DENG XIAOPING
JF-Expert Member
- Mar 6, 2022
- 2,396
- 2,598
Kwani mkuu huu mgogoro tunao uzungumzia hapa tuna ufananisha na wa Russia na Ukraine ?Nilichopinga ni kutuletea baraza la maamuzi la China kana kwamba urusi putin ndo aliamua kuvamia
Ukitaka kujua ukatili wa china waulize India kule mipakani au Pakistan.Mabeberu yameshamgundua china kuwa ni chui wa karatasi! Chui wa karatasi ana sura ile ile ya chui na ametoa meno lakini hawezi kuuma!! Ni sawa na nyoka wa kibisa ambaye hata watoto huwa wanaweza kucheza naye maana alishatolewa meno!
China ilibweka sana kutishia Spika wa bunge la marekani Pelosi asitembelee Taiwan ambayo kimsingi ni sehemu ya china!! Akaandaa mameli na midege ya kijeshi lakini kumbe wenye akili zao walijua anatishia nyau na Pelosi alienda Taiwan na Kurudi bila shida yoyote! baada ya hapo china ikaizingira Taiwan kwa mimeli ya kijeshi pande zote na ikafanya mazoezi ya kijeshi ya kufa mtu lakini mabeberu wakamcheka tu na hujiendea Taiwan na kurudi na china kuishia kubweka hadi aibu!!
Hivi sasa tunavyozungumza kuna ziara nzito ya wabunge wa Canada wakitembelea Taiwan "nchini China" kinyume na matakwa ya China na bila aibu China imebweka tena huku ikijua kuwa imeshagundulika kuwa ni "chui wa karatasi". Ili kuondokana na aibu hii mara mia China iamue kuachana rasmi na Taiwan na kuitangazia uhuru wake kuliko hii aibu ya kubweka kila leo huku dunia nzima inajua ubavu wa kung'ata haina!!
Isijidanganye kuwa miongoni mwa wababe ambao wakisema kitu huwa hawapepesi macho!! Hapo ndipo ninapoziheshimu nchi kama Iran, Korea ya kaskazini, Uturuki na baba lao Urusi!!
Beijing fumes over latest foreign visit to Taiwan
A trip to Taipei by Canadian lawmakers “grossly interfered” in China’s internal affairs, Beijing said
[emoji2398] Twitter / MOFA_Taiwan
The Chinese government has condemned a recent visit to Taiwan by Canadian MPs, demanding that Ottawa cease direct diplomatic ties with the island and respect its territorial claims.
In a statement issued to the Globe and Mail on Thursday, China’s embassy in Canada denounced a trip to Taiwan by Liberal lawmaker Judy Sgro and other members of the ‘Canada-Taiwan Parliamentary Friendship Group,’ which began last Sunday.
“China has consistently and firmly opposed any form of official exchanges between the Taiwan region and countries having diplomatic ties with China,” it said, adding that the visit “blatantly violates the one-China principle, grossly interferes in China’s internal affairs and sends a seriously wrong signal to the ‘Taiwan independence’ separatist forces.”
Unabishana na watoto wa jana Mkuu,Kwanza kabla ya yote nikuulize swali moja: Mkuu mgogoro wa PRC na ROC umeanza kuufatilia toka lini [ mwaka gani ] ?
Hiyo hata wa shule wanajua ipo kwenye vitabu dogo weweKwa taarifa yako mimi nakimbilia miaka 70!! Mgogoro huu ninaujua toka vita vyao vya wenyewe kwa wenyewe enzi ya Mao!! Hao walioko Taiwan walishindwa vita wakakimbilia kisiwa cha Taiwan!! Kubali tu kunipa shikamooo!!
Ndio china hana Sera ya vita yupo kimkakati wa biashara zaidi,anajua anapotokaTuliwahi kusema humu toka vita ya Ukraine na Russia inaanza, tukasema China atakaa mbali kabisa na Russia sababu hawezi kugombana na watu ambao wamemfanya awe tajiri namna hii.
Hilo la kwanza, la pili. Ubabe usiokuwa na maana kama wa Russia umeshapitwa na wakati, China amestaarabika mno.
Sijasema hivyo lakini nimesema huo mgogoro wa 1927 haukuzaa Taiwani iliyojitenga ambayo ndiyo tunayoiongelea leo!Kwa hiyo mkuu mwaka 1927 mpaka mwaka 1936 China CPC/PLA haikupigana na Kuomitang/CNA ?
Kama hivyo ndivyo, anapiga makelele ya nini? analalamika nini? ukishajua wewe ni nyumba ya udongo hauhimili vishindo inabidi uwe mpole!!Ndio china hana Sera ya vita yupo kimkakati wa biashara zaidi,anajua anapotoka
USSR
Ila huo mgogoro wa 1927 ulizaa nini ?Sijasema hivyo lakini nimesema huo mgogoro wa 1927 haukuzaa Taiwani iliyojitenga ambayo ndiyo tunayoiongelea leo!
Mchina anakwambia Kwa msemo wao local kwamba " all the great battles are won without fighting "View attachment 2386678
Hawa top elite wa China sio wajinga wala wazembe kama wewe unavyo tanabaisha hapa , maamuzi yote wanayo fanya China yana fanyiwa upembuvi akinifu kuliko wewe unavyo dhani. China imefanya ukombozi na kurudisha maeneo yake mbalimbali mengi sana mfano Tibet, Hong Kong , Macau tena mengine bila kurusha hata risasi hata moja usiwachukulie China kawaida .
Haya mambo tuwa achie wataalamu wenyewe wa CPC na PLA wamalize Vita vyao vya wenyewe kwa wenyewe na hao ROC katika njia wao wanayo ona ni bora zaidi, haya mambo yanahitaji mipango sio mihemko kama unavyo dhani.
Maamuzi yote ya China lazima yapite humu na kuwanyia upembuvi akinifu ndipo yatekelezwe[emoji116]
View attachment 2386691View attachment 2386692View attachment 2386693View attachment 2386694
: Tusubiri maamuzi ya chama kuanzia Oktoba 16 nini kitajadiliwa hapo Great Hall of people Beijing tutajua ni namna gani PRC watalikabili swala la mgogoro wao na ROC.