China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

S

Safi sana. Ili tuendelee kama Taifa lazima tupeane info za msingi kwa haraka sana. Kila la heri
Just like Mapopo do! wako sharp katika kupeana infos za maana na nyeti,
Nipo interest na mashine ndogo za kuzalisha bidhaa majumbani,kama childs shoes and so on..!
 
Hili mkuu kama una mtaji mkubwa wa kuchukua kontena basi utapata kwa bei nzuri kiwandani na faida utaiona. Ila kama utachukua pcs chache (LCL) ili uje uchuuze Tanzania, basi ushauri wangu, tafuta supplier mkubwa Tanzania, nunua kwake na chuuza.

Kipilipili
Nikupongeze Sana sana personally na Wachangiaji wengine Software Engineer na socrate jr
Huu uzi ni very usefully 99%
Very Detailed na unatoa mwanga halisi wa Field mambo yalivyo.
Hujawa na uchoyo wa Taarifa mpak Figures nikupongeze sana.
Nimeusoma kuanzia saa 9 usiku Mpaka sasa
Nimejifunza mengi sana.
Concept ya MOQ minimum order quantity nimeielewa Vizuri Sana.(wabongo huwa wanajazana sana upepo hapo).
Uzi umetoa majibu ya maswali yote yanayotakiwa.
Ubarikiwe sana Sana.
Mwenyezi Mungu akubariki sana na wengine wote waliotoa miongozo mbali mbali.
Mbarikiwe Mpaka mshangae
 
Ndugu watanzania naomba niseme hili kwa dhati kabisa
Biashara za kuvuka Border zinalipa sana
Lakini shida kubwa wengi mtaji mdogo
Utanunua Bidhaa huko nje kwa Bei rahisi sawa lakini ukija kujumlisha nauli na malazi na chakula Faida yote unaiacha njiani
Kuna jamaa alijazwa upepo mtaani China [emoji630] mzigo Bei rahisi
Akachukua visenti vyake Mpaka huko ng’ambo
Mzigo kweli alipata kule kwa Bei rahisi
Ukija kujumlisha na nauli na kulala
Mpaka anafika Tanzania [emoji1241] unakuta mzigo unasimamia Bei zaidi ya Bei ya rejareja hapo kariakoo, waweza kudata
Nashauri Mtu apate taarifa za kutosha kabla hujaanza Safari
Wafanyabiashara Wote tujifunze sana somo Linaitwa PRODUCT COSTING
Ukilijua hilo hupati Shida kwenye kununua na kuuza
Ukifeli hapo hakuna muujiza wa wewe utoe faida Dukani
Cc: Kipilipili , socrate jr
 
Unachosema kina ukweli ndani yake. Mwanzoni mwa uzi huu nilitoa kabisa angalizo, anaekuja China anatakiwa aangalie vitu vingi sana na nimevieleza.
Watu wengi mtaani wanaamini China vitu ni rahisi na akija na mtaji wake basi atanunua na akifika Tanzania atauza tu kirahisi. Mambo ya kuzingatia
1. Gharama halisi mpaka mzigo unafika Tanzania itakuwa kiasi gani? Hapa ni muhimu mnunuaji wa bidhaa ajifunze kukadiria CBM za mzigo. Mfano kama unanunua mashine China, basi mbaki na kujua gharama za kununua, basi ujue makadirio ya ufungashwaji (Packing size) na hili ni rahisi, muulize muuzaji akwambie packing size. Au kama ni mashine basi hakikisha umepata vipimo vyake yaani urefu, upana na kimo halafu kadira itakapofungashwa (mfano kwa wooden package) itakuwa kiasi gani, yaani ongeza kidogo vipimo kutoka kwenye SIZE ya mashine kwa sababu ikifungashwa kuna size kidogo inaongezeka. Halafu jua utasafirisha kama mzigo mdogo (LCL) au kama unachukua kontena zima (FCL) basi jua mashine hizo zitaingia ngapi? Kama ni mzigo mdogo ambao utawapa mashirika ya kusafirisha basi jitahidi kujua wanacharge kiasi gani kwa cbm? Halafu fanya makadirio. Hapo utapata gharama halisi. Haya mambo ya kutojua gharama kamili, yaliwahi kuwakuta watu fulani. Walikuta sofa zinauzwa bei rahisi china. Wakazibeba. Bila kujua kua sofa zinachukua CBM nyingi na wao wakasafirisha kwa wasafirishaji wa kawaida kwa vile mzigo wao haukutosha kontena zima.
Gharama za usafiri walizopigiwa baada ya mzigo kufika, ilikuwa ni bora wangenunua Tanzania tu kutoka kwa makampuni makubwa ambayo huleta bidhaa zao kama full container na hivyo bei zao kuwa za nafuu.

Watu wengi wakiangalia bei za mtandaoni china wanaona ni rahisi tu, ama wanakuja kununua au wanaagiza. Mzigo ukifika bandarini unakuta gharama ni zaidi ya bei halisi sokoni Tanzania.

2. Timing: Ni muhimu kukadiria mpaka mzigo unafika Tanzania, hali ya soko ikoje? Kuna watu wanakuja kuchukua nguo, wakitaraji watauza kabla ya sikukuu halafu mzigo unafika baada ya sikukuu .Hapo tayari kariakoo mzigo kama huo ulishafika siku nyingi, ulishauzwa na bei ya soko iko chini. Hapo ni maumivu tu na hasara tupu.

Mara zote nashauri sana watu waanzie sokoni/wateja wao kabla ya kuamua kununua kitu china. hayo ni machache tu
 
Kumekuwa na changamoto kubwa mbili kwa watu wanaogiza vitu kwenye mitandao hii nguli ya Kichina
Bei ya mali kuwa rahis lakini usafiri kuwa bei kubwa.

Wengine njia za kufanya malipo kushindwa hasa pale supplier anapo demand Wechat payment.

Unique aircargo tumekuja kuwasaidia Watanzania wenzetu. Sisi tunasafirisha mizigo kwa njia ya ndege kutoka China Guangzhou mpaka Dar es Salaam na kama uko nje ya Dar tunakutumia mzigo wako.Tunafanya dola 10.5 kwa kilo.

Ukiwa na kilo nying kama 100 na kuendelea bei
itashuka
mzigo unakufikia kabla ya 2 weeka
tupigie 0652472486


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
ok
 
Duh nimetembelea websites ulizozitaja kweli bei rahisi ndo nafikiria kuhusu hizo gharama za usafiri NAFANYAJE natamani kuagiza Kipilipili
 
nakutumia namba PM ya mtu wa dukani DSM
Unaposema mambo yote mfanyie kwenye alibaba hii ina maana gani? Mfano mm nimempata supplier kupitia alibaba na baada ya kuchat pale tukatumia whatsap kwa mawasiliano rahic ,je hii inaweza kuwa mawasiliano nje ya Alibaba?
 
waone unique aircacrgo namba zao za simu ni 0652472486 hawa ni mabigwa wa usafir wa anga kwa sas ofis zao zipo kariakoo mtaa wa pemba na livingstone na china wapo pale lujing road xiaboi siku 13 ushapaata mzigo wako kwa bei ndogo sana
Mkuu unawajua vizuri hawa?
 
Wasalam wakuu,naomba kujuzwa,je, ukiwa million I kumi na tank(Tsh.15,000,000)inatosha kufuata mzigo (nguo za watoto wachanga) Guangzhou?hapo ni nje na nauli! Natanguliza shukrani.
 
Nadhani hujanielewa. Hizo bidhaa ulizotaja ZIPO KWA WINGI kwa hiyo demand si kubwa kama NYAMA YA NG'OMBE
Vigezo vipi unatakiwa uvikamilishe ile uweze kupata vibali vya kuuza nyama ya ng'ombe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…