Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Ila ndio ukweli na hii sio kwa mahakimu tu hata majaji wako hivyo!
Kuna mifano hai mingi sana na huenda jukwaa hili likatumika kuwaumbua mcchana kweupe!
 
Kwa mantiki hii sasa wenye hoja kuwa mkataba wa DP world mahakama zetu ziwe ndio watatuzi wa kesi btn Gov and Dp na sio South Afrika
 
Sasa wanashtuka kuambiwa ukweli?
 
Haya
 

Attachments

  • 8E4489CA-2873-4251-AAE3-3A494B5B7999.jpeg
    137 KB · Views: 2
Bado watakuja kusema alikuwa mzalendo mpenda amani
 
Rostam aliishuku mahakama hiyo Juni 26, mwaka huu alipozungumzia sakata la bandari akisema, “Hakuna mwekezaji atawekeza kwenye nchi ambayo kesi ikipelekwa hapo Kisutu kiongozi yoyote anaweza kupiga simu akaielekeza mahakama nini cha kufanya.”

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Rostam alizungumzia faida za uwekezaji wa sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari, akirejea mkataba wa ushirikiano uliosainiwa na Serikali ya Tanzania na Dubai kuhusu uwekezaji na uendelezaji wa bandari nchini.

Hata hivyo, sakata hilo limeibua hisia tofauti za wananchi, wengine wakikosoa kutokana na kile wanachoeleza kuwa, baadhi ya vifungu vya mkataba huo vina kasoro na hatari kwa masilahi ya nchi.

Kutokana na kauli yake, iliyotafsiriwa kuwa ni kuidharau Mahakama, JMAT imechapisha taarifa kwa umma leo, Julai 4, 2023 ikimtaka mfanyabiashara huyo athibitishe kauli yake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, chama hicho hakikuwahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha maofisa wa mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa uamuzi.

“Kutokana na maelezo hayo, tumesikitishwa na kauli ya Rostam Aziz ambaye hatukutarajia aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho,” imeeleza taarifa hiyo.

JMAT kupitia taarifa hiyo, imesema kauli za mfanyabiashara huyo zinahatarisha uhusiano na ushirikiano kati ya mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi.

“Tunaomba wananchi wenye nia njema na Mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na imani na mfumo wa utoaji haki nchini," imeeleza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…