Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini?

Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini?

Ni kweli mkuu kuna muumba na mm naamini hivoo lakini mada haijataka tujibu kwa dini 🤣🤣 wala sayansi bali tutunie akili zetuu

Unakubali ya kuwa akili ina ukomo ? Ulitakiwa ujue kwanza akili ni nini, ujue ukamilifu wa akili na udhaifu wake.

Ushawahi kujiuliza kwanini Wanafalsafa wa kale walikuja na majibu mengi juu ya swali Moja la chanzo Cha kila kitu ? Wapo walio sema chanzo Cha kila kitu ni Moto, wapo waliosema hewa, wapo waliosema Moshi, wapo walio sema Atomu, bali wapo waliosema namba wakaenda mbali wakasema ukamlifu unawakilishwa na namba kumi. Lakini wapo jaribu kuukaribia ukweli lakini wakakosea katika katika kuelezea mfano ni Aristotle aliyekuja na nadharia ya Prime Mover na zile ten Categories zake. Sasa Hawa walitumia akili na wakakosea sababu akili ina ukomo wake.

Sasa ufunuo Toka kwa yule aliye umba ukaja kutoa majibu ambayo akili imekomea, lakini Kuna ishara za kutumia akili na milango ya fahamu ambazo zipo ukiziangalia hizo unakubali ya kuwa Ulimwengu umeumbwa.
 
1. Si lazim awe ameumbwa.
Umesema vitu haviji from no where.

So kama ni hivyo chanzo cha uwepo wa tuvionavyo na tusivyo viona ni nini? Material yaliyotumika yalitoka wapi?

Jiwe unaloliona mahala popote liwe dogo au kubwa.. Hakuna binadamu ambaye lisogelea kwa umri. Hewa unayo vuta binadamu kaikuta. Unalijua hilo?

Naam sio tu kwamba nimesema bali huo ndio uhalisia. Hakuna anaye pinga hili labda mjinga asiye fikiria mambo kwa undani na aliye athiriwa na nadharia za Kisayansi au Falsafa.

Chazo ni Mungu muumba, yeye ndio anajua yalitoka wapi, katika uumbaji upo wa aina tofauti, Kuna uumbaji ule wa Adamu na mama yetu Hawa, Kuna uumbaji unaotokana na sisi kujamiina na Wanawake na Kuna uumbaji wa Mola akisema kitu fulani kiwe na kina kuwa.

Nalijua hilo, sababu mwanadamu ndio kiumbe wa mwisho kuumbwa.
 
Unathibitishaje kwamba dunia na maisha yalisukwa kwa mipangilio?

Hili pia unahitaji ushahidi ? Hivi hii mijadala huwa mnajipanga kwa ajili ya ubishi au ? Hivi uwepo wa usiku na mchana ni jambo la Bahati mbaya ? Uwepo wa jua ni jambo limezuka tu ? Kwanini jua lisichomoze Kaskazini na kuzama kusini ?

Huoni misimu ya mvua huoni misimu ya kiangazi ? Hivi vyote vinahitaji ushahidi au uthibitisho gani kwamba vimesukwa na kuwekewa nidhamu maalumu ?
Je dunia na maisha haviwezi kujipangilia vyenyewe tu?

Hivi mtu mwenye akili timamu anawezaje kuuliza swali la kijinga na kitoto kama hili ? Hivi huwa unaandika ilimradi tu au upoteze muda ?

Tuambiwe wewe vinawezaje ? Unajua sifa ya kitu chenye uwezo wa kufanya kitu fulani au kutokkufanya lazima kiwe na uwezo, kiwe na maarifa kiwe na akili kiwe na ujuzi bali kiwe na malengo ? Je Dunia ina hizo sifa ?
Kwa nini unadhani dunia na maisha vilipangiliwa?

Hapo hakuna kudhani bali huo ni uhakika sababu ndio uhalisia wenyewe. Ni sawa na useme kwanini unadhani ya kuwa mtoto ni mkubwa kiumri kumzidi baba, huh ni upunguani.
Kama dunia na maisha lazima viwe vimepangiliwa, Je huyo mpangiliaji wa dunia na maisha, Yeye alipangiliwa na nani?

Chanzo Cha kila kitu hakihitaji kupangiliwa. Chenyewe ni kamili.
 
Bila Imani au Dini sidhani kama utapata jibu,maana kwenye Imani au dini ndio kuna jibu lake.
 
Swali: Ukitoa principles zote za kisayansi unazozijua na usizojijua na Ukitoa imani zote za Dini zote unazozijua na usizozijua Je, Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini ?

NB; Uzi huu utawekwa kwenye record za Dunia kwamba ndio uzi pekee uliotaja chanzo cha Dunia, Uhai na ulimwengu bila kutaja principle zozote za Kisayansi au Imani (Dini)

Nawasilisha.
Huwezi kuargue habari za ulimwengu huu bila sayansi.

Labda kama huelewi maana ya science
 
Mleta mada unataka swali lijibiwe na watu wenye mlengo gani?
Unataka watu wa imani za kidini wakujibu au wanasayansi?
 
Unashida ya akili, tuambiwe Sasa imekuwaje mpaka Binadamu akawepo na Ulimwengu ukawepo ?
Tuanze kwa huyo unayesema ni muumba, Yeye ilikuwaje akawepo?

Huyo muumba kabla ya kuumba, alikuwa wapi?

Huko alikokuwa kulitoka wapi?

Usianze kuleta hadithi za kwenye Quran.

Maana hukawii kufanya hivyo.
 
Hili pia unahitaji ushahidi ? Hivi hii mijadala huwa mnajipanga kwa ajili ya ubishi au ? Hivi uwepo wa usiku na mchana ni jambo la Bahati mbaya ? Uwepo wa jua ni jambo limezuka tu ? Kwanini jua lisichomoze Kaskazini na kuzama kusini ?

Huoni misimu ya mvua huoni misimu ya kiangazi ? Hivi vyote vinahitaji ushahidi au uthibitisho gani kwamba vimesukwa na kuwekewa nidhamu maalumu ?


Hivi mtu mwenye akili timamu anawezaje kuuliza swali la kijinga na kitoto kama hili ? Hivi huwa unaandika ilimradi tu au upoteze muda ?

Tuambiwe wewe vinawezaje ? Unajua sifa ya kitu chenye uwezo wa kufanya kitu fulani au kutokkufanya lazima kiwe na uwezo, kiwe na maarifa kiwe na akili kiwe na ujuzi bali kiwe na malengo ? Je Dunia ina hizo sifa ?


Hapo hakuna kudhani bali huo ni uhakika sababu ndio uhalisia wenyewe. Ni sawa na useme kwanini unadhani ya kuwa mtoto ni mkubwa kiumri kumzidi baba, huh ni upunguani.


Chanzo Cha kila kitu hakihitaji kupangiliwa. Chenyewe ni kamili.
Hata ulimwengu ni kamili na hauhitaji, mpangiliaji.

Ulimwengu ni kamili, Hauna chanzo chochote kile.
 
Labda tujadili nadharia sasa..Kila mtu aseme anavyofikiri japo without proof

Ngoja nijarb kwa hii sasa.
1." Maisha si kitu halisi, wote tupo ndotoni na siku moja tutaamka"

2.Japo naweza nisijue imetoka wapi, lkn nguvu ipo na hiyo nguvu inapita ukomo wa nguvu za binadamu, nguvu hiyo ndiyo chanzo cha Maisha.
Ukitoa zote hizo ulizozitaja, then utakuja kwenye kitu kinaitwa "nothingness" - yaani wewe, mimi, na wengine na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana hakuna hata kimoja kilichopo. Na vyote vilivyopo (what we see, hear, smell, taste and feel) are just an illusion. Na katika situation kama hii ndiyo mind inaanza ku'inquire' to know why things are as they are and not anything else? And this inquiry (desire to know) is not in vain.
 
Swali: Ukitoa principles zote za kisayansi unazozijua na usizojijua na Ukitoa imani zote za Dini zote unazozijua na usizozijua Je, Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini ?

NB; Uzi huu utawekwa kwenye record za Dunia kwamba ndio uzi pekee uliotaja chanzo cha Dunia, Uhai na ulimwengu bila kutaja principle zozote za Kisayansi au Imani (Dini)

Nawasilisha.
Ukijua chanzo cha kuku na yai basi utakuwa umejua chanzo cha dunia
 
Naam sio tu kwamba nimesema bali huo ndio uhalisia. Hakuna anaye pinga hili labda mjinga asiye fikiria mambo kwa undani na aliye athiriwa na nadharia za Kisayansi au Falsafa.

Chazo ni Mungu muumba, yeye ndio anajua yalitoka wapi, katika uumbaji upo wa aina tofauti, Kuna uumbaji ule wa Adamu na mama yetu Hawa, Kuna uumbaji unaotokana na sisi kujamiina na Wanawake na Kuna uumbaji wa Mola akisema kitu fulani kiwe na kina kuwa.

Nalijua hilo, sababu mwanadamu ndio kiumbe wa mwisho kuumbwa.
Kama unaamini binadamu aliumbwa. Kwanini sasa usiamini uwepo wa Mungu ni kwa sababu ya uwepo wa nguvu nyingine iliyo mweka hapo?
 
Sio Kila kitu lazima kiwe na mwisho. Mwisho wa kitu unatokana na asili yake, pia vipo ambavyo vinawahi kufikia mwisho kwasababu ya kukiuka asili yake.

Kama kitu asili ya maisha yake ni duara mara nyingi huwa havinaga mwisho Hadi pale vinapokiuka asili zake. Mfano mzuri ni viumbe visivyo hai kama mawe, hewa, maji and they so called mungu
 
Swali: Ukitoa principles zote za kisayansi unazozijua na usizojijua na Ukitoa imani zote za Dini zote unazozijua na usizozijua Je, Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini ?

NB; Uzi huu utawekwa kwenye record za Dunia kwamba ndio uzi pekee uliotaja chanzo cha Dunia, Uhai na ulimwengu bila kutaja principle zozote za Kisayansi au Imani (Dini)

Nawasilisha.
Hapo nani atakua mwenye akili zaidi?Mimi nitakayesahihisha swali au yeye atakayejibu swali?
 
Swali: Ukitoa principles zote za kisayansi unazozijua na usizojijua na Ukitoa imani zote za Dini zote unazozijua na usizozijua Je, Chanzo cha Dunia, Uhai na Ulimwengu ni nini ?

NB; Uzi huu utawekwa kwenye record za Dunia kwamba ndio uzi pekee uliotaja chanzo cha Dunia, Uhai na ulimwengu bila kutaja principle zozote za Kisayansi au Imani (Dini)

Nawasilisha.
Hakuna chanzo
 
Back
Top Bottom