Chato: Kijiji kilichokaribia kuwa makao makuu ya mkoa-2

Chato: Kijiji kilichokaribia kuwa makao makuu ya mkoa-2

Upotoshaji upotoshaji, Watanzania wana haki ya kupewa maelezo sahihi. Sehemu ya kwanza ya kuchumi kudorora kuna mambo 3 hayasemwi. La kwanza ni Covid-19 ya 2019/2020 hii inajibu kila kitu. Marehemu "Dikteta" alikataa kuifunga Nchi, hatukuumia kama walivyoumia almost dunia nzima. He was a Visionary, more so than Trump, or the EU, or WHO, dunia nzima. Na kuna sala tulifunga kwa kuongozwa na Mufti na Askofu Malasusa na Askofu Ruwaichi kwa pamoja, umoja huo haujawahi kuonekana hapa duniani.

Imetajwa benki ya CRDB sababu za kipuuzi tu. Maendeleo huletwa na uwepo wa benki, hasa kama ni za umma, siyo benki kupelekwa kwenye maendeleo tayari. Hili Dr Kimei analijua, na ndivyo alivyosema, Wahariri kwa wametumbukiza maneno yao mdomoni mwake kwa sababu zao.

Jiulize NBC: hii 1997 ilipobinafsishwa, matawi mazuri yaliyokuwa mijini yalinyofolewa wakapewa makaburu almost for free. NBC wakaitafuna, sasa angalia NBC iko wapi? Yale matawi ya hasara yemekaa kama Chatochato yalimegwa ikapewa NMB mpya, benki ya makabwela. Leo NMB ndiyo benki kubwa inayoongoza Tanzania, how do you explain that?

NBC ilikuwa iende DSE kama mashirika mengine TBL, TCC, TOL, nk, wanunue Watanzania, lakini hadi leo makaburu wamekataa kuipeleka DSE kwa makusudi kabisa, inatumiwa kama conduit ya hela zao tu.

Pia imetajwa benki moja eti "mbovu" - ya Twiga Bancorp. Hii si mbovu hata kidogo, it was the best bank in the NBC system kwa sababu ndiyo pekee iliyokuwa na forex wakati mgumu tulipokuwa Nchi haina hela za kigeni. Ilikuwa ichukukiwe na makaburu pamoja na NBC lakini ni Wazalendo hawa hawa kina Dr Kimei wakaona ukweli huu ikanyofolewa NBC haraka haraka kabla haijauzwa. Hilo nalo halisemwi, Magufuli wala hahusiki.

Benki zingine ikiwamo ya Wanawake ni za tangu zamani, na hizo zingine zililemewa na Covid, si za Magufuli.

Umetajwa pia mradi wa hoteli ya Burigi Chato, hii tatizo lake pekee lilikuwa Covid mapato ya Utalii kupungua, si ya Magufuli. Mbuga za wanyama magharibi ya Ziwa toka Kyerwa Ibanda hadi Rubondo na Chato ni nzuri mno, uamuzi wa kuzikwamua haukuwa wa Magufuli ni bahati mbaya tu ukakunbwa na Covid.

Huo "utafiti" wa Wahariri ni sawa na zero, sijui ni nani aliyewalipa kutunga hadithi hizo za kitoto.

Naomba wasomaji haya wayatafakari kabla hatujaja "utafiti" wa Chato kama Chato.
Kumtetea Magufuli ni jambo gumu na linahitaji propaganda sana. Hatuhitaji kuwa mtaalamu wa uchumi kujua kuwa Magufuli alifanya ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma alifanya miradi mikubwa bila utafiti wa kutosha au ridhaa ya bunge. Miradi ya Chato ilikuwa ya kwake binafsi ipo mingi; uwanja wa ndege, mahoteli, mbuga ya wanyama, etc. Uthibitisho wa miradi hii kuwa ililazimishwa bila kufuata market demand, ni kwamba miradi hii yote imekufa! Hili sio tatizo la covid.

Magufuli alikuwa the wrong president aliharibu uhuru wa kujieleza, watu waliporwa mali zao kibabe, uchaguzi mkuu ulivurugwa vibaya kuwahi kutokea barani Afrika. watu wameumizwa na kuuwawa. Utamdanganya nani kwamba haya yote ni kwasababu ya covid? Magufuli was a catastrophe for our country!
 
Chato=Gbadolite.Ni kweli alitaka aendeleze kwao kama Mkwere lkn angalia na mazingira kwanza kabla ya kutupa shilingi ikiwa mradi husika utadumu au ukiondoka nao umekufa.By the way Mzilankende alijua ana muda mrefu ila bahat mbaya muda wake ulikuwa ukingoni.Nilichokuwa naogopa ni kukaa siku moja nikijua mtu atatawala daima milele baada ya kutengua katiba hii kitu ilikuwa inaniumiza sana kichwa
Mkwere unamsingizua tu. Zaidi ya kujijengea makazi yake binafsi alifanya nini tena ndani ya Msoga?
 
Wanaomsifia Magufuli ni watoto wa juzi, watu waliokuwa hawana access ya taarifa na watu wazima ambao walikua na maslahi na ujinga wake.

Kwa sisi wengine tunamfahamu tangu akiwa mbunge na waziri na madudu take aliyoyafanya. Tunakaa kimya tu
 
Hivi hayo matrilioni yanayopigwa na mafisadi hamyaoni mkayaandikia kitabu mmebaki kumsema sema marehemu Magufuli kwa chato palikuwa ni Burundi mnajua mnafanya unafiki na chuki nyie vyeti feki, wakwepa kodi, mafisadi,wahujumu uchumi
 
Hivi hayo matrilioni yanayopigwa na mafisadi hamyaoni mkayaandikia kitabu mmebaki kumsema sema marehemu Magufuli kwa chato palikuwa ni Burundi mnajua mnafanya unafiki na chuki nyie vyeti feki, wakwepa kodi, mafisadi,wahujumu uchumi
Acha utoto wako
 
Hivi hayo matrilioni yanayopigwa na mafisadi hamyaoni mkayaandikia kitabu mmebaki kumsema sema marehemu Magufuli kwa chato palikuwa ni Burundi mnajua mnafanya unafiki na chuki nyie vyeti feki, wakwepa kodi, mafisadi,wahujumu uchumi
Hakuna cheti feki kama Magufuli! Ninajua jinsi akina Dr Akwilapo walivyomfanyia PhD yake pale UDSM department of chemistry tukiwa tunaona!
 
Na kitabu cha mazuri ya Magufuli kiandikwe pia ili kubalance stori maana aliijenga Dodoma,alinunua ndege,hapakuwa na mifumuko ya bei kwenye utawala wake,nchi iliingia uchumi wa kati,alidhibiti,wala rushwa na mafisadi,alijenga hospital ya mwalimu Nyerere iliyoshindikana miaka 40 , alinunua rada 3,alifungua balozi 6, alijenga barabara sehemu mbalimbali,aliweka mradi mkubwa wa maji Arusha,alianza ujenzi wa bwawa la umeme la stigler gauge,
 
Kumtetea Magufuli ni jambo gumu na linahitaji propaganda sana. Hatuhitaji kuwa mtaalamu wa uchumi kujua kuwa Magufuli alifanya ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma alifanya miradi mikubwa bila utafiti wa kutosha au ridhaa ya bunge. Miradi ya Chato ilikuwa ya kwake binafsi ipo mingi; uwanja wa ndege, mahoteli, mbuga ya wanyama, etc. Uthibitisho wa miradi hii kuwa ililazimishwa bila kufuata market demand, ni kwamba miradi hii yote imekufa! Hili sio tatizo la covid.

Magufuli alikuwa the wrong president aliharibu uhuru wa kujieleza, watu waliporwa mali zao kibabe, uchaguzi mkuu ulivurugwa vibaya kuwahi kutokea barani Afrika. watu wameumizwa na kuuwawa. Utamdanganya nani kwamba haya yote ni kwasababu ya covid? Magufuli was a catastrophe for our country!
Na kumchafua Magufuli kunahitaji propaganda sana na upotoshaji mkubwa maana ana mazuri mengi mno na mara nyingi ukimuona mtu anaandika habari mbaya kuhusu Magufuli ni wale vyeti feki, wakwepa kodi, wadhulumaji, mafisadi, wezi, walamba asali, majizi, wauza ngada mimi sioni faida ya huu uharo mnaoufanya mitandaoni kumchafua Magufuli ili hali huo uhuru wa vyombo vya habari haujaondoa ufisadi mkubwa unaofanyika leo maisha magumu kwa watanzania
 
Wanaomsifia Magufuli ni watoto wa juzi, watu waliokuwa hawana access ya taarifa na watu wazima ambao walikua na maslahi na ujinga wake.

Kwa sisi wengine tunamfahamu tangu akiwa mbunge na waziri na madudu take aliyoyafanya. Tunakaa kimya tu
Huyu mpaka ukoo ulimtenga...
 
Na kumchafua Magufuli kunahitaji propaganda sana na upotoshaji mkubwa maana ana mazuri mengi mno na mara nyingi ukimuona mtu anaandika habari mbaya kuhusu Magufuli ni wale vyeti feki, wakwepa kodi, wadhulumaji, mafisadi, wezi, walamba asali, majizi, wauza ngada mimi sioni faida ya huu uharo mnaoufanya mitandaoni kumchafua Magufuli ili hali huo uhuru wa vyombo vya habari haujaondoa ufisadi mkubwa unaofanyika leo maisha magumu kwa watanzania
Unaweza kutaja jambo moja tu zuri alotenda Magufuli?
 
Chato=Gbadolite.Ni kweli alitaka aendeleze kwao kama Mkwere lkn angalia na mazingira kwanza kabla ya kutupa shilingi ikiwa mradi husika utadumu au ukiondoka nao umekufa.By the way Mzilankende alijua ana muda mrefu ila bahat mbaya muda wake ulikuwa ukingoni.Nilichokuwa naogopa ni kukaa siku moja nikijua mtu atatawala daima milele baada ya kutengua katiba hii kitu ilikuwa inaniumiza sana kichwa
Mkwere aliendeleza kitu gani kwake?
 
Haya yote ni sehemu ndogo tu ya maovu, ukatili, ufisadi, ubadhirifu, hasara, wendawazimu na ubovu wake.

Nawashukuru na kuwapongeza waandishi na wachapishaji kwa uzalendo wao.
Niwaombe na kuwatia moyo wengine kujitokeza na kuueleza umma yaliyokuwa yakijiri gizani. Lazima ukweli ujulikane na haki itendeke, ili tusijerudi tena huko asilan!

Kwa wale watetezi wa "legacy ya Kishetani " na mashabiki wa Mwendazake, ambao hujietetea kusema "...mbona tuhuma hizi/zinaletwa sasa.....kwa nini zisingetolewa alipokuwa hai ili "
'azijibu au kujitetea'....". Utetezi huo ni wa kipumbavu na wa kinafiki - hivi kuna mtu yeyote aliyepingana na dikteta hadharani, iwe kimawazo au kimatendo akabaki halafu salama? Mwendazake majibu na utetezi wake si ulijulikana waziwazi na kushagiliwa na "wanyonge" - kuua, kufilisi, kutesa, kufunga???

Je damu, maumivu, ulemavu na ukatili, hasara nk waliofanyiwa "wapinzani" wake hamkuviona wala kusikia?? Ukweli mnaujua na siku moja mtakiri mbele za Mola wetu.

Pamoja na hayo, budi sasa mjiandae kusikia na kuona bila chenga authentic 'replay' ya aliyoyatenda "shujaa" wenu dhalim Magufuli kwa HDV.
Tena haya ni mwanzo tu. Kuna mengi mno, tena ya kutisha tutaendelea kuhabirishwa siku na miaka ijayo.
Asante tena kinachofanya Hao watetezi wa Udhalimu wa Magufuli ni kwa sababu wengi walishirikiana nae kutenda hayo maovu kwa hiyo wanapinga kwa kujitetea wenyewe Ufirauni na ufedhuli wake inabidi uwekwe wazi ila baadae akatokea mwingine watu wasijifanye hawakujua
 
Back
Top Bottom