Inahitaji uwe na tabia za kike kwa walau 35% kwa mwanaume kuanzisha mada ya muelekeo wa kimasimango namna hii.
Dear idiots, hawa wadada wa kazi mnaowananga hapa kuwa hawajui kuwasha TV, hawajui tofauti ya soda na maji na kadhalika, wangekuwa na elimu na exposure ya kiwango hicho mnachotamani wawe nacho, wangekuwa majumbani mwenu wakiosha vyombo kwa ujira wa elfu 40 kwa mwezi?
There is always first time for everything...kwa nini umgeuze kituko? Mnawaongelea as if ni watu fulani mliwapeleka shule halafu hamkuona return ya hivyo juhudi yenu. Hayo majiko ya gesi, TV na majokofu, mama na baba zenu huko vijijini wanajua kuyatumia?
Acheni tabia za kujishaua shaua, kuna wasaidizi wa nyumbani wenye elimu zao kama mnataka, wapo huku Masaki, wanajua hadi kutumia majacuzzi, wanaendesha magari kuwafuata watoto shule, wanajua kutumia washing mashine na wanaongea kiingereza na kihispania pia, wanalipwa $400 kwa mwezi, waajirini hao.