Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

New Rider

Senior Member
Joined
Jun 29, 2021
Posts
122
Reaction score
258
Habari wakuu,

Mwishoni mwa mwaka 1998 na mwanzoni mwa miaka 2000 kuna wanajeshi walienda nchini China kuchukua mafunzo ya ngazi Fulani. Baada ya muda Fulani walirejea nchini, walirudi na vitu mbalimbali ikiwemo zawadi, mmoja kati ya wanajeshi hao ambaye tulikuwa na undugu nae, alirudi na mmea fulani mfano wa chapati kubwa sana yenye rangi nyeupe kijivu, ambayo ilikuwa inawekwa kwenye maji, ndani ya sufuria au bakuli kubwa na kujazwa maji, kisha baada ya kama week tatu au mwezi mmoja unamimina Yale maji yake ambayo huwa yamebadirika rangi na kuwa na rangi kama ya chai ya rangi.

Maji hayo huwa na ladha tamu sana kama uchachu fulani au kama ile ladha ya rosela! Wengine uweka sukari au asali kwa kuongeza ladha zaidi. Chapati hiyo ya Kichina ambayo hukuwa kubwa kadri siku zinavyozidi kwenda mbele, na pia hukuwa na kutoa machapati mengine mengi, kwa mwezi unaweza kuvuna mimea chapati hiyo kama miwili au mitatu. Yaani kimsingi hayo machapati mimea huzaliana kila mwezi au baada ya miezi miwili.

Pia hufa, kwasababu chochote kile kilicho na uhai hufa basi pia mmea huo aina ya chapati hufa, kwasababu huishi ndani ya maji, basi kila baada ya mwezi lazima ubadilishe maji yake na kuongeza mengine! Ukiusahahu na kutokuongeza maji basi mmea huo utaukuta umekauka kabisa na kufa, maji yote yameisha. Mmea huo hula maji tu!

Sasa basi baada ya kupewa mmea chapati huo tulijitahidi kuutunza sana na kufaidi juice yake tamu ambayo pia nasikia ni dawa ya magonjwa kadhaa ya mwili wa mwanadamu, ambayo hutumiwa sana kule China kwa matibabu kadhaa. Kwa bahati mbaya kipindi fulani nnilisafiri kwenda mkoani nikiamini kwamba nitawahi kurudi Dar na kuuhudumia mmea wangu, lakini mambo hayakuwa kama nilivyopanga kwani nilipata dharura na kuchelewa kurudi Dar. Nilipowasili nilikuta ule mmea chapati wangu umeshakauka kabisa kwa kukosa maji na kunyauka kabisa na hatimaye kufa.

Kiukweli nilisikitika sana sana, nimejaribu kuutafuta ule mmea bila mafanikio. Hivyo naomba kama kuna mtu yuko humu Jamiiforums anaufahamu ule mmea, au anao, please naomba sana kwa unyenyekevu anisaidie mbegu yake wanandugu! Naomba sana.

 
Huu mmea sidhani kama una mbegu, kinachofanyika ni kuwa kila unapotanuka ukikata kipande na kutia kwenye maji na chenyewe kinakua, kwahiyo cha muhimu ni kufanya timing kila unapokaribia kucover eneo lote la chombo chako unakata kidogo unatumbukiza kwenye chombo kingine chenye maji. Kifupi sijui kama kuna mbegu na sijui unapatikana wapi, ila hata mimi niliwahi kupewa na rafiki, nikakaa nao karibu miezi 2, nikajisahau ukawa ndio mwisho wake.
 
Huu mmea sidhani kama una mbegu,kinachofanyika ni kuwa kila unapotanuka ukikata kipande na kutia kwenye maji na chenyewe kinakua,kwahiyo cha muhimu ni kufanya timing kila unapokaribia kucover eneo lote la chombo chako unakata kidogo unatumbukiza kwenye chombo kingine chenye maji.Kifupi sijui kama kuna mbegu na sijui unapatikana wapi,ila hata mimi niliwahi kupewa na rafiki,nikakaa nao karibu miezi 2,nikajisahau ukawa ndio mwisho wake...

Eeewaaaa!

Hakika unaufahamu vizuri huu mmea! Ndio huo huo uliouelezea, mbegu yake ndio hiyo hiyo unapotanuka na kuubandua hiyo ndiyo mbegu yake mkuu!

Nilikaa nao karibu miaka 3 au 4 hivi, nilikuwa nauhudumia vizuri sana, na unapozaliana nilikuwa naupunguza na kuzitupa mbegu zake yaani yale mazalia yake.

Lakini sasa nikaja kusafiri na kujichelewa kurudi nikakuta umeshakufa kwa kunyauka, sasa natafuta kama kuna mtu ana huo mmea anisaidie utakapotoa mazalia yake (mbegu).

Shukrani sana!
 
Kwa sisi tuliuita mkate wa Mecca. Miaka ya nyuma wengi waliotoka Hijja walirudi nao, na ukizaa/ totoa unampatia na mwenzio, ukweli ni kwamba mmea ule ulikuwa ni Tiba. Sasa hivi mahujaji wengi waakiridi waanarudi na vitu vya kippuuzi zikiwemo simu na dildo.

Duh!

Kweli ni mmea mzuri sana, kuupata ni adimu sana, nimejitahidi sana kuutafuta humu mtaani bila mafanikio! Nikaona bora nije humu kwa waungwana najua sitakosa hata mawazo ya wapi pa kuupata!

Maana penye wengi hapaharibiki neno!
 
Huu mmea sidhani kama una mbegu,kinachofanyika ni kuwa kila unapotanuka ukikata kipande na kutia kwenye maji na chenyewe kinakua,kwahiyo cha muhimu ni kufanya timing kila unapokaribia kucover eneo lote la chombo chako unakata kidogo unatumbukiza kwenye chombo kingine chenye maji.Kifupi sijui kama kuna mbegu na sijui unapatikana wapi,ila hata mimi niliwahi kupewa na rafiki,nikakaa nao karibu miezi 2,nikajisahau ukawa ndio mwisho wake...
Ulitamba sana kwenye miaka ya mwishoni ya 90'.
Kila mtu akikatia kipande cha ' Fungus' mwenzani ili akaoteshe kwenye maji? Sijui ulipotelea wapi...
 
Ulitamba sana kwenye miaka ya mwishoni ya 90'.
Kila mtu akikatia kipande cha ' Fungus' mwenzani ili akaoteshe kwenye maji? Sijui ulipotelea wapi...

Ni kweli mkuu,
Ni aina fulani ya mimea jamii ya FUNGI , kama uyoga n.k.

Ukikua unaongezeka na kuwa mnene zaidi unaubandua taratibu unapata kipande kidogo unakiweka kwenye chombo kingine chenye maji basi unakuwa taratibu!

Nilikuwa naipenda sana juice yake tamu, inachangamsha sana!
 
Kwa sisi tuliuita mkate wa Mecca. Miaka ya nyuma wengi waliotoka Hijja walirudi nao, na ukizaa/ totoa unampatia na mwenzio, ukweli ni kwamba mmea ule ulikuwa ni Tiba. Sasa hivi mahujaji wengi waakiridi waanarudi na vitu vya kippuuzi zikiwemo simu na dildo.
dildo dah!!
umenichekesha sana mkuu.....
Spanish comedia Juan Joya Borja, known on the Internet as ‘Spanish laughing guy’, has died at the age of 65
 
Umenikumbusha mbali mkuu, nakumbuka mama alikuaga ananipa juice yake, chachu tamu, likawa linazaa chapati nyingine.
Itabidi tukikutana na wachina tuwaulize, hata mimi natamani kujua inapopatikana, nikipata jibu nitakuambia

Swaadaktaaa!!

Juice yake nilikuwa chachu tamuuu kama alozera!

Nalilikuwa linazaa chapati nyenzake kisha unaibandua na kuiweka kwenye chombo kingine chenye maji nayo inaendelea kuzaa na kutoa juice yake!

Juice yake nilikuwa nzuriii ajabu, mpaka leo nahisi ule utamu wake wenye ladha ya ajabu, lilivyokufa kwa kunyauka baada ya kusafiri na kulisahahu bila kuliwekea maji, nilisikitika sana tena sana, mapaka leo nahangaika kulitafuta bila mafanikio mkuu!

Mwenye nalo au taarifa ya mahali lilipo tafadhali tusaidiane maana nahisi kunyong'onyea kwa urahibu wa kulikosa!
 
Back
Top Bottom