Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Swaadaktaaa!!

Juice yake nilikuwa chachu tamuuu kama alozera!

Nalilikuwa linazaa chapati nyenzake kisha unaibandua na kuiweka kwenye chombo kingine chenye maji nayo inaendelea kuzaa na kutoa juice yake!

Juice yake nilikuwa nzuriii ajabu, mpaka leo nahisi ule utamu wake wenye ladha ya ajabu, lilivyokufa kwa kunyauka baada ya kusafiri na kulisahahu bila kuliwekea maji, nilisikitika sana tena sana, mapaka leo nahangaika kulitafuta bila mafanikio mkuu!

Mwenye nalo au taarifa ya mahali lilipo tafadhali tusaidiane maana nahisi kunyong'onyea kwa urahibu wa kulikosa!
Weka hata picha basi nasi tulijue sio maneno mengi tu
 
Tuwekeeni picha basi ili na sisi tuufaidi hata kwa macho tu.

Mmmh! Mkuu, bahati mbaya sikubahatika kuupiga picha wakati bado niko nao!

Pia miaka hiyo simu hazija eneo sana, kama zilikuwepo basi kwa watu wachache sana, nakumbuka simu yangu ya kwanza kumiliki nilikuwa SIEMENS C 25 kubwa kama kipande cha Sabuni enzi hizo tunaziita "MSHINDI" (aina ya sabuni) tena nilikuwa hazina camera! Miaka ya mwanzoni mwa 2000! Kabla ya kumilika NOKIA enzi hizo tunaziita "JENEZA" aha aha haaa! Hatari sana mkuu!

Ingekuwa ninalo sasa mbona tayari picha muda mrefu tu!
 
Weka hata picha basi nasi tulijue sio maneno mengi tu

Picha sina mkuu, ni miaka mingi imepita!

Ningekuwa nayo mbona tayari ningeshaiweka mkuu! Wanasema kuona nikiamini!
Lakini kwa shuhuda za watu hapa nadhani umepata picha japo kidogo. Kama kuna mtu bado analo au hata picha yake basi atusaidie kuiweka itapendeza zaidi.
 
New Rider nahisi unaongelea Kombucha....
220px-Kombucha_Mature.jpg
 
Habari wakuu,

Mwishoni mwa mwaka 1998 na mwanzoni mwa miaka 2000 kuna wanajeshi walienda nchini China kuchukua mafunzo ya ngazi Fulani. Baada ya muda Fulani walirejea nchini, walirudi na vitu mbalimbali ikiwemo zawadi, mmoja kati ya wanajeshi hao ambaye tulikuwa na undugu nae, alirudi na mmea fulani mfano wa chapati kubwa sana yenye rangi nyeupe kijivu, ambayo ilikuwa inawekwa kwenye maji, ndani ya sufuria au bakuli kubwa na kujazwa maji, kisha baada ya kama week tatu au mwezi mmoja unamimina Yale maji yake ambayo huwa yamebadirika rangi na kuwa na rangi kama ya chai ya rangi.

Maji hayo huwa na ladha tamu sana kama uchachu fulani au kama ile ladha ya rosela! Wengine uweka sukari au asali kwa kuongeza ladha zaidi. Chapati hiyo ya Kichina ambayo hukuwa kubwa kadri siku zinavyozidi kwenda mbele, na pia hukuwa na kutoa machapati mengine mengi, kwa mwezi unaweza kuvuna mimea chapati hiyo kama miwili au mitatu. Yaani kimsingi hayo machapati mimea huzaliana kila mwezi au baada ya miezi miwili.

Pia hufa, kwasababu chochote kile kilicho na uhai hufa basi pia mmea huo aina ya chapati hufa, kwasababu huishi ndani ya maji, basi kila baada ya mwezi lazima ubadilishe maji yake na kuongeza mengine! Ukiusahahu na kutokuongeza maji basi mmea huo utaukuta umekauka kabisa na kufa, maji yote yameisha. Mmea huo hula maji tu!

Sasa basi baada ya kupewa mmea chapati huo tulijitahidi kuutunza sana na kufaidi juice yake tamu ambayo pia nasikia ni dawa ya magonjwa kadhaa ya mwili wa mwanadamu, ambayo hutumiwa sana kule China kwa matibabu kadhaa. Kwa bahati mbaya kipindi fulani nnilisafiri kwenda mkoani nikiamini kwamba nitawahi kurudi Dar na kuuhudumia mmea wangu, lakini mambo hayakuwa kama nilivyopanga kwani nilipata dharura na kuchelewa kurudi Dar. Nilipowasili nilikuta ule mmea chapati wangu umeshakauka kabisa kwa kukosa maji na kunyauka kabisa na hatimaye kufa!

Kiukweli nilisikitika sana sana, nimejaribu kuutafuta ule mmea bila mafanikio. Hivyo naomba kama kuna mtu yuko humu Jamiiforums anaufahamu ule mmea, au anao, please naomba sana kwa unyenyekevu anisaidie mbegu yake wanandugu! Naomba sana!
Hii kitu alikuja nayo shangazi kama sio dingi kutoka mkoani mbeya.

Huu mmea hata Tanzania tunao sababu tuna utajiri wa species nyingi sana za mimea.

Ngoja nikutafutie jina na ukipatikana nitashare na ninyi hapa jina na ikibidi tugawane mbegu ni mzuri sana ile kitu tulikuwa tunaigida sana juice yake.

Tuliweka kwenye zaidi ya vyomba sita tukilina maji yake. Alikuja kuharibu bi mkubwa alipookoka akaambiwa na pastor wake kuwa kile kitu ni mapepo na ni maagano ya mizimu. Yule pastor choko sana hadi leo namind kichizi nikimuona natamani nimlabue makofi na mitama maaana ndie alimchanganya bi mkubwa akaona ule m'mea una uhausiano na maswala ya giza na kumbe ni ukosefu tu wa elimu ya mimea na tiba asili.

Bi mkubwa aliyamwaga yale masufuria yote kimya kimya ndo hadi leo sijuagi pa kuupata.
 
Eeewaaaa!!!

Hakika unaufahamu vizuri huu mmea! Ndio huo huo uliouelezea, mbegu yake ndio hiyo hiyo unapotanuka na kuubandua hiyo ndiyo mbegu yake mkuu!

Nilikaa nao karibu miaka 3 au 4 hivi, nilikuwa nauhudumia vizuri sana, na unapozaliana nilikuwa naupunguza na kuzitupa mbegu zake yaani yale mazalia yake.

Lakini sasa nikaja kusafiri na kujichelewa kurudi nikakuta umeshakufa kwa kunyauka, sasa natafuta kama kuna mtu ana huo mmea anisaidie utakapotoa mazalia yake (mbegu).

Shukrani sana!
Ungekuwa unashare na wengine now usingepata shida ya kupata mbegu.
 
Kwa sisi tuliuita mkate wa Mecca. Miaka ya nyuma wengi waliotoka Hijja walirudi nao, na ukizaa/ totoa unampatia na mwenzio, ukweli ni kwamba mmea ule ulikuwa ni Tiba. Sasa hivi mahujaji wengi waakiridi waanarudi na vitu vya kippuuzi zikiwemo simu na dildo.
Kabisa inasikitisha sana. Lishe tiba ni kitu muhimu sana.
 
Swaadaktaaa!!

Juice yake nilikuwa chachu tamuuu kama alozera!

Nalilikuwa linazaa chapati nyenzake kisha unaibandua na kuiweka kwenye chombo kingine chenye maji nayo inaendelea kuzaa na kutoa juice yake!

Juice yake nilikuwa nzuriii ajabu, mpaka leo nahisi ule utamu wake wenye ladha ya ajabu, lilivyokufa kwa kunyauka baada ya kusafiri na kulisahahu bila kuliwekea maji, nilisikitika sana tena sana, mapaka leo nahangaika kulitafuta bila mafanikio mkuu!

Mwenye nalo au taarifa ya mahali lilipo tafadhali tusaidiane maana nahisi kunyong'onyea kwa urahibu wa kulikosa!
Yaan huo mmea nautafuta kwa gharama yoyote, nakumbuka miaka ya 90 mzee alikuwa anatuletea, unatoa juice juice moja nzuri sana ambayo ni dawa na kinga ya maradhi mbali mbali, ni vizuri ukiwa nao ndani na kuizoesha familia kutumia juice yake badala ya kutumia juice za viwandani.
 
Daa zamani sana huo mmea niliuona. Kuna jamaa alikuwa nao kama sikosei alikuwa anauita "mybao/mibao/maibao". Si na hakika na matamshi ya hilo jina ila mnaweza kuanzia hapo. Enzi hizo kila tukimuona jamaa ametoka kazini akiingia tu kwake kabla hajakaa tumeshafika na vikombe vyetu vya plastiki kujimiminia ilikuwa kama chai ya rangi hivi.
 
Back
Top Bottom