CHATO: Rais Magufuli asema Serikali haitafunga mipaka wala kuwazuia watu kutoka ndani ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona

CHATO: Rais Magufuli asema Serikali haitafunga mipaka wala kuwazuia watu kutoka ndani ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona

Mpelelezi J. Hata Usa ni law enforcement agencies ndio wanasimamia haya. Nimeona wanaweka hadi cones kama alama ili mtu asimame hapo ili awe mbali na mwingine kama anakata ticket au la. Na sisi tuige hao waliofanikiwa. Na kama ikiwezekana ifanyike mapema.
Hili wazo lako la kukaa mbalimbali litasababisha madhara. Kumbuka kuna nchi 8 zinatutegemea. 😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
..pia watu wote walazimishwe kavaa face mask, vitambaa, kukinga pua na mdomo.

..hatua yoyote ya tahadhari ambayo iko ndani ya UWEZO wetu tusiache kuichukua.
Sasa utapata wapi pesa za kununua hizo mask. Kaendelee kuchapa kazi achana na mambo ya kuvaa maski. Chapa kazi kuna nchi zinatutegemea.
 
Hii nchi hatupo seriaz saiv tunapeana kauli za kishujaa

Yakifika kama ya Italy na Spain tutaanza kuuza kesi kwa Mabeberu na wapinzani
Kuna mstari mwembamba unaotenganisha ushujaa na ujinga, huwezi kumwona simba mwenye njaa amelala ukaenda kuminya kengele zake
 
View attachment 1415673

Amesisitiza kuwa Serikali imeamua kutowazuia Watu ndani ya nyumba zao wala kufunga mipaka kwa kutambua madhara mkubwa yanayoweza kutokeza kwa kufanya hivyo.

Aidha, amesema madhara hayo yanaweza pia kuziathiri nchi 8 ambazo zinatengemea kupata huduma na bidhaa kupitia Tanzania hususan bandari ya Dar es Salaam.

Lakini pia amebainisha kuwa kutokana na madhara ya #CoronaVirus upo uwezekano mkubwa wa kutokea kwa upungufu wa chakula, hivyo amewataka Wananchi kuzalisha chakula cha kutosha.

Pia, amesisitiza Wananchi waendelee kuchapa kazi kila mahali walipo huku wakichukua tahadhari ya kutokuambukizwa kwa kufuata ushauri wa Wataalamu na pia wasisahau kumuomba Mungu atuepushe na janga hili
Rais Magufuli ameyasema hayo alipokuwa akiongea na Waumini wa Kanisa Katoliki katika Parokia ya Mlimani, Wilayani Chato mkoani Geita ambapo alihudhuria ibada ya Ijumaa Kuu.



View attachment 1415488View attachment 1415489
Rais wa Tanzania, John Magufuli akiwa katika Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana-Maria Mzeyi Parokia ya Mlimani Chato mkoani Geita leo. Picha na Ikulu

Haijalishi ata aseme hatafunga mipaka na hakuna lockdown, wananchi wenyewe wanaangalia upepo unavyopiga hali ikibadilika zaidi wataanza lockdown wenyewe bila ya kuambiwa
 
Sasa utapata wapi pesa za kununua hizo mask. Kaendelee kuchapa kazi achana na mambo ya kuvaa maski. Chapa kazi kuna nchi zinatutegemea.

..tuwe wabunifu.

..tunaweza kutengeneza za vitambaa.

..tufanye yaliyoko ndani ya uwezo wetu.

..pia tusitoe kauli za kupuuzia ugonjwa huu, kwani ni hatari.

..kwa mfano nimemsikia Raisi akasime Covid19 ni " kaugonjwa ". Nadhani siyo sahihi kusema hivyo.
 
Hongera sana Rais Pombe.

Wewe Ni kiongozi usiyeongozwa na hisia. Una tabia za uongozi ( acha wanaolalamika walalamike tu maana Ni kazi yao )

Mwagize Ndalichako atangaze wanafunzi warudi vyuoni, #Hapa kazi tu.

Tunamtumaini Mungu. Na hajawahi kutuacha tumeonesha imani kwake.

Vyuo vifunguliwe maana na vyenyewe Ni sehemu ya kazi.

Tuchukue Tahadhari juu ya Corona, tuwasikilize wataalamu wetu wa afya
 
baada ya wiki mbili watanzania wataimba haleluya CORONA SIO MCHEZO KAMA TANGAZO LA SALAM NA MWANA FA


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
..tuwe wabunifu.

..tunaweza kutengeneza za vitambaa.

..tufanye yaliyoko ndani ya uwezo wetu.

..pia tusitoe kauli za kupuuzia ugonjwa huu, kwani ni hatari.

..kwa mfano nimemsikia Raisi akasime Covid19 ni " kaugonjwa ". Nadhani siyo sahihi kusema hivyo.
Mask siyo kama khanga mkuu. Zina utaalam wake. Ingekuwa ni kitambaa hata leso ingefaa.

Muhimu hapa ni kuwa tuna nchi zinatutegemea. Sisi tuchape kazi tu ili nao wenzetu wasije wakapata madhara.
 
Salaaaam.....


Iv tunavolalamika mipaka aifungwi mara cjui rais ajasema lockdown...kwan sisi wenyewe atuwezi kujua kipi kizuri kipi kibaya.. kama cha msingi ni lockdown tukiamua watu wote ni lock down na tukakaa ndani kwani serikali itatulazimisha tutoke njee....au ndo mpaka kila kitu tupewe amri......


ila yote na yote hakunaga kaburi la mtu muoga.....pia ikifika siku yako ya kufa lazima utakufa tu.....salaaam
Hata mimi nashangaa watu wanalalamika kuwa kwa nini hakuna lockdown. Hivi si wakae nyumbani? Tumeambiwa tufate taratibu za kujikinga ambazo zinajulikana watu hawafati wanataka kulazimishwa. Watanzania Sisi ni watu wa ajabu sana
 
Wewe mdanganye tu baba wa watu watoto wakifa unafikiri tutamdai shetani..?

Kwa unadhani yeye hapendi kuendelea kupiga picha juu ya mawe? Wewe ropoka ropoka tu wakati unajua kuna korona imeanza kutamalaki
 
Kwa hili la kufunga nakuunga mkono kwa asilimia 100 japo tumechelewa lakini athari zinaweza kupungua kuliko hii njia tunayoitumia. Wataalamu wa afya wangeruhusiwa kutueleza hatua sahihi za kujikinga na ugonjwa huu badala kuamuliwa na wanasiasa. Tujiulize swali dogo Watanzania kule Makao Makuu ya Kabisa Katoliki ibada ilivyoendeshwa bila Misongamano kabisa kwa nin?
Mura unataka kusema hujui njia za kujikinga na huu ugonjwa?
 
Back
Top Bottom