Changamoto ya Malezi: Watoto kuharibu vitu

Changamoto ya Malezi: Watoto kuharibu vitu

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Wasalaam Wakuu!.

Watoto ni baraka kubwa sana na kila mzazi angelipenda kuwa na watoto ili kujenga familia yenye furaha na amani. Watoto ni faraja kubwa sana kwa wazazi lakini muda mwingine ni changamoto sana.

Je, umewahi kukutana na changamoto ya watoto kuharibu mali na vitu vya thamani katika kipindi cha ukuaji wao? Tena kwa sababu ya utoto wake, huna cha kufanya. Unabaki kugugumia tu kwa maumivu.

Mimi ilinitokea hivi,
Smart Tv yangu ya LG, nimenunua zangu kwa Benson Electronics (Arusha), Tsh 2,700,000. Nikatumia kwa miezi miwili tu 😭😭😭.

Nipo sebuleni naagalia TV, mwanangu wa miaka minne aliwekewa Movie ya Jet Lee (sina hakika). Sasa kashazoea kuangalia mara nyingi sana. Movie ile ilikuwa ni ya kutumia majambia.

Mimi nipo zangu busy kumuangalia anavyocheza na mwiko mkononi, 'baba anafanya hivi'.

Najisemea moyoni, nimepata kidume. Atakuja kuwatandika watu mpaka washangae. Pasipo ya kujua nahatarisha amani ya moyo wangu kwa dakika chache zijazo.

Dogo anacheza mbele yangu, ili nimuone vizuri. Wala hata sikumuambia aje mbele, basi tu baada ya kuona nafurahia akaamua kuja mbele kunifurahisha zaidi.

Karusha rusha mwiko, Paaph Kwenye TV. Aliipiga kwa nguvu na tv kuweka crack na kuvujia wino. Haikuonyesha tena.

Ile hasira niliyokuwa nayo, acha kabisa. Dogo kanichomea 2.7m yangu wakati hata sijaenjoy bado? Hasira zilinitanda sana. Nikabaki naduwaa tu.

Pasipo kujua akaniletea remote, 'babaa imezima, niwashie'. Nikatamani nimuwashe yeye kibao cha nguvu, ila mkono unashindwa kunyanyuka kumfikia.

Kwa ile hasira, akatokea mama yake. Nikamuwakia yeye kuwa kamfundisha mwanae upuuzi kaja kuvunja TV bure. Hahahaha!.

Anamuambia mama yake, mbona haioneshi? In fact, sauti bado ilikuwa inasikika kutoka kwenye Theater.

Basi bhana, nikapotezea. Sasa ningelifanyaje? Ndiyo ile, umia utakavyotaka. Huna cha kunifanya 😂😂😂.

Ni bora watoto wafanye uharibifu ukiwa mbali. Vinginevyo unaweza kufanya jambo ambalo hukulitegemea. Hasira zitakuongoza kufanya jambo ambalo utalijutia baadae.

Je, ni changamoto gani iliyowahi kukukumba wewe kama mzazi?
 
Wasalaam Wakuu!.

Watoto ni baraka kubwa sana na kila mzazi angelipenda kuwa na watoto ili kujenga familia yenye furaha na amani. Watoto ni faraja kubwa sana kwa wazazi lakini muda mwingine ni changamoto sana.

Je, umewahi kukutana na changamoto ya watoto kuharibu mali na vitu vya thamani katika kipindi cha ukuaji wao? Tena kwa sababu ya utoto wake,
Asee Pole sana Kwa mtihani huo, Watoto ni haraka ila sasa wanaweza kufanya jambo ukabaki unamuangalia tu na huna kitu utamfanya

Sent from my SM-C9000 using JamiiForums mobile app
 
Mtoto wa miaka minne unasema eti kazoea kuangalia movie za kupigana na kutumia kwa kutumia majambia!!hauko siriazi Chief aiseh mpige mamake marufuku kumvukisha mtoto hatua za makuzi.haiwezekani mtoto wa umri huo useme eti kazoea.😳😳

Kwanza hongera zimfikie mtoto mvunja tv.ukiangalia kwa jicho la tatu ni funzo amewapa.mbadilishie haraka sana mtoto makuzi.
 
Liwe fundisho kwako na mke wako kumuachia mtoto aangalie movie za wakubwa. Movie zinakuwaga na umri umeandikwa Kwa sababu kama hizi. Watoto wadogo hawatakiwi kujua mambo ya mapanga panga. Si ulitaka dume katili basi amekufanyia huo ukatili, hongera.
 
Baba junior jitahidi malezi huyo mwanao asije anza bangi mapema mana chuga ni kiwanda cha bangi sasa ka nidhamu imekushinda ngoja akue kidogo age ya foolish ndo utajua hujui. Mfundishe mtoto nidhamu
 
Mtoto wa miaka minne unasema eti kazoea kuangalia movie za kupigana na kutumia kwa kutumia majambia!!hauko siriazi Chief aiseh mpige mamake marufuku kumvukisha mtoto hatua za makuzi.haiwezekani mtoto wa umri huo useme eti kazoea.😳😳

Kwanza hongera zimfikie mtoto mvunja tv.ukiangalia kwa jicho la tatu ni funzo amewapa.mbadilishie haraka sana mtoto makuzi.
Chakorii,

Muda mwingi nipo kazini. Narudi saa mbili, nikiwahi sana saa 1. Walau weekend napata muda wa kuwepo.

Sasa kwa kuwa anashinda na dada wa nyumbani, basi anachokiangalia dada naye anakiangalia.

Ni ngumu sana dada kumkataza kwa kuwa hata yeye anapenda kuziangalia.

Lakini, nikiri ya kuwa ni jambo lisilo na afya. Hapaswi kuangalia kwa umri wake na ndivyo ambavyo nimekataza movie zote za aina hiyo isipokuwa ya kitoto kuangaliwa nyumbani.

Ahsante kwa ushauri!.
 
Liwe fundisho kwako na mke wako kumuachia mtoto aangalie movie za wakubwa. Movie zinakuwaga na umri umeandikwa Kwa sababu kama hizi . Watoto wadogo hawatakiwi kujua mambo ya mpanga panga. Si ulitaka dume katili basi amekufanyia huo ukatili, hongera.
Naam!.

Nikiri kosa na limeshatatuliwa!.

Akhsante kwa ushauri.
 
Mimi wa kwangu alichukua coin ya sh. mia akaifunga kwenye rubberband halafu akairusha kama manati paaah kwenye kioo. Halafu akajiwahi eti nisamehe usinipige...nilikosa nguvu hata ya kuongea
 
Baba junior jitahidi malezi huyo mwanao asije anza bangi mapema mana chuga ni kiwanda cha bangi sasa ka nidhamu imekushinda ngoja akue kidogo age ya foolish ndo utajua hujui. Mfundishe mtoto nidhamu
Hahahahaha!.

Cariha,

Naamini hataanza kuvuta bangi. Tangu anivunjie TV, nimemnyoosha barabara. Kaingia kwenye line.

Ptyuu Mbaka!. Mungu aepushie mbali mwanangu kunishinda tabia.
 
Mwanangu wa mwaka mmoja na nusu alichukua simu yangu mpya akarusha chini alafu anacheka. Ilipasuka kioo ila nililichua nikamwangalia then nikatoka karibu yake.
Unashindwa cha kufanya, unabaki kuumia tu.

Usipoangalia unaweza kumuumiza.
 
Nimecheka......mimi wa kwangu alichukua coin ya sh mia akaifunga kwenye rubberband halafu akairusha kama manati paaah kwenye kioo. Halafu akajiwahi eti nisamehe usinipige...nilikosa nguvu hata ya kuongea
Watoto ni wajanja sana.

Anajua amekosa alafu anakuwahi. Inakubidi tu umsamehe kweli. Huna la kufanya.
 
Hahahahaha!.

Cariha,

Naamini hataanza kuvuta bangi. Tangu anivunjie TV, nimemnyoosha barabara. Kaingia kwenye line.

Ptyuu Mbaka!. Mungu aepushie mbali mwanangu kunishinda tabia.
Ila na wewe huyo mtoto kwanini usiwe unampeleka shule una mwachia house girl ukute anaangalia hata video za ngono na mtoto, sasa ka anaangalia video za mapigano si anaharibu akili ya mtoto. Block chanel zote marufuku kuangalia vitu vya ajabu na mtoto bana, hafu kafundishe nidhamu na kaelekeze kwa upendo hakatakuwa kaharibifu bana
 
Ila na wewe huyo mtoto kwanini usiwe una mpeleka shule una mwachia hausegirl ukute anaangalia hata video za ngono na mtoto, sasa ka anaangalia video za mapigano si anaharibu akili ya mtoto. Block chanel zote marufuku kuangalia vitu vya ajabu na mtoto bana, hafu kafundishe nidhamu na kaelekeze kwa upendo hakatakuwa kaharibifu bana
Yupo shule. Anarudi saa 6. Kwa hiyo bado ana muda mwingi sana wa kuwa nyumbani.

Mdada nishamuelekeza aangalie Tv mtoto wakati hayupo. Asubiri mpaka mama yake mtoto arudi then wataendelea kuangalia.
 
Miezi michache iliyopita niliingia chumbani kusali. Nikamuacha mwanangu na mama yake ghafla nikasikia TV imedondoka kumbe kuna waya alishika ikaanguka chini. Kiukweli nilimwambia mama yake sitatoa senti kununua TV mpya nyingine. Ila kesho yake ikabidi nichukue fedha yangu ya akiba nikaenda kununua TV na kila nilipokua nikimuangalia mtoto alikuwa anaonyesha kweli kakosea.

Ni mtoto wa miaka miwili kamili. Sikuwa na namna zaidi ya kununua TV mpya na nikasema ni afadhali ni mwanangu angekua yupo kwa mwingine angejisikiaje. Hii ni baraka kutoka kwa Mungu.
 
Chakorii,

Muda mwingi nipo kazini. Narudi saa mbili, nikiwahi sana saa 1. Walau weekend napata muda wa kuwepo.

Sasa kwa kuwa anashinda na dada wa nyumbani, basi anachokiangalia dada naye anakiangalia.

Ni ngumu sana dada kumkataza kwa kuwa hata yeye anapenda kuziangalia.

Lakini, nikiri ya kuwa ni jambo lisilo na afya. Hapaswi kuangalia kwa umri wake na ndivyo ambavyo nimekataza movie zote za aina hiyo isipokuwa ya kitoto kuangaliwa nyumbani.

Ahsante kwa ushauri!.
Una TV ya 2. something unashindwa kuicontrol na kutia mipassword kwenye baadhi ya channel. Man kuwa mkali juu ya mtoto, kuna siku utakuja kukuta mwanao kamkata mtoto mwenzie kwa panga kisa Aliona jana yake kwenye tv. Ndugu yangu kuwa mkali na tv, weka password kila kitu.
 
UNatv ya 2.something unashindwa kuicontrol na kutia mipassword kwenye baadhi ya chanel.man kuwa mkali juu ya mtoto.kuna siku utakuja kukuta mwanao kamkata mtoto mwenzie kwa panga kisa Ali ona jana yake kwenye tv.ndugu yangu kuwa mkali na tv.weka password kila kitu
Noted with thanks.
 
Back
Top Bottom