Tetesi: Chanjo za Corona zimetua nchini rasmi

Tetesi: Chanjo za Corona zimetua nchini rasmi

Mbona chanzo ulichoweka hakijasema kama chanjo tayari zimeletwa?
Na kadri ya habari hakuna mahali imesemwa kuwa serikali imeaagiza/itaagiza chanjo kwa ajili ya watanzania isipokuwa imeruhuru ofisi za balozi na taasisi za kimataifa kuagiza na kuchanja raia wa nchi zao na wafanyakazi wa ofisi zao ili kuendana na taratibu zilizopo katika nchi zao(NB chanjo hizo zitaletwa kwa utaratibu chini ya wizara ya afya nchini)
Hebu soma upya tena.
 
Ndo nini?
TRUMPET.jpg
 
Nchi isimame maana yake nini?
Kwanini unalalamika kuwa habari ya chanjo imeletwa wakati wa sakata la Sabaya? Ulitaka iletwe lini? Kwanini unaita kinyemela wakati na tangazo unaliona hapo linasema ndio kwanza wameruhusiwa kuleta balozi kwa ajili ya raia wao?
 
Kwanini unaita kinyemela wakati na tangazo unaliona hapo linasema ndio kwanza wameruhusiwa kuleta balozi kwa ajili ya raia wao?

Sishangai wewe kutokusoma na kuelewa.

Maana wengi wenu humu mna uwezo hafifu wa kuchanganua mambo katika muktadha wake.

Na cha ajabu kuna wengine wanajiita majasusi humu (sijui hata huo ujasusi waliutoa wapi?).

Tanzania inajulikana msimamo wake tangu kipindi cha Rais Magufuli kwamba imekataa kufuata masharti yaliyowekwa kupambana na huo ugonjwa wa kizungu unaoitwa corona.

Kisha mama samia akaunda kamati ili kupima kama huo msimamo wa Rais Magufuli uko sawasawa!

Kamati ikatoa majibu kwamba, msimamo uliowekwa na Rais Magufuli haukuwa sawasawa (as expected).

Unatarajia samia aende tofauti na hilo?

Kama angekuwa anatambua kwa dhati kwamba msimamo wa Rais Magufuli uko sawasawa, unadhani angeunda kamati?
 
Sishangai wewe kutokusoma na kuelewa.

Maana wengi wenu humu mna uwezo hafifu wa kuchanganua mambo katika muktadha wake.

Na cha ajabu kuna wengine wanajiita majasusi humu. (sijui hata waliutoa wapi huo ujasusi?).

Tanzania inajulikana msimamo wake tangu kipindi cha Rais Magufuli kwamba imekataa kufuata masharti yaliyowekwa kupambana na huo ugonjwa wa kizungu unaoitwa corona.

Kisha mama samia akaunda kamati ili kupima kama huo msimamo wa Rais Magufuli uko sawasawa!

Kamati ikatoa majibu kwamba, msimamo uliowekwa na Rais Magufuli haukuwa sawasawa (as expected).

Unatarajia samia aende tofauti na hilo?

Kama angekuwa anatambua kwa dhati kwamba msimamo wa Rais Magufuli uko sawasawa, unadhani angeunda kamati?
Mbona unahangaika sana mkuu hadi unakuwa hueleweki sasa. Shida yako nini hasa tukusaidie maana mwanzo umelalamika kwamba Tanzania imeruhusu chanjo kinyemela tumekujibu kuwa haijaruhusu bado ila maamuzi ya kamati yanakwenda kujadiliwa na baraza la mawaziri, ukageuka ukasema kwanini hata hiyo ya raia wa kigeni imeruhusiwa eti kipindi Sabaya kapelekwa mahakamani nikachukua muda wangu kukuelimisha kuwa kupelekwa mahakamani kwa Sabaya ulitakaje kwani, kila kitu kisimame? Who is Sabaya kwani? Umegeuka sasa unazungumzia msimamo wa Magufuli kuhusu korona!

Unauliza iwapo Rais Samia angetambua msimamo wa Magufuli uko sawa angeunda kamati, ina maana hujui kuwa Rais Samia kaona huo msimamo hauko sawa hadi sasa?

We jamaa usituchoshe. Chanjo sio lazima, wewe kama hutaki kuchanjwa tuliza bega sijui kalio acha wanaotaka kuchanjwa wachanjwe fullstop! Huna haki kuwasemea wengine na kuanzia sasa tambua kupelekwa mahakamani kwa Sabaya ni kama kupelekwa kwa mshtakiwa mwingine yoyote na hakuna mantiki eti kushangaa kwanini kitu fulani kimetokea wakati Sabaya anapelekwa mahakamani. Nakuuliza tena, ULITAKA SABAYA AKIPELEKWA MAHAKAMANI KILA KITU KISIMAME NCHINI?
 
Back
Top Bottom