Vyamavingi
JF-Expert Member
- Oct 3, 2014
- 5,818
- 5,555
Kwa hiyo unataka waunge mkono hata mambo yasiyo na tija kwa kuwa tu watafaidika wao?Kinachonisikitisha ni watu wa Kigoma na Kagera wakisema hivyo.! [emoji22]
Chato imekuwa mkoa lini wewe Lumaga? Kwa nini wasijenge kwanza Katavi, Njombe au Songwe? Hiyo ndio mikoa mipya, nchi yako mwenyewe, lkn huijui.Nashangaa wabunge hawajui kuwa hospitals zote za mikoa zine hadhi ya rufaa walichokuwa wanacheka mini kama siyo unafiki. Hospitals zote za mkoa ikiwemo Chato ndani ya Geita ni za rufaa. Fanyeni ufuatiliaji kuliko kuchekacheka
Usitake tuanze kutaja vyote vilivyojengwa Chattle kwa muda wa miaka chini ya sita kisha tulinganishe na miaka 10 ya JK mwenyeji wa Msoga Bagamoyo/Chalinze Pwani, na miaka 10 ya Mwinyi Mkuranga Pwani.
Wasukuma wa Bariadi uwezi linganisha na wasumbwa,wasubi na wasukuma wa Chato,Bariadi ndo inawasukuma wajanja na weupeππ,nafikiri nikisema wasukuma weupe unajua namaanisha wana ng'ombe wengi,pili ndo wanaomiliki biashara ya madini kanda ya Ziwa yote,huwezi linganisha msukuma (Mnyantuzu) wa Bariadi na ujinga huo wa Chatto,Chatto hata mfanye nchi kabisa haina human capital ya kupaendeleza,angejikita kuwasomesha wanachato zaidi ya anavyofanya hivi sasa,sijui nani anamshauri huu ujinga,nakumbuka alikuwa ana ndoto ya kupafanya mkoa siku nyingi,isingekuwa Kikwete Geita isingekuwa makao makuu ya mkoaPataachaje kuendelea pakiwa mkoa? Hivi ushawahi fika Bariadi kabla na baada ya kuwa mkoa? Kama ushawahi fika Bariadi nenda sasa hivi ukaone maendeleo ya pale
Magufuli sio wa kumtetea kabisa,hayo ni maelekezo yake asilimia 100,wala usisingizie wasaidizi wakeUsitake tuanze kutaja vyote vilivyojengwa Chattle kwa muda wa miaka chini ya sita kisha tulinganishe na miaka 10 ya JK mwenyeji wa Msoga Bagamoyo/Chalinze Pwani, na miaka 10 ya Mwinyi Mkuranga Pwani.
Usituletee kichekesho kama licholeta mwenzio nikamyamazia kama sijaona cha kuhesabu na viwanda vilivyojengwa Pwani na wawekezaji binafsi kwa fedha zao huku hivyo vya Chattle vikijengwa na serikali.
Sina chuki na mpambanaji wangu Mh. Magufuli, I wish asome comment zangu zote aone ninavyomtetea na kumkubali lakini pia aone na hizi nilizokosoa watendaji wake kufanya yaliyofanyika kwao, sina hakika kama yana baraka zake au maagizo yake.
Huenda ni kujipendekeza tu kwa watendaji walio chini yake kwa boss wao. Kama ni maagizo yake basi namuomba aangalie ushauri wetu.
Pale kuna umaskini wa kutupwa,yaani hii roho mbaya aliyonayo kwa watanzania anayo mpaka pale kijijini kwake Chatto,yaani kama alivyosema Nyerere dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana,yaani anavyobagua mikoa na wilaya ndo anavyobagua mitaa na vijiji vya Chatto,huyu jamaa makuzi yake yalikuwa yana shida kubwa sana ,pale Chatto maendeleo na majengo mengi anajenga karibu na ka-hoteli kake ambapo ndo kwake,yaani kwa kifupi vitu vingi anajenga kijijini kwake pale,mita mia mbili tu kutoka kwake pale hali ni mbaya haswa,nilikosea sana kumpigia kura mtu wa namna hiiWananchi wa chato naona neema imewatembelea kwakweli.
Mapungufu yake kwenye jambo au sekta moja hayawezi kuwa sababu ya kuto mtetea kwenye mengi mazuri anayofanya.Magufuli sio wa kumtetea kabisa,hayo ni maelekezo yake asilimia 100,wala usisingizie wasaidizi wake
Kwa hiyo ana mapungufu machache zaidi ya mazuri,seriously πππ,mimi nilikuwa namkubali sana kipindi akiwa waziri mpaka kuna kipindi kile iliposemekana kawekewa sumu akakimbizwa sijui hospitali ya dodoma mara Ujerumani roho iliniuma sana,lakini leo yaani kwenye ule wimbo Idd Amini akifa mimi siwezi kulia hapo kwa Idd Amin weka jina lakeMapungufu yake kwenye jambo au sekta moja hayawezi kuwa sababu ya kutomtetea kwenye mengi mazuri anayofanya.
Kila mtu ana mapungufu flani, hakuna mtu mkamilifu kwa yote.
Sikujua kama ulikuwa hapa kubishana! Binafsi nipo hapa kuelimishana.Kubishana na wewe ni 'futile worth no effort' sababu hakutakuwa na muafaka.
Kama hauoni yaliyo fanywa na Nyerere basi sina namna ya kukufanya uyaone.
Kama ndege ziliuzwa, mashirika yaliuzwa, viwanda viliuzwa, nyumba ziliuzwa.
Reli ya TAZARA ipo, meli bado zilikufa au kuzama wakati ameshaondoka, vyuo vipo, shule zipo.
Hizo huduma za kijamii zilizokuwa zinatolewa wakati wa Nyerere huwezi kuzitunza kama kitu tangible, sijui ulitaka tukutunzie vipi uzuone.
Kwa kifupi nenda kawaulize wakubwa wako au kama ungekuwa karibu na Mh. Magufuli tafuta siku akiwa na nafasi japo dakika 2 muulize mambo ya Nyerere wakati yeye anasoma, muulize mzee unajipimaje na yule mzee muadilifu na mchapa kazi mwenzio?
Kama sio mnafiki, na mimi nina uhakika, nina imani nae atakuwa mkweli atakuambia yeye anafikia wapi kwenye kipimo cha utendaji na uzalendo wa Nyerere, achana na uadilifu.
Unachekesha unapojaribu kumponda sera za Nyerere kwamba ndizo zilizo tufanya tuwe maskini huku ukimsifia Magufuli ndio anatupeleka njia sahihi wakati anachofanya Magufuli ni kujaribu kuiga karibu kila kitu cha Nyerere.
Kuanzia sera na misimamo japo bado hajafikia level ya Nyerere.
Inaonesha hata hujui nini hasa anachokifanya Magufuli na nini alichofanya Nyerere. Haujui hata ideology ipi watu hawa wawili waliifuata au huyu anaifuata sasa.
Humjui kiitikadi mtu hata unaemshangilia na kumsifia.
Hizo document hazina chochote cha ajabu, na hazitakusaidi wewe wala Tanzania kuleta maendeleo yako binafsi na ya nchi yetu. Yamejaa propaganda za kimagharibi ambazo huyu Mwamba Magufuli anazijua na kuzipiga na Nyerere alikabiliana nazo hadi siku anakata kauli.
Huo ni mtazamo wako sio wa wote.Kwa hiyo ana mapungufu machache zaidi ya mazuri,seriously πππ,mimi nilikuwa namkubali sana kipindi akiwa waziri mpaka kuna kipindi kile iliposemekana kawekewa sumu akakimbizwa sijui hospitali ya dodoma mara Ujerumani roho iliniuma sana,lakini leo yaani kwenye ule wimbo Idd Amini akifa mimi siwezi kulia hapo kwa Idd Amin weka jina lake
Kwa sentensi hii nishakujua wewe wa namna gani.Kiongozi imara na mzalendo hapimwi kwa kutojenga kwao!. nyerere huyu aliyetengeneza gap la ufaulu baina ya jamii fulani na jamii fulani ndio awe mzalendo?!
Nyerere angekuwa na akili kama za huyu mzee, basi ikulu ingejengwa butiama, tena ukizingatia uhuru alienda kudai yeye mwenyewe kwa mguu wake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama Baba wa Taifa na marais wengine waliomfuatia wangalikuwa na tabia hizi za kichoyo, kukosa aibu na upendeleo wa wazi wa maendeleo ya vitu, huku waliowazunguka wakishindana kupeleka kwa kasi maendeleo ya vitu ktk maeneo waliyotoka, sijui taifa letu leo lingalikuwa ni la namna gani.
Sent using Jamii Forums mobile app