Cheo cha Makamu wa Rais hakina tija, tukiondoe, tubakishe cha Waziri Mkuu

Cheo cha Makamu wa Rais hakina tija, tukiondoe, tubakishe cha Waziri Mkuu

We unajielewa kweli? Makamu wa Raisi hupangiwa kila kitu , ni Kati ya watu ambao ni high power Ila hawana nguvu ya maamuz , hawezi fanya chochote Kwa kujiamulia
Basi atoke tu, Katiba ifanyiwe amendment arudi chuoni akashike chaki, mshahara wake wa mwezi unalipa zaidi ya walimu Mia moja wa sekondari
 
Hiki cheo cha vice president kifutwe tu hakina kazi. Tangu aingizwe madarakani hakuna lolote lile tumesikia kutoka kwake zaidi ya kwenda airport kumsubiri mama ampokee. Anakula kodi zetu bure tu. Aina hii ya viongozi ni mzigo na hasara kwa taifa, sijui kwanini wasomi wa bongo akili zao hazileti matokeo chanya kwa taifa.

Huyu ni mwanauchumi wa makaratasi tu lakini utendaji ni zero kabisa, yupoyupo kuinama na kukunja mikono kumsalimia aliyemteua. Hii Safu kwanzia Rais, Makamu wake na waziri mkuu hapa tumepigwa hawafai hata kuwa monitor wa darasa la tatu. Ni unproductive wapo kuzunguka tu kila siku wanawaza kukutana na mzungu hali za wananchi zinazidi kuwa ngumu. Wananchi tusipobadilika kukataa viongozi wachumia tumbo tutaburuzwa maisha yetu yote.
Naunga mkono hoja.
 
Hii nafasi nilisema apewe Majaliwa ila basi tu watu wabishi mno pale juu.
 
Hicho cheo kilianzishwa kwa ajili wa kuwatawala watu wa Zanzibar, safari hii Mungu ameona sisi wa Bara kuanza kutawaliwa then mnaingiza hasira.
Nyakati za tawala zote watu watu walikua kimya...na sisi tuwe kimya.
Sheria ni msumeno, mama tunae hadi 2030 ndo akili itatukaa sawa na ukoloni mamboleo.
 
Hiki cheo cha vice president kifutwe tu hakina kazi. Tangu aingizwe madarakani hakuna lolote lile tumesikia kutoka kwake zaidi ya kwenda airport kumsubiri mama ampokee. Anakula kodi zetu bure tu. Aina hii ya viongozi ni mzigo na hasara kwa taifa, sijui kwanini wasomi wa bongo akili zao hazileti matokeo chanya kwa taifa.

Huyu ni mwanauchumi wa makaratasi tu lakini utendaji ni zero kabisa, yupoyupo kuinama na kukunja mikono kumsalimia aliyemteua. Hii Safu kwanzia Rais, Makamu wake na waziri mkuu hapa tumepigwa hawafai hata kuwa monitor wa darasa la tatu. Ni unproductive wapo kuzunguka tu kila siku wanawaza kukutana na mzungu hali za wananchi zinazidi kuwa ngumu. Wananchi tusipobadilika kukataa viongozi wachumia tumbo tutaburuzwa maisha yetu yote.
Anasubiri litokee kama la 17 March aende front
 
Hicho cheo kilianzishwa kwa ajili wa kuwatawala watu wa Zanzibar, safari hii Mungu ameona sisi wa Bara kuanza kutawaliwa then mnaingiza hasira.
Nyakati za tawala zote watu watu walikua kimya...na sisi tuwe kimya.
Sheria ni msumeno, mama tunae hadi 2030 ndo akili itatukaa sawa na ukoloni mamboleo.
Akili zako hazipo Sawa nenda hospital Sasa hivi
 
Hiki cheo cha vice president kifutwe tu hakina kazi. Tangu aingizwe madarakani hakuna lolote lile tumesikia kutoka kwake zaidi ya kwenda airport kumsubiri mama ampokee. Anakula kodi zetu bure tu. Aina hii ya viongozi ni mzigo na hasara kwa taifa, sijui kwanini wasomi wa Bongo akili zao hazileti matokeo chanya kwa taifa.

Huyu ni mwanauchumi wa makaratasi tu lakini utendaji ni zero kabisa, yupoyupo kuinama na kukunja mikono kumsalimia aliyemteua.

Hii safu kwanzia Rais, Makamu wake na waziri mkuu hapa tumepigwa hawafai hata kuwa monitor wa darasa la tatu. Ni unproductive wapo kuzunguka tu kila siku wanawaza kukutana na mzungu hali za wananchi zinazidi kuwa ngumu. Wananchi tusipobadilika kukataa viongozi wachumia tumbo tutaburuzwa maisha yetu yote.
Vyeo vipo kugawana ulaji tu,
Jiulize kuna wabunge wangapi kutoka Zanzibar bungeni wakijadili mambo yasiyo ya muungano,
Mfano wanajadili mradi wa maji Bariadi na wanalipwa salary na posho zote,
Angalia idadi ya watu na wabunge wa Zbar
na ukubwa wa eneo,
Na wakati huohuo wana bunge lao(Baraza La Wawakilishi) ambalo hakuna Mtanganyika anayeruhusiwa kuingia humo.
Tunahitaji marekebisho kuboresha Muungano wetu,
 
Kuna yule mwingine alikuwa na koti kuubwa kumbe mfukoni alikuwa anachukua mkasi kazi yake kukata tepe
 
Akili zako hazipo Sawa nenda hospital Sasa hivi
Kama utaki kukubali kuwa cheo Cha Vice President pamoja na hizo job description kwa ajili kuwalambisha watu wa Zenji ni wewe... Ila ukweli ndo hiyo.
Nitajie makamu wa Rais aliewahi kufanya Jambo la maana ili Mimi niwahi Hospitali.
 
Nchi yetu ni nchi masikini, kutokana na hali hiyo ni muhimu kila senti inayopatikana ikatumika vizuri.
Leo hii nchi yetu ina viongozi wakubwa wafuatao
1. Rais
2. Makamu wa Rais
3. Waziri Mkuu
4. Rais wa Zanzibar
5. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
6. Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar

Ukiangalia kwa muundo huu wa serikali zote mbili ya Muungano na ya Zanzibar, hii ni serikali kubwa sana, viongozi hawa wote kila ofisi yake ina bajeti kubwa tu inayopitishwa na bunge/Baraza la wawakilishi kila mwaka. Ili kubana matumizi tunahitaji serikali ndogo lakini yenye ufanisi wa hali ya juu!

Leo hii Waziri Mkuu ana bajeti, lakini ukikaa chini na kuchunguza utaona kimuundo Waziri Mkuu anatumika zaidi Upande wa Tanganyika kuliko Zanzibar (Sijiu ni ziara ngapi za kitendaji Waziri Mkuu amekwenda kufuatilia shughuli za kila siku za serikali huko Zanzibar kama afanyavyo katika mikoa ya huku Tanganyika).

Ukichunguza, utaona kwamba Mamlaka ya Waziri mkuu kwa huko Zanzibar yamekasimiwa kwa Makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar (Cheo ambacho zamani kilikuwa ni Waziri kiongozi), Hata kwa mambo ambayo ni ya Muungano utaona kuwa kwa huko Zanzibar yanafanywa na ofisi hii badala ya Waziri Mkuu!. Sasa hapa tunapokuja katika Bajeti, huu ni mzigo mkubwa kwa Walipa kodi wa nchi hii, kuhudumia Ofisi mbili za mambo yaleyale!

Tukija kwenye ofisi ya Makamu wa Raisi, Utaona kwamba majukumu yake ni kumsaidia raisi pindi raisi akiwa hayupo ofisini na pia kuna majukumu machache tu ambayo katiba imempa, angalia ibara hii ya katiba hapa chini kuhusu madarka ya makamu wa raisi.


View attachment 975882

Katika mazingira haya, Je ni kitu gani kilishindikana Kuunganisha Majukumu haya machache ya ofisi ya makamu wa raisi ili yaingie katika ofisi ya Waziri Mkuu na hivyo kusaidia kupunguza matumizi ya pesa ya Umma kwenye kugharamia ofisi hii?

HOJA YA KULINDA MUUNGANO KWA MUUNDO HUU INA MANTIKI?

Utaratibu wa sasa unasema kuwa kama Rais atatoka upande mmoja wa muungano basi Makamu atoke upande wa pili, lengo hapa ni kuwa na uwakilishi wa pande mbili katika serikali, lakini cha kujiuliza Je haiwezekani tukawa na Utaratibu mwingine mzuri na ulionafuu kiuendeshaji kuliko wa sasa?- NAAMINI INAWEZEKANA, - Tuondoe cheo cha Makamu wa Raisi kupunguza gharama, kisha tuwe na Vyeo viwili tu vikubwa Cha Raisi wa JMT na cheo cha Waziri Mkuu, Lakini Waziri Mkuu huyu apatikane kutoka upande wa pili wa Muungano( Yaani kama raisi atatoka bara, Waziri Mkuu atoke Zanzibar) na athibitishwe na Mabunge yote mawili (Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi), Kama bunge moja kati ya hayo mawili litamkataa basi atafutwe mwingine.

FAIDA ZAKE NINI

  • Kutakuwa na Waziri Mkuu mtendaji, Mwenye Mandate ya kufanyia kazi mambo ya muungano kwenye pande zote mbili akiwa anajiamini kwa kuwa kapitishwa na mabunge yote mawili
  • Itapunguza gharama za uendeshaji wa serikali
  • Tutapunguza gharama za kuhudumia Wastaafu, tufahamu wazi kuwa Kila mstaafu katika wale viongozi wetu wakubwa yaani rais, makamu, waziri mkuu n.k wanaendelea kupata mishahara minono na stahiki nyingi sana, Tukiondoa cheo cha makamu wa rais tutapunguza gharama
HITIMISHO
  • Ukisoma majukumu ya Waziri mkuu na Makamu wa Raisi kwa mujibu wa katiba, kuna sehemu majukumu yao yanafanana, nayo ni "Kupangiwa kazi yoyote na raisi kadri atakavyoona inafaa", Sasa kama hili linawezekana maana yake ni kwamba inawezekana kabisa Waziri mkuu kufanya majukumu ya kawaida ya kila siku ya makamu wa raisi "kama akiagizwa na raisi", sasa kwa nini tuwape kazi ileile watu wawili wakati mmoja anaweza kuifanya?-TUTUMIE VIZURI KODI ZA WANANCHI TUONDOE CHEO CHA MAKAMU WA RAISI
  • Pili, Hiki cheo cha kungoja raisi asiweze kutimiza majukumu yake ili mtu ahesabiwe kuwa eti kusubiri kwake huko ni sehemu ya kazi yake halafu kila mwezi tuendelee kumlpia mshahara, mimi nadhani huu ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi
  • Hakuna chochote kile kinachofanywa na ofisi ya Makamu wa Raisi ambacho hakiwezi kufanywa na ofisi ya Waziri Mkuu mwenye mandate iliyoshiba ya nchi nzima, Kwa maoni yangu Cheo cha Waziri Mkuu kinatutosha, Cheo cha makamu wa rais kinaongeza mzigo kwa Taifa!
Andiko zuri ila ungeweza kuliboresha zaidi. Hakuna muungano wa nchi mbili halafu zikabaki kuwa nchi mbili au moja na serikali mbili, huo ni UNAFIKI. Hapa hamna muungano ni mazingaumbwe na sekeseske za viongozi. Vunja muungano au vunja nchi na serikali ya Zanzibar na kuunda nchi moja na serikali moja ya Tanzania....FULL STOP.
 
Hicho Cheo ni Ceremonial tu ndio maana hata JPM alivokufa, Makamu wake baada ya kusworn in akaanza kulalamika utawala wa JPM kama hakuwa sehemu ya utawala huo hio ina prove kuwa Cheo cha VP kipo tu kusubiri hali ya hatari kama kifo cha incumbent, Lakini naamini ofisi hii ya Vice president imesheheni watu wa kila aina ivo ofisi hii tunaihudumia kwa kodi zetu bila impact yoyote ile, Nashauri Office hii iwe demolished
 
Job desc yake iko wazi, ni nafasi ya kimkakati hasa kwa nchi yetu ya mfumo wa Muungano. Mara nyingi idara yake ni ile ya mazingira! Iko hivyo miaka yote!
 
Back
Top Bottom