China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

Hii inafariji sana.! Shukran za pekee kwa wachangiaji wote.
 
mku naomba kufahamu , ni kampuni gani inayohusika kununua na kusafirisha mzigo pasipokuwa na udanganyifu wowote?
Wapo watu binafsi/kampuni za kitanzania ambazo zina ofisi/maduka Tanzania na zinatoa huduma hiyo ya kununua na kusafirisha mzigo na unapokea mzigo wako kwenye ofisi/maduka yao yaliyopo Tanzania. Nitataja baadhi unaweza google na utapata mawasiliano yao. Baadhi ni silent ocean (wameanza kutoa huduma hii hivi karibuni), GNM Cargo, Tuagize Co.Ltd (mashine na vifaa vya ujasiriamali. Facebbook/Instagram@tuagizeltd), Afigreen (Vifaa vya ufugaji. Nadhani sina hakika sana ila Instagram pia wanatumia jina hili, ), Salome furniture/collection Dodoma (Furniture & Nguo). Pia wapo watu maarufu wengi wanaotoa huduma hiyo.
NB: Deal nao kwa kufuata taratibu salama.
 
Hili mkuu kama una mtaji mkubwa wa kuchukua kontena basi utapata kwa bei nzuri kiwandani na faida utaiona. Ila kama utachukua pcs chache (LCL) ili uje uchuuze Tanzania, basi ushauri wangu, tafuta supplier mkubwa Tanzania, nunua kwake na chuuza.
Mimi naulizia Ream paper, nitapata kwa bei gani kutoka china? gharama za usafirishaji na kodi vipi? Mwenye uzoefu anielekeze. Ahsante
 
Mkuu, SI RAHISI kama hivyo!. Buyer akupe pesa tu hivi hivi? Kwanza unatakiwa uwe ni kampuni iliyosajiliwa na uwe umefata sheria zote za kusafirisha bidhaa tajwa nje ya nchi.
Nimewahi kulitolea maelezo hili kwenye comments zilizopita. Tafuta utaona maelezo kwa kina.
Nikitaka kuexport mazao ya jamii ya kunde kama choloko, Dengu
inatakiwa niwe na mtaji wangu tu ? Kwani siwezi kunegotiate na buyers akanipa feza nikamukusanyia
maana ukiwa na mtaji kidogo biashra ya export ni ngumu
 
Hili nimeshajibu nadhani, ila kwa faida ya wengine, google kampuni hizi utapata mawasiliano yao kwenye mitandao ya kijamii. Zote zinatoa huduma hiyo unayohitaji
Silent ocean, Tuagize Co.Ltd, GNM cargo, Thebridgetz, Afigreen, Tanzania food processing club nk
 
uzi safi sana.. leo tu nimetuma usd zangu 3000 pale silent ocean...

huduma nimepata safi.. mdada mrembo recho na totoz za kiarabu zinapiga kazi safiiiiii...

kiukweli dunia sasa kama kijiji... kila unachotaka kinapatikana mikononi.mwako
Mkuu vp delivery time yao?
 

Mapembelo Cargo pia wapo vizuri sana
 
Hiyo machine ya kutengenezea ice cream/barafu! Unamaanisha hizi za Mia Mia au zile za bakhresa?
 
Habari mkuu,kwanza pongezi kwa kuanzisha uzi bora kabisa

Japo sijapitia thread zote za nyuma najua unaweza kua ulifafanua,ninachotaka kujua mimi ni jinsi unaweza kwenda na fedha nyingi china yani kama una dollar kuanzia elfu kwenda mbele maana pale airport huwa hawaruhus kupita na kiasi kikubwa cha fedha

Na je ukitaka kununua vitu china kwa kampuni zilizokua listed kwenye online platform ya alibaba kuna usalama kiasi yani niwatumie tu hela na mzigo uje bila mimi kwenda china inawezekana hicho kitu kwa uzoefu wako?

Na je hapa tanzania kuna bank ambazo zina ingiliana na bank za china yani kiasi kwamba nikiweka hela bongo hapa kwenye account na nikifika china nina toa bila shida kiasi kikubwa sio kwa ATM(visa) maana hapo nitatoa kidogo kidogo sana japo sijui masharti ya kule china yapoje kwenye masuala ya bank

Naomba uzoefu wako kwenye hili
 
Nina maanisha dollar za marekani elfu kumi kuendelea mbele.
 
kwenye kulipa alibbaba hapo hakikisha unalipia alibaba na sio kumlipa supplier..ila kwny kusafiri na hela hapo sjajua
 
Asante sana boss na vip kuhusu masupplier wachache unaoweza kutusaidia contact zao ambao viatu vyao viko vizuri na bei yake sio mbaya
Be bless
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…