ChatGPT imetimiza unabii uliotolewa takriban miaka 2500 iliyopita!!

ChatGPT imetimiza unabii uliotolewa takriban miaka 2500 iliyopita!!

Mstari mzima unasema "watu wataenda mbio huku na huko na maarifa yataongezeka." Leo hii watu wanaenda mbio sana kwa magari na kwa ndege, huwezi kamwe kulinganisha mbio za leo na za wakati ule. Hivyo ni dhahiri wakati unaozungumwa ni huu, sio kabla ya miaka 2500.
Sawa, sikatai. ila na mimi nauliza, nisiulize sasa?!

Kipindi cha Kuanzia Miaka 2500 kabla ya kutolewa unabii hadi siku ya kutolewa unabii, maarifa yaliongezeka au yalipungua?
 
Sawa, sikatai. ila na mimi nauliza, nisiulize sasa?!

Kipindi cha Kuanzia Miaka 2500 kabla ya kutolewa unabii hadi siku ya kutolewa unabii, maarifa yaliongezeka au yalipungua?
Yaliongezeka lakini watu hawakuenda mbio. Hivyo hoja yako haikanushi unabii huo
 
Hakuna lolote. We waishangaa chatgpt kwa sababu mengine umeyakuta. Wewe wadhan watu wa zama za miaka ya 60 walioanaje uvumbuzi wa computer?

Mara ya kwanza kujua uwepo wa Google, nilikuwa nashangaa nasearch kitu inaniletea majibu niliona ni kitu kimoja amazing sana.

So chagpt ni uvumbuzi tu wa kawaida sema ni exciting kwa sababu ni uvumbuzi mpya.
Vip kuhusu waliogundua umeme? Vipi kuhusu waliogundua engine? ChatGpt naona kama hata sio uvumbuzi mpya bali mwendelezo tu wa tekonolia ya computer
 
Yaliongezeka lakini watu hawakuenda mbio. Hivyo hoja yako haikanushi unabii huo
Sasa kama yalikuwa yanaongezeka kipindi hicho maana yake nusu ya utabiri huo tayari sio utabiri. Haya tuendeleee..

Kipindi utabiri unatolewa, watu walikuwa wanakimbia mbio kwa speed ipi, na hivi leo watu wanaenda mbio kwa speed ipi? (In km/hr)..?
 
Vip kuhusu waliogundua umeme? Vipi kuhusu waliogundua engine? ChatGpt naona kama hata sio uvumbuzi mpya bali mwendelezo tu wa tekonolia ya computer
Nimeishasema, nimeitaja chatGPT kwa kuwa ni habari ya mjini kwa sasa. Lakini chatGPT ni sehemu tu ya ongezeko kubwa la maarifa katika nyanja mbalimbali. Hivyo kugunduliwa kwa umeme na engine, yote hayo bado yanatimiza huo unabii maana hayakuwepo hayo wakati unabii unatolewa.
 
Sasa kama yalikuwa yanaongezeka kipindi hicho maana yake nusu ya utabiri huo tayari sio utabiri. Haya tuendeleee..

Kipindi utabiri unatolewa, watu walikuwa wanakimbia mbio kwa speed ipi, na hivi leo watu wanaenda mbio kwa speed ipi? (In km/hr)..?
Usiwe mvivu. Muulize chatGPT atakuambia Speed ya farasi(usafiri wa mbio wa wakati ule na ndege/airplane usafiri wa mbio wa sasa)
 
Sasa kama yalikuwa yanaongezeka kipindi hicho maana yake nusu ya utabiri huo tayari sio utabiri.
Ngoja nikupe elimu zaidi. Kuongezeka kwa maarifa ni sehemu tu ya ishara na dalili nyingi zilizotabiriwa kuwa zitatokea kabla ya kurudi kwa Yesu na mwisho wa dunia. Soma dalili nyingine zilizotimia katika Mathayo 24.

Sasa Maandiko yanasema: Mt 24:33 SUV "nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni."
 
Miaka takriban 2500 iliyopita, Mungu alimwambia Nabii Danieli awaambie watu kuwa wakati wa mwisho maarifa yataongezeka. Tunasoma hivyo katika kitabu cha Danieli 12:4: "Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie mhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huku na huko, na maarifa yataongezeka."

Leo, tunaona wazi kutimia kwa unabii huo kupitia maendeleo makubwa ya teknolojia, hasa katika Akili Mnemba. Zamani, maarifa yalihifadhiwa katika vitabu na kupatikana polepole, lakini sasa, kwa sekunde chache tu, mtu anaweza kupata maarifa na taarifa nyingi kwa njia ya mitandao, AI, na mifumo ya kisasa ya kompyuta. Akili Mnemba si tu kwamba inachakata taarifa haraka, bali pia inajifunza, inafikiri, na hata kusaidia kufanya maamuzi magumu. Ni dhahiri, maarifa yameongezeka kama ilivyotabiriwa.

Kuongezeka kwa maarifa ni moja ya dalili za siku za mwisho. Katika Mathayo 24:3-14, Yesu alieleza ishara na dalili nyingine zitakazotokea kabla ya kuja kwake na kabla ya mwisho wa dunia. Dalili na ishara hizo karibu zote zimeishatimia. Huu ni uthibitisho wa wazi kuwa Biblia ni kitabu cha kuaminika. Kwa wanaoamini kitabu hiki, kuongezeka huku kwa maarifa ni maonyo kwamba nyakati tulizo nazo si za kawaida. Huu ni wakati wa kuwa macho, ni wakati wa kujiandaa kiroho, na kusimama imara kwa Mungu, kwa kuwa siku ya kurudi kwa Yesu imekaribia!

Ibilisi anajua wakati uliobaki ni mchache(Ufunuo 12:12), kwa sababu hiyo anafanya kila jitihada kuwashawishi watu wasiamini kuwa Mungu yupo. Anatumia mbinu nyingi kuwashawishi watu wazame katika matendo ya dhambi kama ushoga, uzinzi, ulevi, wizi, uongo nk, ili siku hiyo ikifika waachwe, maana Yesu akirudi atawachukua na kuwapeleka mbinguni wale tu waliotubu dhambi zao na kumwamini Yesu. Watakaoachwa watabaki katika dhiki kuu ambayo haijawahi kuwepo tangu kuumbwa kwa ulimwengu(Mathayo 24:21); na hatimaye siku ya mwisho wote wasioamini watatupwa pamoja na Ibilisi katika moto wa milele(Mathayo 25:41).

Wimbo huu na picha hizi zimetengenezwa kwa msaada wa chatGPT/AI
View attachment 3235549 View attachment 3235550View attachment 3235551View attachment 3235552View attachment 3235553
Kijana kwako chatgpt ndio umeona ndio kiwango cha juu sana cha maendeleo?
 
Ngoja nikupe elimu zaidi. Kuongezeka kwa maarifa ni sehemu tu ya ishara na dalili nyingi zilizotabiriwa kuwa zitatokea kabla ya kurudi kwa Yesu na mwisho wa dunia. Soma dalili nyingine zilizotimia katika Mathayo 24.

Sasa Maandiko yanasema: Mt 24:33 SUV "nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni."
Haya yalianza jadiliwa kabla kristo, kila jambo jipya duniani binadamu hutahayari na kuona sasa maandiko yatatimia, siku yatakapo timia ndipo mtakumbuka maandiko, ila sio mkumbuke maandiko ndio itimie
 
Yani umri huu bado unaamini kwenye hekaya za watu WA jangwani😂😂😂
 
Nipe habari ww unayeijua mbinguni
Soma Biblia kitabu cha Mwanzo hadi Ufunuo. Kwa ufupi, mbinguni hakuna kuugua, hakuna kulia, hakuna njaa, siku 1000 ni sawa na siku moja, hakuna giza, hakuna vita, hakuna kifo nk nk nk nk nk nk
 
Hakuna lolote Ka maana kikawaida ni kwamba kila technology mpya inapo gundulika huwa ni kama Miujiza lakini yote watu tulikuwa hatufahamu Hicho kitu
 
Hakuna lolote
Sawa. Hata wakati wa Nuhu watu waliambiwa gharika itakuja wakapuuza. Mimi nimeishatoa onyo huu ni wakati wa mwisho
Mit 29:1-14 SUV
Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.
 
Haya mambo ya siku za mwisho ni hadithi za kutungwa na wahuni fulani
 
Sio lazima iwe hivyo. Tangu ulipoanza kula chumvi imepita miaka mingapi. Kuna chumvi mpya umeiona
Hili swali ni sawa na kuniuliza kama nimeona aina mpya ya maji tofauti na yaliyopo.

Ila kwa umro nilionao nmeyaona mabadiliko mengi ya kiteknolojia na hata hapa tulipo sio mwisho wa ujio wa teknolojia mpya.

Sawa na watu walioishi kipindi ambacho hapakuwa na radio, ujio wa radio ilionekana kama jambo la kistaajabisha sana, iweje mtu aongee kwenye vipande vya nyaya na vibatii?, ndio sawa na sisi tunavyoiwaza AI na utendaji kazi wake.
 
Back
Top Bottom