Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Habari wakuu,

Mwishoni mwa mwaka 1998 na mwanzoni mwa miaka 2000 kuna wanajeshi walienda nchini China kuchukua mafunzo ya ngazi Fulani. Baada ya muda Fulani walirejea nchini, walirudi na vitu mbalimbali ikiwemo zawadi, mmoja kati ya wanajeshi hao ambaye tulikuwa na undugu nae, alirudi na mmea fulani mfano wa chapati kubwa sana yenye rangi nyeupe kijivu, ambayo ilikuwa inawekwa kwenye maji, ndani ya sufuria au bakuli kubwa na kujazwa maji, kisha baada ya kama week tatu au mwezi mmoja unamimina Yale maji yake ambayo huwa yamebadirika rangi na kuwa na rangi kama ya chai ya rangi.

Maji hayo huwa na ladha tamu sana kama uchachu fulani au kama ile ladha ya rosela! Wengine uweka sukari au asali kwa kuongeza ladha zaidi. Chapati hiyo ya Kichina ambayo hukuwa kubwa kadri siku zinavyozidi kwenda mbele, na pia hukuwa na kutoa machapati mengine mengi, kwa mwezi unaweza kuvuna mimea chapati hiyo kama miwili au mitatu. Yaani kimsingi hayo machapati mimea huzaliana kila mwezi au baada ya miezi miwili.

Pia hufa, kwasababu chochote kile kilicho na uhai hufa basi pia mmea huo aina ya chapati hufa, kwasababu huishi ndani ya maji, basi kila baada ya mwezi lazima ubadilishe maji yake na kuongeza mengine! Ukiusahahu na kutokuongeza maji basi mmea huo utaukuta umekauka kabisa na kufa, maji yote yameisha. Mmea huo hula maji tu!

Sasa basi baada ya kupewa mmea chapati huo tulijitahidi kuutunza sana na kufaidi juice yake tamu ambayo pia nasikia ni dawa ya magonjwa kadhaa ya mwili wa mwanadamu, ambayo hutumiwa sana kule China kwa matibabu kadhaa. Kwa bahati mbaya kipindi fulani nnilisafiri kwenda mkoani nikiamini kwamba nitawahi kurudi Dar na kuuhudumia mmea wangu, lakini mambo hayakuwa kama nilivyopanga kwani nilipata dharura na kuchelewa kurudi Dar. Nilipowasili nilikuta ule mmea chapati wangu umeshakauka kabisa kwa kukosa maji na kunyauka kabisa na hatimaye kufa!

Kiukweli nilisikitika sana sana, nimejaribu kuutafuta ule mmea bila mafanikio. Hivyo naomba kama kuna mtu yuko humu Jamiiforums anaufahamu ule mmea, au anao, please naomba sana kwa unyenyekevu anisaidie mbegu yake wanandugu! Naomba sana
Mimi nilitafutaga sana kipindi fulani ila nikakosa. Watoto wa elifu mbili hawajui hii kitu
 
Unaitwaje kwa English ni google naona mmeshindwa kuweka picha

Mkuu, sifahamu unaitwaje kwa kiingereza, lakini kuna mdau hapa kanikumbusha jina moja nadhani ni la kiswahili "kombucha" nakumbuka pia hilo jina!
 
Hii kitu alikuja nayo shangazi kama sio dingi kutoka mkoani mbeya.

Huu mmea hata Tanzania tunao sababu tuna utajiri wa species nyingi sana za mimea.

Ngoja nikutafutie jina na ukipatikana nitashare na ninyi hapa jina na ikibidi tugawane mbegu ni mzuri sana ile kitu tulikuwa tunaigida sana juice yake.

Tuliweka kwenye zaidi ya vyomba sita tukilina maji yake. Alikuja kuharibu bi mkubwa alipookoka akaambiwa na pastor wake kuwa kile kitu ni mapepo na ni maagano ya mizimu. Yule pastor choko sana hadi leo namind kichizi nikimuona natamani nimlabue makofi na mitama maaana ndie alimchanganya bi mkubwa akaona ule m'mea una uhausiano na maswala ya giza na kumbe ni ukosefu tu wa elimu ya mimea na tiba asili.

Bi mkubwa aliyamwaga yale masufuria yote kimya kimya ndo hadi leo sijuagi pa kuupata.

Dah, aha aha haaa!

Pole sana mkuu, inachekesha lakini pia inafurahisha!

Ni kweli hata Mimi kuna wakati lile lichapati lililopokuwa linazaa nilikuwa natenga masufuria mengine na mabakuli makubwa kama yakunawia mikono nayaweka hayo machapati mimea humo! Basi bi.makubwa akawa ana mind sana! Analalamika,"sasa wewe unataka kugeuza vyombo vyote kuwa vya kuwekea hilo lidude lako?!" Alafu sisi tutapikia wapi?!" aha ha haaa! ilikuwa zahama!

Ule mmea ulikuwa mzuri sana aisee,,, mpaka leo nautafuta lakini bado sijaupata!

Mwenye nao tunaomba wandugu!
 
Ungekuwa unashare na wengine now usingepata shida ya kupata mbegu.

Mkuu, tatizo miaka ile ya katikati mwa 1990, watu wengi walikuwa hawaujui huu mmea, mengine walikuwa hata wana uogopa! Wengine wanauonea kinyaa! Na mengine mpaka wanadiriki kuuita ni mambo ya kishirikina!(kichawi).

Kwahiyo kumpa mtu ambaye anauhisi labda ni mambo ya kishirikina sio rahisi mkuu, sisi zile mbegu zake tulikuwa tunafukia chini, tunachimbia shambani.
 
Yaan huo mmea nautafuta kwa gharama yoyote, nakumbuka miaka ya 90 mzee alikuwa anatuletea, unatoa juice juice moja nzuri sana ambayo ni dawa na kinga ya maradhi mbali mbali, ni vizuri ukiwa nao ndani na kuizoesha familia kutumia juice yake badala ya kutumia juice za viwandani.

Kabisa mkuu!

Ukiwa na huu mmea, hata magonjwa ya ajabu ajabu hayakupati kirahisi, unasaidia ku-boost kinga mwili na pia unasaidia mfumo wa usagikaji wa chakula digestion.
 
Unaitwa KOMBUCHA nakumbuka enzi hizo tumeinywa sana juice yake kwa Bibi hukoooo Marangu. Aisee umenikumbusha mbali sana


Kombucha (also tea mushroom, tea fungus, or Manchurian mushroom when referring to the culture; Latin name Medusomyces gisevii[1]) is a fermented, lightly effervescent, sweetened black or green tea drink commonly consumed for its purported health benefits. Sometimes the beverage is called kombucha tea to distinguish it from the culture of bacteria and yeast.[2] Juice, spices, fruit or other flavorings are often added.


Kombucha
 
Dah, aha aha haaa!

Pole sana mkuu, inachekesha lakini pia inafurahisha!

Ni kweli hata Mimi kuna wakati lile lichapati lililopokuwa linazaa nilikuwa natenga masufuria mengine na mabakuli makubwa kama yakunawia mikono nayaweka hayo machapati mimea humo! Basi bi.makubwa akawa ana mind sana! Analalamika,"sasa wewe unataka kugeuza vyombo vyote kuwa vya kuwekea hilo lidude lako?!" Alafu sisi tutapikia wapi?!" aha ha haaa! ilikuwa zahama!

Ule mmea ulikuwa mzuri sana aisee,,, mpaka leo nautafuta lakini bado sijaupata!

Mwenye nao tunaomba wandugu!
Sifa ya kukaa na ule m'mea ni kushare na wengine usiposhare unakuwa unaukosea.

Unatakiwa uwe unawakatia watu na kuwagawia usambae. Ni m'mea ambao hautakiwi kumchaji mtu kuupata.
 
Unaitwa KOMBUCHA nakumbuka enzi hizo tumeinywa sana juice yake kwa Bibi hukoooo Marangu. Aisee umenikumbusha mbali sana


Kombucha (also tea mushroom, tea fungus, or Manchurian mushroom when referring to the culture; Latin name Medusomyces gisevii[1]) is a fermented, lightly effervescent, sweetened black or green tea drink commonly consumed for its purported health benefits. Sometimes the beverage is called kombucha tea to distinguish it from the culture of bacteria and yeast.[2] Juice, spices, fruit or other flavorings are often added.


Kombucha

Ni kweli mkuu,


Kama unao au ukisikia mtu anao tujulishane ndugu yangu!
 
Sifa ya kukaa na ule m'mea ni kushare na wengine usiposhare unakuwa unaukosea.

Unatakiwa uwe unawakatia watu na kuwagawia usambae. Ni m'mea ambao hautakiwi kumchaji mtu kuupata.

Ni kweli kabisa,

Lakini miaka ile watu wengi walikuwa hawaujui huu mmea, na mengine walikuwa wanauogopa hata kuuhusisha na ulozi.
Hivyo inakuwa ngumu kumpa mtu. Kwasasa nadhani wengi wanaufahamu hivyo kuwa rahisi kushare!
 
Huu mmea uliwahi kuniponya Athma nikiwa binti mdogo...Nilikuwa nikibanwa Mara kwa Mara na kutumia vidonge vya hospital na zile dawa za ku inhale lakini Mambo yalikuwa mperampera, Kama kawaida ya Tanzania Mambo ya milipuko Ni mengi,Mara Ngetwa3,Mara Ngoka11,Mara mayai ya kwale,Mara Kikombe Cha Mwaisapile...Basi ikatokea hili lichapati ,hii kitu nilikunywa Kama miezi miwili Nakumbuka mama yangu aliyapanda kwenye madishi,Basi nakunywa Kama juisi daily....ninachokumbuka baada ya hapo sijabanwa Tena kifua mpaka Sasa nimezeeka....Ila linachefua ukiliona Kama miutelezi gani sijui🥴
 
Back
Top Bottom