Chato: Kijiji kilichokaribia kuwa makao makuu ya mkoa-2

Watu walitabili, lakini utabili ukatimia kabla hata mizizi haijaota
 
Nipo Chato yaliyoandikwa hapa nikweli tupu kuna watu walikuwa na viwanja vyao wakazingua wanataka mamilioni sahivi wanalia bora wangeuza wakati huo kwa sasa wanakubembeleza hata laki 5 uchukuwe kiwanja. Maisha haya balaa sana
 
Haya yote ni sehemu ndogo tu ya maovu, ukatili, ufisadi, ubadhirifu, hasara, wendawazimu na ubovu wake.

Nawashukuru na kuwapongeza waandishi na wachapishaji kwa uzalendo wao.
Niwaombe na kuwatia moyo wengine kujitokeza na kuueleza umma yaliyokuwa yakijiri gizani. Lazima ukweli ujulikane na haki itendeke, ili tusijerudi tena huko asilan!

Kwa wale watetezi wa "legacy ya Kishetani " na mashabiki wa Mwendazake, ambao hujietetea kusema "...mbona tuhuma hizi/zinaletwa sasa.....kwa nini zisingetolewa alipokuwa hai ili "
'azijibu au kujitetea'....". Utetezi huo ni wa kipumbavu na wa kinafiki - hivi kuna mtu yeyote aliyepingana na dikteta hadharani, iwe kimawazo au kimatendo akabaki halafu salama? Mwendazake majibu na utetezi wake si ulijulikana waziwazi na kushagiliwa na "wanyonge" - kuua, kufilisi, kutesa, kufunga???

Je damu, maumivu, ulemavu na ukatili, hasara nk waliofanyiwa "wapinzani" wake hamkuviona wala kusikia?? Ukweli mnaujua na siku moja mtakiri mbele za Mola wetu.

Pamoja na hayo, budi sasa mjiandae kusikia na kuona bila chenga authentic 'replay' ya aliyoyatenda "shujaa" wenu dhalim Magufuli kwa HDV.
Tena haya ni mwanzo tu. Kuna mengi mno, tena ya kutisha tutaendelea kuhabirishwa siku na miaka ijayo.
 
Chato=Gbadolite.Ni kweli alitaka aendeleze kwao kama Mkwere alivyotaka kuendeleza kwao lkn angalia na mazingira kwanza kabla ya kutupa shilingi ikiwa mradi husika utadumu au ukiondoka nao umekufa.By the way Mzilankende alijua ana muda mrefu ila bahat mbaya muda wake ulikuwa ukingoni.Nilichokuwa naogopa ni kukaa siku moja nikijua mtu atatawala daima milele baada ya kutengua katiba hii kitu ilikuwa inaniumiza sana kichwa
 
Wapi kinapatikana kitabu hiki?

Kumbukeni na mm nakaribia kutoa kitabu changu kiitwacho "MAGUFULI, The Master of Chaos".
Kila la heri.

Pamoja na utangulizi msisahau kutujulishs vitabu venu vitakapokuwa vinapatikana, home and abroad.
 
Nipo Chato yaliyoandikwa hapa nikweli tupu kuna watu walikuwa na viwanja vyao wakazingua wanataka mamilioni sahivi wanalia bora wangeuza wakati huo kwa sasa wanakubembeleza hata laki 5 uchukuwe kiwanja. Maisha haya balaa sana
Asante kwa kutupa ushahidi.
 
Kama Nyerere angekuwa na ubinafsi kama wa huyu mwamba wa chato basi musoma ingekuwa Jiji la pili kwa ukubwa baada ya dar.Tena Kuna mbuga ya wanyama ya Serengeti sio ile ya kutengeneza burigi chato.ila mzee wa watu hakuwa na makuu kabisa
Tukiuliza kwani kilifanyika nini chato kikubwa? Utasikia watu wazima wanalalamikia taa za barabarani! Ujenzi wa CRDB, uwanja wa mpira! Mambo ya kijinga kabisa as if kama sehemu nyingine hamna!
 
Pole kwa hilo; yaani hata mimi lilinisumbua hasa kati ya 2017/2018, nilifuatilia kauli na matendo yake wakati wa kampeni 2020 na alionyesha kiburi na jeuri hatari sana; baada tu ya uchaguzi wa 2020, nilipata majibu yaliyonipa amani sana. Nakumbuka nilitamka "Magufuli kafanya yake, lakini si lazima kwamba atamaliza huu mhula" - Maana niliona jinsi alivyovuka mstari mwekundu wa uovu, na hakujali kabisa. Nilihisi na kuamini 100% kwamba sasa Magufuli alijiweka rasmi ulingoni dhidi ya Mwenyezi Mungu. Kiburi na tamaa zake vilimfikisha kwenye 'point of no return'. Kuanzia pale ilikuwa ni kuhesabu tu siku na saa - Litimie.

::By the way; huwa iko hivyo hata kwenye maisha ya kawaida tu ya watu. Ukichunguza (observe) utaona, huwa kuna downward patterns ambazo baadaye huwa trends....halafu - The End.

"Ushujaa" na ujasiri wake ulikuwa wa Kishetani kabisa. Wengine tutaendelea kumshukuru Mwenyezi MUNGU kila tunapokumbuka haya.
 
Hii kauli aliongea Dr Kimei mwenyewe siku ya ufunguzi nakumbuka
 
Naomba kuuliza Tangu lini kijiji kikawa na watu zaidi ya laki 5?
 
Upotoshaji upotoshaji, Watanzania wana haki ya kupewa maelezo sahihi. Sehemu ya kwanza ya kuchumi kudorora kuna mambo 3 hayasemwi. La kwanza ni Covid-19 ya 2019/2020 hii inajibu kila kitu. Marehemu "Dikteta" alikataa kuifunga Nchi, hatukuumia kama walivyoumia almost dunia nzima. He was a Visionary, more so than Trump, or the EU, or WHO, dunia nzima. Na kuna sala tulifunga kwa kuongozwa na Mufti na Askofu Malasusa na Askofu Ruwaichi kwa pamoja, umoja huo haujawahi kuonekana hapa duniani.

Imetajwa benki ya CRDB sababu za kipuuzi tu. Maendeleo huletwa na uwepo wa benki, hasa kama ni za umma, siyo benki kupelekwa kwenye maendeleo tayari. Hili Dr Kimei analijua, na ndivyo alivyosema, Wahariri kwa wametumbukiza maneno yao mdomoni mwake kwa sababu zao.

Jiulize NBC: hii 1997 ilipobinafsishwa, matawi mazuri yaliyokuwa mijini yalinyofolewa wakapewa makaburu almost for free. NBC wakaitafuna, sasa angalia NBC iko wapi? Yale matawi ya hasara yemekaa kama Chatochato yalimegwa ikapewa NMB mpya, benki ya makabwela. Leo NMB ndiyo benki kubwa inayoongoza Tanzania, how do you explain that?

NBC ilikuwa iende DSE kama mashirika mengine TBL, TCC, TOL, nk, wanunue Watanzania, lakini hadi leo makaburu wamekataa kuipeleka DSE kwa makusudi kabisa, inatumiwa kama conduit ya hela zao tu.

Pia imetajwa benki moja eti "mbovu" - ya Twiga Bancorp. Hii si mbovu hata kidogo, it was the best bank in the NBC system kwa sababu ndiyo pekee iliyokuwa na forex wakati mgumu tulipokuwa Nchi haina hela za kigeni. Ilikuwa ichukukiwe na makaburu pamoja na NBC lakini ni Wazalendo hawa hawa kina Dr Kimei wakaona ukweli huu ikanyofolewa NBC haraka haraka kabla haijauzwa. Hilo nalo halisemwi, Magufuli wala hahusiki.

Benki zingine ikiwamo ya Wanawake ni za tangu zamani, na hizo zingine zililemewa na Covid, si za Magufuli.

Umetajwa pia mradi wa hoteli ya Burigi Chato, hii tatizo lake pekee lilikuwa Covid mapato ya Utalii kupungua, si ya Magufuli. Mbuga za wanyama magharibi ya Ziwa toka Kyerwa Ibanda hadi Rubondo na Chato ni nzuri mno, uamuzi wa kuzikwamua haukuwa wa Magufuli ni bahati mbaya tu ukakunbwa na Covid.

Huo "utafiti" wa Wahariri ni sawa na zero, sijui ni nani aliyewalipa kutunga hadithi hizo za kitoto.

Naomba wasomaji haya wayatafakari kabla hatujaja "utafiti" wa Chato kama Chato.
 
Mmeshauza nakala ngapi za hicho kigazeti chenu? Jaribuni kugawa bure kina mama wapate karatasi za kufungia maandazi
 
Tukiuliza kwani kilifanyika nini chato kikubwa? Utasikia watu wazima wanalalamikia taa za barabarani! Ujenzi wa CRDB, uwanja wa mpira! Mambo ya kijinga kabisa as if kama sehemu nyingine hamna!
Sio kwamba havipo sehemu zingine ila sehemu vipojengwa ndio shida,hivi unaonaje tukijenga shule katikati ya mbuga ya wanyama.will it be useful? Yani uwanja wa ndege wa kimataifa kijijini chato ambapo hakuna kivutio chochote Wala shughuli za kiuchumi,really?

Sent from my Infinix X665B using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ