Charles Kimei: Serikali itakuwa tayari kurejesha Kodi iliyokusanywa kwa shinikizo? Mwigulu amjibu

Charles Kimei: Serikali itakuwa tayari kurejesha Kodi iliyokusanywa kwa shinikizo? Mwigulu amjibu

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Bungeni, Mbunge wa Vunjo ameuliza swali lililoanzia kwenye misamaha ya kodi kwenye taasisi za dini ambapo Waziri Mwigulu alisema Taasisi za dini zinazofanya shughuli za kiuchumi kwa lengo la kujipatia faida zinatakiwa kusajiliwa na TRA kama wafanyabiashara wengine na kulipa kodi ya mapato kulingana na faida inavyopatikana.

Pia waziri Mwigulu amesema Serikali imekuwa ikipokea maombi ya kusamehe kodi za miaka ya nyuma na ianaendelea kutathmini maombi hayo kuona hatua zinazoweza kuchukuliwa bila kuathiri sheria zilizopo.

Baada ya hapo Kimei aliuliza swali la Nyongeza

Dkt. Charles Kimei: Nampongeza waziri kwa kutoa majibu mazuri yanayotoa faraja sana kwa wanaoendesha shughuli hizo. Serikali itakuwa tayari kurejesha kodi iliyokusanywa kutoka kwenye taasisi hizo kwa shinikizo na hatimaye kuzidhoofisha sana? Pili Serikali iko tayari kuchukua hatua za kinidhamu kwa maofisa wa TRA wanaokiuka sheria?

Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba: Serikali ina utaratibu wa kerejesha fedha ambazo zilichukuliwa kwa mujibu wa sheria zinatakiwa kurejeshwa kwa utaratibu ulio wa kawaida wa kufanya refund.

Kwa maeneo ambayo kuna ukiukwaji wa kisheria, taratibu za kisheria huwa zinafuatwa na hatua stahiki za kinidhau kuchukuliwa kwa wale wanaokiuka sheria.

 
Serikali inatakiwa kuwekwa under intense pressure warudishe pesa walizopora wafanyabiashara awamu iliyopita, kama wakishindwa kufanya hivyo, basi hizo pesa wakatane kidogo kidogo kwenye kodi watakazotakiwa kulipa hao wafanyabiashara mpaka kiasi kilichoporwa kitimie.
 
Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba: Serikali ina utaratibu wa kerejesha fedha ambazo zilichukuliwa kwa mujibu wa sheria zinatakiwa kurejeshwa kwa utaratibu ulio wa kawaida wa kufanya refund.

Kwa maeneo ambayo kuna ukiukwaji wa kisheria, taratibu za kisheria huwa zinafuatwa na hatua stahiki za kinidhau kuchukuliwa kwa wale wanaokiuka sheria.
Ina maana Kimei hayajui haya? Au waziri amekwepa kinamna swali halisi la KImei?
 
Leo Bungeni, Mbunge wa Vunjo ameuliza swali lililoanzia kwenye misamaha ya kodi kwenye taasisi za dini ambapo Waziri Mwigulu alisema Taasisi za dini zinazofanya shughuli za kiuchumi kwa lengo la kujipatia faida zinatakiwa kusajiliwa na TRA kama wafanyabiashara wengine na kulipa kodi ya mapato kulingana na faida inavyopatikana...
Kimei anauliza maswali mepesi level ya msukuma au kibaji
 
Serikali inatakiwa kuwekwa under intense pressure warudishe pesa walizopora wafanyabiashara awamu iliyopita, kama wakishindwa kufanya hivyo, basi hizo pesa wakatane kidogo kidogo kwenye kodi watakazotakiwa kulipa hao wafanyabiashara mpaka kiasi kilichoporwa kitimie.
... na kwa zile biashara zilizofilisika baada ya kubambikwa kodi za kiuonevu?
 
Serikali inatakiwa kuwekwa under intense pressure warudishe pesa walizopora wafanyabiashara awamu iliyopita, kama wakishindwa kufanya hivyo, basi hizo pesa wakatane kidogo kidogo kwenye kodi watakazotakiwa kulipa hao wafanyabiashara mpaka kiasi kilichoporwa kitimie.
Kiendacho kwa mganga hakirudi mkuu
 
Kwa hiyo wamekubali kwa kauli moja kwamba marehemu alikwapua fedha za watu bila kufuata sheria eee!! hii nchi ilikuwa inaelekea kubaya aisee
 
Mwisho wao ni Bunge hili la Bajeti. Baada ya hapo Mama atasuka Baraza jipya la Mawaziri.
Msimuwekee mama maneno mdomoni. Muacheni aamue anavyotaka. Ni kweli wapo wanaopwaya. Wapo wenye mazoea. Ila sio kila siku kuchagua na kutengua. Kazi zitafanyika lini?
 
Huyu kibaraka katili toka kwa Mwendazake amepewa madaraka yanayomzidi kimo.
nami nilishangaa kusikia ameteuliwa waziri wa fedha, hii nchi ina vituko sana, huyu alikuwa hastahili kabisa kuwa waziri na yeye analijua hilo
 
Mwisho wao ni Bunge hili la Bajeti. Baada ya hapo Mama atasuka Baraza jipya la Mawaziri.
Tatizo ni kwamba wakati wa uundaji wa serikali huwa kuna kubalance mikoa. Yaani at least kila mkoa awepo waziri.

So, ukiangalia Singida hao ndio wanasiasa wakubwa waliopo.

  • Mwigulu
  • Mkumbo ( Ingizo jipya )

Hata Shonza alikuwa anapitia mbinu hii kupata Unaibu Waziri, maana ndiye aliyekuwa mwanasiasa anayefahamika huko Songwe japo sasa hivi wameingia kwenye ushindani na Selasini.
 
Back
Top Bottom