Cheo cha Makamu wa Rais hakina tija, tukiondoe, tubakishe cha Waziri Mkuu

Cheo cha Makamu wa Rais hakina tija, tukiondoe, tubakishe cha Waziri Mkuu

Kwenye suala la waziri mkuu hoja yako ni dhaifu na haina mashiko. Waziri mkuu ni mtu mdogo kwa Rais wa Zanzibar which means hawezi kuextend utendaji wake Both Tanganyika and Zanzibar

Ka Zanzibar ni kadogo sana kangefaa kuwa mkoa tu wala haifai kuwa Nchi ni mara mia muungano ufe waachwe wenyewe uone Tanganyika itavyopumua baada ya kujivua zigo la kuilea Zanzibar iliyojaa watu wengi wavivu wakaa vibarazani hawapendi kufanya kazi mda mwingi huutumia kulalamika tu juu ya muungano usio na Tija kwa Taifa kwa sasa Zaidi ya kuwa muungano mzigo kwa walipa kodi
 
Tatizo ukivunja Muungano, Je unaujua mpaka wa Tanganyika na Zanzibar ulipo?

Baada ya Muungano kufa ama ni vita ya kugombea mpaka wa maji baharini au ni Tanganyika kupata kaeneo kadogo ka bahari katika uelekeo wa zanzibar na Pemba!. Yaani ili kuipata Bahari kuu kutokea Tanga na Dar lazima ushuke hadi mtwara huku la ndo uitafute, La sivyo utalazimika kupita ama katika maji ya Kenya au katika maji ya nchi ya Zanzibar

Mipaka ipo na Tanganyika ana nafasi kubwa baharini pia ukumbuke muungano ukifa lazima na pemba watajitenga na unguja na kuwa Nchi tofauti hilo lipo na halina Ubishi.
 
Mam
Yule mama anatusaidia kweli kutuwakilisha huko nje. Sasa hivi kungekuwa na references kibao za font page, hiyo hiyo huko duniani.
Mama pia anatusaidia sana kupoza moto ENGINE pindi ENGINE ikipata moto!
 
Umekosea kusema ivo.

Nadhani hujui majukumu ya Makamu wa Rais wewe vizuri.

Ungesema kua aondolewe kwa kua hana kazi tena awamu hii.

Traditionally, Kazi kubwa ya Makamu wa Rais ni kua MKATA UTEPE mkuu wa Serikali.

Kumbuka enzi za Gharib Bilal alikua anatembea na mkasi wake huku akitoa hotuba maridhawa!

Ila awamu hii Kazi ya Makamu wa RAIS inafanywa na Rais....kila utepe unakatwa na John Pombe...

Sasa Makamu wa Rais hana kazi tena zaidi ya kula mshahara wa bure tuu.
 
Makamo wa raisi alikuwa bwana mikasi ila awamu hii raisi ndo bwana mikasi mzinduzī
 
Nchi yetu ni nchi masikini, kutokana na hali hiyo ni muhimu kila senti inayopatikana ikatumika vizuri.
Leo hii nchi yetu ina viongozi wakubwa wafuatao
1. Raisi
2.Makamu wa raisi
3.Waziri Mkuu
4.Raisi wa Zanzibar
5.Makamu wa Kwanza wa raisi wa Zanzibar
6.Makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar


Ukiangalia kwa muundo huu wa serikali zote mbili ya Muungano na ya Zanzibar, hii ni serikali kubwa sana, viongozi hawa wote kila ofisi yake ina bajeti kubwa tu inayopitishwa na bunge/Baraza la wawakilishi kila mwaka. Ili kubana matumizi tunahitaji serikali ndogo lakini yenye ufanisi wa hali ya juu!

Leo hii Waziri Mkuu ana bajeti, lakini ukikaa chini na kuchunguza utaona kimuundo Waziri Mkuu anatumika zaidi Upande wa Tanganyika kuliko Zanzibar (Sijiu ni ziara ngapi za kitendaji Waziri Mkuu amekwenda kufuatilia shughuli za kila siku za serikali huko Zanzibar kama afanyavyo katika mikoa ya huku Tanganyika).

Ukichunguza, utaona kwamba Mamlaka ya Waziri mkuu kwa huko Zanzibar yamekasimiwa kwa Makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar (Cheo ambacho zamani kilikuwa ni Waziri kiongozi), Hata kwa mambo ambayo ni ya Muungano utaona kuwa kwa huko Zanzibar yanafanywa na ofisi hii badala ya Waziri Mkuu!. Sasa hapa tunapokuja katika Bajeti, huu ni mzigo mkubwa kwa Walipa kodi wa nchi hii, kuhudumia Ofisi mbili za mambo yaleyale!

Tukija kwenye ofisi ya Makamu wa Raisi, Utaona kwamba majukumu yake ni kumsaidia raisi pindi raisi akiwa hayupo ofisini na pia kuna majukumu machache tu ambayo katiba imempa, angalia ibara hii ya katiba hapa chini kuhusu madarka ya makamu wa raisi.


View attachment 975882

Katika mazingira haya, Je ni kitu gani kilishindikana Kuunganisha Majukumu haya machache ya ofisi ya makamu wa raisi ili yaingie katika ofisi ya Waziri Mkuu na hivyo kusaidia kupunguza matumizi ya pesa ya Umma kwenye kugharamia ofisi hii?

HOJA YA KULINDA MUUNGANO KWA MUUNDO HUU INA MANTIKI?

Utaratibu wa sasa unasema kuwa kama Rais atatoka upande mmoja wa muungano basi Makamu atoke upande wa pili, lengo hapa ni kuwa na uwakilishi wa pande mbili katika serikali, lakini cha kujiuliza Je haiwezekani tukawa na Utaratibu mwingine mzuri na ulionafuu kiuendeshaji kuliko wa sasa?- NAAMINI INAWEZEKANA, - Tuondoe cheo cha Makamu wa Raisi kupunguza gharama, kisha tuwe na Vyeo viwili tu vikubwa Cha Raisi wa JMT na cheo cha Waziri Mkuu, Lakini Waziri Mkuu huyu apatikane kutoka upande wa pili wa Muungano( Yaani kama raisi atatoka bara, Waziri Mkuu atoke Zanzibar) na athibitishwe na Mabunge yote mawili (Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi), Kama bunge moja kati ya hayo mawili litamkataa basi atafutwe mwingine.

FAIDA ZAKE NINI
  • Kutakuwa na Waziri Mkuu mtendaji, Mwenye Mandate ya kufanyia kazi mambo ya muungano kwenye pande zote mbili akiwa anajiamini kwa kuwa kapitishwa na mabunge yote mawili
  • Itapunguza gharama za uendeshaji wa serikali
  • Tutapunguza gharama za kuhudumia Wastaafu, tufahamu wazi kuwa Kila mstaafu katika wale viongozi wetu wakubwa yaani rais, makamu, waziri mkuu n.k wanaendelea kupata mishahara minono na stahiki nyingi sana, Tukiondoa cheo cha makamu wa rais tutapunguza gharama
HITIMISHO
  • Ukisoma majukumu ya Waziri mkuu na Makamu wa Raisi kwa mujibu wa katiba, kuna sehemu majukumu yao yanafanana, nayo ni "Kupangiwa kazi yoyote na raisi kadri atakavyoona inafaa", Sasa kama hili linawezekana maana yake ni kwamba inawezekana kabisa Waziri mkuu kufanya majukumu ya kawaida ya kila siku ya makamu wa raisi "kama akiagizwa na raisi", sasa kwa nini tuwape kazi ileile watu wawili wakati mmoja anaweza kuifanya?-TUTUMIE VIZURI KODI ZA WANANCHI TUONDOE CHEO CHA MAKAMU WA RAISI
  • Pili, Hiki cheo cha kungoja raisi asiweze kutimiza majukumu yake ili mtu ahesabiwe kuwa eti kusubiri kwake huko ni sehemu ya kazi yake halafu kila mwezi tuendelee kumlpia mshahara, mimi nadhani huu ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi
  • Hakuna chochote kile kinachofanywa na ofisi ya Makamu wa Raisi ambacho hakiwezi kufanywa na ofisi ya Waziri Mkuu mwenye mandate iliyoshiba ya nchi nzima, Kwa maoni yangu Cheo cha Waziri Mkuu kinatutosha, Cheo cha makamu wa rais kinaongeza mzigo kwa Taifa!
Ukiniuliza Makamu wa Rais wa Tanzania kazi zake ni zipi hata sijui
 
Nchi yetu ni nchi masikini, kutokana na hali hiyo ni muhimu kila senti inayopatikana ikatumika vizuri.
Leo hii nchi yetu ina viongozi wakubwa wafuatao
1. Raisi
2.Makamu wa raisi
3.Waziri Mkuu
4.Raisi wa Zanzibar
5.Makamu wa Kwanza wa raisi wa Zanzibar
6.Makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar


Ukiangalia kwa muundo huu wa serikali zote mbili ya Muungano na ya Zanzibar, hii ni serikali kubwa sana, viongozi hawa wote kila ofisi yake ina bajeti kubwa tu inayopitishwa na bunge/Baraza la wawakilishi kila mwaka. Ili kubana matumizi tunahitaji serikali ndogo lakini yenye ufanisi wa hali ya juu!

Leo hii Waziri Mkuu ana bajeti, lakini ukikaa chini na kuchunguza utaona kimuundo Waziri Mkuu anatumika zaidi Upande wa Tanganyika kuliko Zanzibar (Sijiu ni ziara ngapi za kitendaji Waziri Mkuu amekwenda kufuatilia shughuli za kila siku za serikali huko Zanzibar kama afanyavyo katika mikoa ya huku Tanganyika).

Ukichunguza, utaona kwamba Mamlaka ya Waziri mkuu kwa huko Zanzibar yamekasimiwa kwa Makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar (Cheo ambacho zamani kilikuwa ni Waziri kiongozi), Hata kwa mambo ambayo ni ya Muungano utaona kuwa kwa huko Zanzibar yanafanywa na ofisi hii badala ya Waziri Mkuu!. Sasa hapa tunapokuja katika Bajeti, huu ni mzigo mkubwa kwa Walipa kodi wa nchi hii, kuhudumia Ofisi mbili za mambo yaleyale!

Tukija kwenye ofisi ya Makamu wa Raisi, Utaona kwamba majukumu yake ni kumsaidia raisi pindi raisi akiwa hayupo ofisini na pia kuna majukumu machache tu ambayo katiba imempa, angalia ibara hii ya katiba hapa chini kuhusu madarka ya makamu wa raisi.


View attachment 975882

Katika mazingira haya, Je ni kitu gani kilishindikana Kuunganisha Majukumu haya machache ya ofisi ya makamu wa raisi ili yaingie katika ofisi ya Waziri Mkuu na hivyo kusaidia kupunguza matumizi ya pesa ya Umma kwenye kugharamia ofisi hii?

HOJA YA KULINDA MUUNGANO KWA MUUNDO HUU INA MANTIKI?

Utaratibu wa sasa unasema kuwa kama Rais atatoka upande mmoja wa muungano basi Makamu atoke upande wa pili, lengo hapa ni kuwa na uwakilishi wa pande mbili katika serikali, lakini cha kujiuliza Je haiwezekani tukawa na Utaratibu mwingine mzuri na ulionafuu kiuendeshaji kuliko wa sasa?- NAAMINI INAWEZEKANA, - Tuondoe cheo cha Makamu wa Raisi kupunguza gharama, kisha tuwe na Vyeo viwili tu vikubwa Cha Raisi wa JMT na cheo cha Waziri Mkuu, Lakini Waziri Mkuu huyu apatikane kutoka upande wa pili wa Muungano( Yaani kama raisi atatoka bara, Waziri Mkuu atoke Zanzibar) na athibitishwe na Mabunge yote mawili (Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi), Kama bunge moja kati ya hayo mawili litamkataa basi atafutwe mwingine.

FAIDA ZAKE NINI
  • Kutakuwa na Waziri Mkuu mtendaji, Mwenye Mandate ya kufanyia kazi mambo ya muungano kwenye pande zote mbili akiwa anajiamini kwa kuwa kapitishwa na mabunge yote mawili
  • Itapunguza gharama za uendeshaji wa serikali
  • Tutapunguza gharama za kuhudumia Wastaafu, tufahamu wazi kuwa Kila mstaafu katika wale viongozi wetu wakubwa yaani rais, makamu, waziri mkuu n.k wanaendelea kupata mishahara minono na stahiki nyingi sana, Tukiondoa cheo cha makamu wa rais tutapunguza gharama
HITIMISHO
  • Ukisoma majukumu ya Waziri mkuu na Makamu wa Raisi kwa mujibu wa katiba, kuna sehemu majukumu yao yanafanana, nayo ni "Kupangiwa kazi yoyote na raisi kadri atakavyoona inafaa", Sasa kama hili linawezekana maana yake ni kwamba inawezekana kabisa Waziri mkuu kufanya majukumu ya kawaida ya kila siku ya makamu wa raisi "kama akiagizwa na raisi", sasa kwa nini tuwape kazi ileile watu wawili wakati mmoja anaweza kuifanya?-TUTUMIE VIZURI KODI ZA WANANCHI TUONDOE CHEO CHA MAKAMU WA RAISI
  • Pili, Hiki cheo cha kungoja raisi asiweze kutimiza majukumu yake ili mtu ahesabiwe kuwa eti kusubiri kwake huko ni sehemu ya kazi yake halafu kila mwezi tuendelee kumlpia mshahara, mimi nadhani huu ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi
  • Hakuna chochote kile kinachofanywa na ofisi ya Makamu wa Raisi ambacho hakiwezi kufanywa na ofisi ya Waziri Mkuu mwenye mandate iliyoshiba ya nchi nzima, Kwa maoni yangu Cheo cha Waziri Mkuu kinatutosha, Cheo cha makamu wa rais kinaongeza mzigo kwa Taifa!

maana ya makamo wa raisi ni sawa hospitali kuwa na madaktari wawili. wanao tibu hakiwepo huyu hata msaidia mwengine
 
Ngoja wengine wenye damu ya Kunguni kuelekea ' Krismasi ' hii tunyamaze.
 
Muungano ufe kila mmoja akae kwake kwani pesa inayotumika kuubembeleza kuulea muungano, kuwalipa mishahara utitiri wa watumishi Zanzibar ikibakia Tanganyika ujue kuwa Tanganyika itakuwa Nchi tajiri kuliko Nchi zote barani Africa kwani pesa inayotumika huko Zanzibar ni kubwa mno kupita wanachozakisha wao kama visiwa, Hazina ya Tanganyika inamenyeka kuwalisha Zanzibar ambao huwa hawana shukrani na mda wote hulalamika na wanataka muungano Ufutike ili waolewe na kufunga ndoa na Oman wakidhani Zanzibar itakuwa kama Dubai wana ndoto nyingi za asubuhi saa 12 .
Mkuu kama ndivyo, washawishi wakubwa waiache Zanzibar ili uchumi wa Tanganyika unawiri. Nionavyo ni kinyume na uonvyo wewe, na hii ndio kibinadamu. Tafadhali anza hiyo kampeni.
 
Mfano sasa hivi Rais ni Pombe. PM ni Majaliwa. Ukimwondoa Samia, Zanzibar watakosa uwakilishi nafasi za juu.

Dhana ya running mate ni kwamba kati ya Rais na Makamu wake, mmoja akiwa Mtanganyika, mwingine awe Mzanzibar
 
Majukumu ya Makamu wa Rais yanaweza kufanywa kwa urahisi sana na ofisi ya waziri mkuu, hivyo basi itakuwa ni jambo la busara endapo cheo hiki kikafutiliwa mbali, na majukumu yake akapewa Waziri mkuu, maana hata hivyo hakuna kazi yeyote inayoonekana moja kwa moja ikifanywa na makamu wa Raisi, kikubwa ni kusibiri mtu atangulie ili ashike kiti cha urais, hakuna lingine.

Kuna tetesi nazisikia huko, eti kuna bilioni 18 zinatumika kumjengea ofisi Makamu wa Rais, nadhani hii habari ni ya upotoshaji, sitaamini hadi nione kwa macho yangu hiyo ofisi ikijengwa kwa pesa hizo; hii habari itakuwa ni ya uzushi, nchi hii hakuna taahira wa kupitisha bajeti ya bilioni 18 kujenga ofisi.

Taahira wa hivyo hajazaliwa bado, tusidanganyane hapa..; hostel za Magufuli zilijengwa kwa bilioni 10, na leo vijana wanajiachia tu pale, sasa ofisi ya bilioni 18? Ridiculous joke!
 
Sasa atakae kata tepe za makanisani atakuwa waziri mkuu?


Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Huwajui ccm wewe! Chato unakuwa mkoa soon ndio wafute VP?
 
Hii nchi ni maskini kwa sababu Mapato yake karibu yote yanatumika kwenye utawala.

Hiyo ndiyo siri kubwa ya CCM kungangania madaraka makubwa yabaki kwa Rais na wakubwa ili waendelee kuneemeka kupitia maofisi na miradi ya kuwajengea maofisi huku wananchi na wafanyakazi wa Chini wakiwa hawana makazi bora ya kuishi.

Tanzania tungekua na uchumi mkubwa kama Uingereza nadhani Jengo la Bunge au ofisi ya Malkia ingejengwa inayoelea angani kwa dola trili. 100.

Watawala ni tofauti sana na viongozi. Tanzania tuna watawala. Watawala wanawaza ufahari na kuwa juu ili waogipwe na kuheshimiwa.

Viongozi wanaonyesha njia ya kutoka kwenye utumwa na unyonge wa jamii. Afrika na Tanzania bado tuna watu wanaopenda kutawala wengine. Mtu anapewa nafasi kwa miaka mitano lakini ukichunguza muda wote huo anachoangalia ni kujenga hofu kwenye jamii ,kujikweza na kuifanya jamii imuogope na kumwona ni mtu wa hali ya juu asiyehojiwa wala kukosolewa wala kulaumiwa . Watawala wanapenda kusifiwa tuu na kuheshimiwa tu hata kwa Lazima.

Hivyo hatutashangaa ikijengwa ofisi kwa mabilioni ya fedha kwenye nchi inatotegemea miamala kujiendesha.

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Huwajui CCM au wewe sio wa nchi hii, au ni nini?

Unafikiri wanajali matumizi sahihi ya kodi? Basi jitayarishe, kama umesikia ujue hilo balaa linakuja. Waliuza nyumba zote za serikali muda mfupi kabla ya Rais kumaliza muda wake.

Rais aliyefuata kama kawaida akafanya mabadiliko, wateule wote walikaa mahotelini kwa miaka. Ni mabilioni mangapi yaliyoteketea, kuna anayejali?
 
Huwajui CCM au wewe sio wa nchi hii, au ni nini?

Unafikiri wanajali matumizi sahihi ya kodi? Basi jitayarishe, kama umesikia ujue hilo balaa linakuja. Waliuza nyumba zote za serikali muda mfupi kabla ya Rais kumaliza muda wake.

Rais aliyefuata kama kawaida akafanya mabadiliko, wateule wote walikaa mahotelini kwa miaka. Ni mabilioni mangapi yaliyoteketea, kuna anayejali?
Aisee, ila hii ofisi kwa bilioni 18 hapana, nasisitiza, waunganishwe na ofisi ya waziri mkuu, hiki cheo kife, awamu ya 6 ndio iwe ya mwisho kubeba huu mzigo! Umakamu wa Rais ni mzigo kwa wanachi!
 
Mkuu hili mbona lipo wazi, kama ni swala la succession plan endapo rais atashindwa kufanya majukumu mbona yupo spika wa bunge na jaji mkuu? mmojawapo anaweza kukaimu madaraka ya rais na uchaguzi kuitishwa katika kipindi cha miezi sita.
 
Back
Top Bottom