahakamani wanashinda haraka sana mkuu. Serikali inawasingizia kushirikishwa wakati walioshirikishwa ni Medical Association of TANGANYIKA (MAT). Ndicho ninachomanisha hapa mkuu.
 
Back
Top Bottom