Chato yazidi kuneemeka; Serikali kujenga Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa

Chato yazidi kuneemeka; Serikali kujenga Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa

Vitu vyote hivyo vingeweka ( kujengwa ) kahama .Kahama ingewini sana


Chato Mzee ndio anaikuza aseh

Sent using Jamii Forums mobile app
Chato haiwezi kukua,bora yeye angejikita kuwajengea shule na kuwatafutia kazi za upendeleo zile nono kama huko TRA na bandarini,ila hayo madude ya majengo atafurahi mwenyewe akitoka madarakani yatakavyochakaa,hawaamini,jamaa huyu akili zake
 
TANAPA nao wanapeleka simba 20 burigi national park sasa sijui watakula nyasi kule
 
Chato haiwezi kukua,bora yeye angejikita kuwajengea shule na kuwatafutia kazi za upendeleo zile nono kama huko TRA na bandarini,ila hayo madude ya majengo atafurahi mwenyewe akitoka madarakani yatakavyochakaa,hawaamini,jamaa huyu akili zake
Chato inaenda kuwa mkoa wa Rubondo, na chato itakuwa makao makuu ya mkoa mpya wa Rubondo, so hiyo economic and social infrastructure itabaki kuwa relevant hata akiondoka. Sababu mkoa ni tofauti na kijiji
 
Waliozembea kina che nkapa tuu..


Che nkapa unaona mwezio huyooo we ulijenga daraja tuuu
 
Chato inaenda kuwa mkoa wa Rubondo, na chato itakuwa makao makuu ya mkoa mpya wa Rubondo, so hiyo economic and social infrastructure itabaki kuwa relevant hata akiondoka. Sababu mkoa ni tofauti na kijiji
Hata akifanya mkoa,kwanza atakuwa ni mpuuzi,na pili Chato hapataweza kuendelea,angesomesha watu na kuwawezesha kiuchumi kwanza,pale watu wana umaskini wa kutisha,na nimiongoni mwa maeneo yanayosababisha watu wa kaskazini watucheke sisi watu wa kanda ya Ziwa,upuuzi mkubwa kabisa,
 
Hospitali ya Rufaa inajengwa wilayani! Kwa mkakati huu ni wazi mambo mawili yatokea; ama makao makuu ya mkoa wa Geita yatahamia Chato, au utaundwa mkoa mpya ambao makao makuu yatakuwa Chato. Nilipoamka nikajua kuwa nilikuwa ndotoni.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya Tanzania itajenga Hospitali ya Rufaa wilayani Chato Mkoa wa Geita.
Akiwasilisha taarifa yake kwa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii leo Jumatatu Januari 20, 2020, Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ummy Mwalimu amesema Serikali inatarajia kujenga hospitali hiyo kutokana na idadi kubwa ya watu kuwa eneo hilo.

“Tumefanya utafiti na kugundua kuna wagonjwa wengi Kanda ya Ziwa kwa hiyo tunajenga Zonal Hospital (hospitali ya Kanda) Chato,” amesema.

Amesema kuwa sababu ya kujenga hospitali hiyo Chato ni Mikoa ya kanda ya ziwa kuwa na watu zaidi milioni 15.

Baada ya Waziri Ummy kueleza hayo, baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba walicheka.

Baadaye wajumbe wa kamati hiyo watapata fursa ya kuichangia na kama kutakuwa na maswali, mapendekezo watayatoa.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma Serikali kujenga hospitali ya kikanda ya kitalii Geita

Mbona mmechelewa sana ? Miaka 50 sasa ndio mnafikiria kujenga? Tumepiteza mamilioni ya watu na wengine kuwa vilema vya maisha kwa kukosekana huduma za karibu na uhakika.

Ni wakati ccm iyondoke madarakani, na tuwsfungilie mbali, mmetupa umasikini wa kutupa, nyerere alipo pata urais tu kauwa viwanda vyote tanga, kawafilisi matajiri na kuchukua mali zao.

Ile dhambi inaendelea hadi sasa na imekuwa censer kwa ccm na utawala wake.

Mnasema watu wasio julikana hamuwajui, lakini hatusikii kitekwa kiongozi wa ccm au kuuliwa au kupotea kimatata.
 
Wacha Nyerere aitwe baba wa Taifa.
Ingawa nahisi watu wa 'Butihama' karibuni wataanza kumlaumu kwa kutotumia fursa.
Mzee Mwinyi na Kikwete mlikwama wapi mbona Mkoa wa Pwani haukupata mavitu makubwa haraka?
Hadi leo hakuna mataa ya kuongozea magari kama 'Chattle'
Kwani Mloganzila iko Singida au

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata akifanya mkoa,kwanza atakuwa ni mpuuzi,na pili Chato hapataweza kuendelea,angesomesha watu na kuwawezesha kiuchumi kwanza,pale watu wana umaskini wa kutisha,na nimiongoni mwa maeneo yanayosababisha watu wa kaskazini watucheke sisi watu wa kanda ya Ziwa,upuuzi mkubwa kabisa,
Pataachaje kuendelea pakiwa mkoa? Hivi ushawahi fika Bariadi kabla na baada ya kuwa mkoa? Kama ushawahi fika Bariadi nenda sasa hivi ukaone maendeleo ya pale
 
Hakuna cha ubaba! Taifa umaskini chanzo ni yeye. Magufuli ndiyo ananyoosha hii sasa.

Pwani ipi? Au hujui viwanda takribani 73 vimejengwa enzi za Kikwete?! Mloganzila kwanini haikupelekwa Iringa?!

Tuwe wakweli zama za Umwinyi na Umangi kwisha habari yake. U-Daslam utapotea ili taifa lisonge.

Haiwezekani mtu Kigoma na Kagera yupo mahtuti mpaka afike Daslam kwa tiba! Haiwezekani, Daslam ni kipande kidogo sana kwa Tanzania.

Maendeleo endelevu ya Tanzania
Hospitali ya rufaa, tena ya serikali inajengwa wilayani! Yaani mji wa Chato? Chato kunani?

Chato 'International ' Airport, Chato International stadium, Chato Referal Hospital, Chato TRA 'Regional ' office! Baada ya miaka 5, Chato ndio utakuwa mji mkubwa na wa kisasa zaidi katika Kanda ya Ziwa.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pembezoni ipi unayoisemea?! Daslam?, Zama hizo zimeisha.

Kwa takribani miaka 60 sasa wakazi wa Kigoma na Kagera wamekuwa wakifuata huduma za kijamii Daslam, Elimu ya juu, Hospitali, Usafiri wa Kimataifa na mengineyo. Haiwezekani hii lazima ifike ukomo kwa maendeleo ya taifa hili! U-Daslam lazima ufe.
Tunasubiri Zitto awe mkulu tupate

Sent using Jamii Forums mobile app
 
center-chato.png
 
Back
Top Bottom