China: Marekani chagua moja unataka vita ama ushirikiano?

China: Marekani chagua moja unataka vita ama ushirikiano?

Mnada wa Mhunze

Senior Member
Joined
Mar 1, 2023
Posts
168
Reaction score
819
China.jpg

Mwanadiplomasia mkuu wa China amesema chanzo kikuu cha msuguano katika uhusiano kati ya China na Marekani ni "mtazamo mbaya" wa Marekani kuhusu nchi yake.

Wang Yi alimwambia Blinken "hakuna nafasi ya majadiliano" juu ya Taiwan, kulingana na taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya China baada ya mkutano huo.

Pia aliitaka Marekani kuondoa vikwazo vya upande mmoja dhidi ya China, "ikomeshe ukandamizaji" wa maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China, na kutoingilia mambo ya ndani ya China.

"Lazima kuwe na chaguo kati ya majadiliano au makabiliano, ushirikiano au migogoro," amesema


BBC.
 

Mwanadiplomasia mkuu wa China amesema chanzo kikuu cha msuguano katika uhusiano kati ya China na Marekani ni "mtazamo mbaya" wa Marekani kuhusu nchi yake.

Wang Yi alimwambia Blinken "hakuna nafasi ya majadiliano" juu ya Taiwan, kulingana na taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya China baada ya mkutano huo.

Pia aliitaka Marekani kuondoa vikwazo vya upande mmoja dhidi ya China, "ikomeshe ukandamizaji" wa maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China, na kutoingilia mambo ya ndani ya China.

"Lazima kuwe na chaguo kati ya majadiliano au makabiliano, ushirikiano au migogoro," amesema


BBC.
Kwaiyo China wanapapatua waondolewe vikwazo vya technologia ya sayansi, ndio maana tulikuwa tunawambia humu kwamba China technolojia yake yote aliyonayo ipo chini ya US na kwamba China hawezi kununa na US maana ndie anayemuweka mjini.
 
Si ndo hawahawa walisema Spika wa US asifike Taiwan? Wakawa na mazoezi mazito ya kijeshi? Mwisho wa siku Peros akatua salama na kuondoka salama.
Tena US walivyokuwa wahuni yule mama walimpandisha ndege ya Rais Air Force One, ili kama China ataangusha ndege ya Rais wa US kuwe na sababu ya maana kwa US kumshughulikia Mchina lakini wachina wakabaki kuisindikiza ile ndege kwa macho tu, maamae
 
Wachina wamenifurahisha sana kwa kuwa wawazi kimsimamo


"Eidha majadiliano au walibwage"
Uwazi uko wapi mkuu mchina analalamika aondolewe vikwazo vya teknolojia ya sayansi, bado tu hujafumbua macho kwamba mchina anaekwa mjini ni US.
 
Kwaiyo China wanapapatua waondolewe vikwazo vya technologia ya sayansi, ndio maana tulikuwa tunawambia humu kwamba China technolojia yake yote aliyonayo ipo chini ya US na kwamba China hawezi kununa na US maana ndie anayemuweka mjini.
Sio kweli, USA ndo anaweka vikwazo Kwa mchina asiuze teknojia yake Marekani na washirika wa china kama vile Irani na Rusia
 
Uwazi uko wapi mkuu mchina analalamika aondolewe vikwazo vya teknolojia ya sayansi, bado tu hujafumbua macho kwamba mchina anaekwa mjini ni US.
Marekani imepiga ban Huawei, ZTE, TikTok n.k

Kitendo cha kuzipiga ban hizo ni ukandamizaji wa maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China

Ndicho alichomaanisha Bwana Wang Yi
 
Marekani imepiga ban Huawei, ZTE, TikTok n.k

Kitendo cha kuzipiga ban hizo ni ukandamizaji wa maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China

Ndicho alichomaanisha Bwana Wang Yi
Lakini YouTube, Facebook, WhatsApp, Google zilipigwa ban china kitambo sana. Hii inakula kotekote

Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom