Changamoto za kuishi nyumba moja na rafiki au mtu yeyote

Changamoto za kuishi nyumba moja na rafiki au mtu yeyote

Ninamaanisha kushirikiana kodi ili kupunguza ugumu wa maisha. Inaweza kuwa ni wanafunzi wa Chuo, waajiriwa wapya au hata waliopata ajali za maisha na wanaanza moja. Mfano wanafunzi wanachukua chumba cha 40,000 wanachangia kodi.

Kuna wale waajiriwa wasiopenda kuishi Uswahilini. Wanachukua nyumba nzima ya vyumba vitatu wanagawana vyumba. Lakini wanapika jiko moja na kuoga bafu moja.

Changamoto nyingi zinaanzia kwenye usafi, chakula na matumizi ya sitting vroom. Kama mnakula pamoja kuna wanategea kununua chakula na wengine kunywa hata pombe za wengine.

Usafi pia huwa ni kero ya ziada.
Sijaelewa huu uzi una lengo gani...
 
Bwana Mimi tulikaa hostel keko na jamaa mmoja mnyaturu . Bwana wee jamaa alikuwa mchafuu sijawai ona. Afu full mtu wa dini kwaya kama zote. Na lile joto la dar tulikoma humo room.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi shida ilikuwa nakutana na wadada ni wachafu,mmoja huyo alikuwa mzenji jamani anaweza lala na kiatu kitandani et kisa kachoka
Huyo wa pili sasa alikuwa yeye anachojua ni kuvaa lakini mambo ya ndani usimuulize nyumba iko rafu mda wote na ilikuwa nikimbeba kwenye matumizi lakini ikitokea kapata hela anaenda kununua nguo jamani inachosha aswa!
Pole sana, inakera kwa kweli
 
Ninamaanisha kushirikiana kodi ili kupunguza ugumu wa maisha. Inaweza kuwa ni wanafunzi wa Chuo, waajiriwa wapya au hata waliopata ajali za maisha na wanaanza moja. Mfano wanafunzi wanachukua chumba cha 40,000 wanachangia kodi.

Kuna wale waajiriwa wasiopenda kuishi Uswahilini. Wanachukua nyumba nzima ya vyumba vitatu wanagawana vyumba. Lakini wanapika jiko moja na kuoga bafu moja.

Changamoto nyingi zinaanzia kwenye usafi, chakula na matumizi ya sitting vroom. Kama mnakula pamoja kuna wanategea kununua chakula na wengine kunywa hata pombe za wengine.

Usafi pia huwa ni kero ya ziada.
Uzi mzuri, Safi kabisa
 
First Year nilipanga na mwamba mmoja (binamu yangu) yeye alikua second year, aisee alinyoosha siwezi sahau. [emoji23]

Kwanza, alikua anapenda juice za matunda. Kila siku alikua ananunua lita mbili za juice ya matunda, halafu alikua hamalizi yote, lazima abakize kwenye chupa.
Halafu hayo mabaki ya juice alikua anayatunza ndani ya nyumba hata kwa mwezi mzima mpaka yanavunda bila kuyatupa dampo. Alikua anapenda kufunga madirisha, hiyo harufu ya uvundo ndani ya ghetto aiseee ukikaa dakika moja tu lazima ukimbizwe ICU kwa matatizo ya upumuaji [emoji23].

Pili, alikua hajui kupika wala kuosha vyombo ila nikipika alikua wa kwanza kuja kula. Sema fresh tu nilivunga sababu alikua mwenyeji wangu wa jiji wakati huo.

Tatu, Alikua anafua nguo mara moja kwa semester, mara zote ilikua kipindi anachotaka kurudi nyumbani baada ya kumaliza UE. Nguo chafu alikua anatunza uvunguni mwa kitanda halafu anachagua zile zilizochafuka kidogo anarudia kuzivaa tena ( kitaalamu inaitwa system update). Harufu ya uvundo wa nguo ilifanya kusiwe na tofauti kati ya gari la taka na ghetto.

Nne, Alikua anapenda kuangalia movies mpaka sasa 8 usiku huku sauti ikiwa juu sana na wakati mwingine alikua akikesha na movies mpaka asubuhi. Hivyo alinipa wakati mgumu sana wakati wa kulala sababu ya makelele.

Tano, Alikua anapenda kushinda ndani hata wakati wa mchana akicheki movies hivyo alininyima chance ya kuleta totoz ghetto. Hivyo sikuweza kumpiga exile hata mara moja, inauma sana [emoji23]

Sita, alikua hapendi wageni waje ghetto sababu ya uchafu wa ghetto. Hivyo hata rafiki zangu sikuwahi kuwakaribisha nyumbani licha ya wao kutaka kunitembelea mara kwa mara. Alikua mchafu asiependa kudhalilika.

Sema mwamba alikua anapenda sana kusikiliza mahubiri ya Mwl.Mwakasege na kusoma Biblia hivyo alikua ananifundisha mambo mengi ya Kikristo.
Kingine hakua na mkono wa birika.

Nilikaa na mwamba semester moja tulivyorudi chuo kutoka likizo nikapanga ghetto langu nikapumua, nikaanza kula utawala na mimi.
 
Hakuna kitu Cha kushare ambacho hakina kero.Hata unaposhare chumbana mwenza wako bado Kuna kero utaziona. Chamsingi Ni kuvumiliana.
 
First Year nilipanga na mwamba mmoja (binamu yangu) yeye alikua second year, aisee alinyoosha siwezi sahau. [emoji23]

Kwanza, alikua anapenda juice za matunda. Kila siku alikua ananunua lita mbili za juice ya matunda, halafu alikua hamalizi yote, lazima abakize kwenye chupa.
Halafu hayo mabaki ya juice alikua anayatunza ndani ya nyumba hata kwa mwezi mzima mpaka yanavunda bila kuyatupa dampo. Alikua anapenda kufunga madirisha, hiyo harufu ya uvundo ndani ya ghetto aiseee ukikaa dakika moja tu lazima ukimbizwe ICU kwa matatizo ya upumuaji [emoji23].
Namba 6 imenichekesha sana
 
Kuishi pamoja inasaidia kimtindo kupunguza gharama za maisha hasa Ile kiwanafunzi au washkaji tu lkn kuishi na watu wa staili hii wanachosha

Wavivu.
Kuzingatia mazingira ya geto kwao kipengele hadi mpigizane kelele , kwenye inshu ya usafi ,kupika ,wavivu kujitolea

Ma don't care
Hawa mm ndio wamenishinda Kabisa ,anaweza kuingia chooni akakuta choo kichafu na Wala hasijishughurishe nacho anafanya yake anatembea, wanaweza kuishi mazingira machafu ,wakala kwenye mazingira ya hovyo na aisione tatizo lolote....mtu kama huyu wa kuishi mwenyewe kuishi naye itakuwa kama amekuoa
 
Mimi jamaa niliyekuwa naishi nae kuchangia kodi ndo ilikuwa mtihani yaani mimi nilikuwa nalipia 80% ya kodi yeye kumalizia hiyo 20% ni shida na ukijiroga umpe hiyo ili aongezee apeleke,basi ujue hata ongeza hata hiyo uliyompa ataila.kingine kuteka maji hataki na ukiteka basi akiingia kuoga anamaliza ndoo 2 za 20L.
 
Namba 6 imenichekesha sana
Chief, kuishi wanaume wawili ghetto moja its an underrated talent. Siwezi rudia kosa tena .
Bora nipange chumba cha elfu 20 kwa mwezi nikiwa nina freedom ya maisha yangu kuliko kuishi ghetto kali ukiwa hauna uhuru.
 
Back
Top Bottom