Corona ilipoingia dunia ilijifungia ndani lakini Tanzania haikujifungia ndani kwa sababu moja tu,ukijifungia ndani utakufa kwa njaa,shukrani kwa Hayati Rais John Pombe Magufuli aliyeliona hili na kuamua kutowafungia watu wake ndani,yalikuwa ni maono ya kuwazia kesho ya taifa lake iwe atakuwepo au hatokuwepo,ni dhahiri janga la corona lilitupa chaguzi mbili kufa kwa corona au njaa,waliochangua kufa na njaa wakaji-lockdown ili wasife kwa corona,Ila wafe kwa njaa,lakini mwamba,Rais Magufuli akasema shughuli ziendelee licha ya dunia nzima kupiga kelele baada ya kuona maisha yakiendelea kama kawaida hapa Tanzania.
Gonjwa la corona lilihusiana na upungufu wa kinga ya mwili,Watanzania tukasema kinga tunayo,hatuwezi kujifungia ndani kufa njaa ni kujitakia,tukifa njaa hata Mungu atatuona wajinga,Watanzania wakaendelea na shughuli zao na uchumi ukaendelea kukua kwa asilimia 7,ni dhahiri ukiwa na njaa kinga ya mwili itashuka na corona itakuua,kama una njaa utapambana vipi kuushinda ugonjwa,nguvu za kinga mwilini huna na pesa huna? lazima utakufa,wakati tukichukua uamuzi kama nchi, Chadema wakagoma wao wakawa wamechagua lockdown,jambo la ajabu wabunge wa Chadema na Zitto walikuja kwenda lockdown baada ya posho zao za bunge shilingi milioni 110 kuingia kwenye akaunti zao,
Baada ya posho wabunge wa Chadema hawakuingia bungeni wakajifungia mahotelini na majumbani kwao baada ya kuwa na uhakika wa chakula yaani food security ndio wakajilock down,sasa vipi kuhusu mwananchi anayejitafutia kipato kwa kufanya day walker kila siku,kila ukitoka ndio unapata hela,awa waliunga mkono uamuzi wa Rais Magufuli,ikiwa umeshiba na pesa unayo hapo kupigana na corona unakuweza hata immunity mwilini inakuwemo sababu mwili umeshiba virutubisho vya kila namna unakuwa corona proof, Watanzania waliamua kuendelea na shughuli zao kama kawaida,uchumi waliujali tusife njaa na corona tukapambana nayo,tukapigana vita zote kwa mpigo na kwa hakika tulishinda na baada ya kushinda,Mungu alimuita jemedari wetu Hayati Rais John Pombe Magufuli.
Kwa namna ya pekee Watanzania tulitembea kifua mbele kipindi cha Hayati Rais Magufuli,Rais Magufuli alionyesha Ulimwengu kuwa watanzania hatuna akili za kushikiwa kama nchi zingine duniani "we are independent thinkers" ndio maana Rais Magufuli alipoongea kijijini Chato,Mkoani Geita basi wazungu walipanda kwenye studio za BBC na CNN kujibu hoja za Rais Magufuli,hoja moja wapo aliuliza imekuwaje chanjo ya corona ipatikane haraka kuliko chanjo ya ugonjwa wa ukimwi iliyoanza kufanyiwa utafiti miaka ya 1980,swali hili lenye ukweli liliwagusa wazungu vilivyo na kuonekana kama siri inakwenda kutoboka,kwenye vita waweza kuwa na adui wengi unatakiwa upigane nao kwa mpigo,kipindi cha corona tulikuwa na adui wawili wa corona,njaa na uchumi kuyumba wote walitakiwa washambuliwe kwa pamoja,Upande Wa kushoto watanzania tulikuwa na panga la kupigana na njaa na uchumi, mkono wa kulia tulikuwa na panga la kupigana na corona,
Rais Magufuli hakumuacha Mungu,alimuomba Mungu atusaidie wakati wa corona sababu hata mataifa wababe kwa vita duniani kama Marekani na China walikimbilia ndani wakajifungia lockdown waksshindwa kupigana vita zote mbili kwa mpigo,kwa hakika Rais Magufuli alituvusha kwenye vita ya dunia ambayo ilimshinda Mchina na Mmarekani maraisi waliomtangulia walituvusha vita na majirani na makaburu lakini Hayati Rais Magufuli alituvusha vita ambayo hata ulaya China,Marekani na nchi wababe wa nchi za kiafrika hawakuiweza,pumzika kwa amani Shujaa Rais John Magufuli,wewe ni war commander than any president on Earth,japo wachache wanakutukana,upo ule usemi nabii hakubaliki nyumbani. Je, Magufuli ni nabii? Tanzania wanambeza, Afrika walimlilia! Tanzania ilipigiwa mfano Magufuli awe Rais wa Afrika,na Marais wote wa Afrika walimuona Rais Magufuli akipita njia ile ile ya Pan Africanist Kwame Nkrumah, George Padmore,Marcus Gavey,Thomas Sankara,Oliver Tambo,Nelson Mandela na Julius Nyerere.
Nimalizie kwa kusema kuwa vita ya njaa ni mbaya kuliko vita yoyote ile,siku kilo ya mchele ikifika elfu tano watu wataanza kuelewa vita ya njaa,tunashukuru Tanzania tulipata mtu mtu kweli,kamanda kamanda kweli na Rais,Rais kweli, Daktari John Pombe Joseph Magufuli,pumzika kwa amani,Mzee wetu.
Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master of Leadership and Management.
Recent Publications;-
-Assessment on the effect of Micro-Financing on Poverty Reduction.