China vs USA: Infrastructure, Technology and Development


Hizo habari za kusema majengo fulani na fulani ya China yamebuniwa na raia wa US ameleta nani hapa kama sio wewe na zina uhusiano gani na nchi gani imemzidi mwenzie kimiundombinu ?
 
Hizo habari za kusema majengo fulani na fulani ya China yamebuniwa na raia wa US ameleta nani hapa kama sio wewe na zina uhusiano gani na nchi gani imemzidi mwenzie kimiundombinu ?
Nisome tena unielewe, mdau!

Nimekataa hicho kipimo cha idadi ya miundombinu. Kipimo hicho hakizingatii utofauti uliopo kati ya hizo nchi mbili. Isitoshe, ulinganisho unakosa nguvu kwa sababu mmoja wapo hapo (USA) ni mhusika katika usanifu wa miundombinu kadhaa mashuhuri za pande zote mbili.
 
May you please come with supportive evidence mkuu,

Kuhusu panama canal, steel industry, na suspension bridge technology.
 
May you please come with supportive evidence mkuu,

Kuhusu panama canal, steel industry, na suspension bridge technology.

 
Nani ameichukulia China kama Malawi? Hoja zako ziko kishabiki zaidi kuliko kisomi!

Wewe unazungumzia construction wakati mimi nazungumzia architecture. Hapo ndipo tatizo lilipo. Hakuna construction bila architecture.
Mzee acha hizo. Hebu leta hizo facts hapa na references zake.
 
Nani aliyesema Great Wall of China imejengwa na USA?
Mzee umesema USA ipo na architects bora eti ndio wanao design majengo ya china!!!! Hahahaha!!! Nimekuuliza sasa hiyo Great Wall iliyojengwa 2000 years ago nani ali design?
 
Nembo Zina signify uthabiti wa Taifa, Eagle vs Dragon. Sijui kwanini sisi tulichagua Twiga
Twiga anakula majani kutokana na urefu wa shingo, ndio sisi tunakula kutokana na urefu wa kamba..na raia namba moja kalibariki hili.
 
Hata ukienda Marekani kuna majengo mengi tu yamesanifiwa na makampuni ya nje ya Marekani
 
Mzee acha hizo. Hebu leta hizo facts hapa na references zake.
Construction na architecture ni vitu viwili tofauti.

Anayefanya construction ya majengo ya kisasa anatumia nyenzo (tools/equipments) zilizopo tayari pamoja na design/blueprint kutoka kwa aliyefanya architecture.

Anayefanya architecture anatumia ubunifu na ujuzi wa kiufundi (creative and technical skills) ili kuunda majengo (design/blueprint) kabla hata ya mchakato wa construction kuanza.

Kazi ya architecture katika karne hii inahitaji qualifications na ujuzi zaidi kuliko construction.

Mfano: Kwa nchi kama Marekani, wala hauhitaji university degree ili kuwa licensed contractor wa majengo, wakati ili uwe licensed architect ni lazima uwe na kisomo cha juu zaidi kuanzia degree. Nafikiri hata kwa Tanzania ni vivyo hivyo.

Soma zaidi tofauti zao hapo chini (zingatia sana hizo sehemu nilizopigia mstari mwekundu):



Links:
 
Kwa hiyo unamaanisha nini mkuu?
 
Mzee umesema USA ipo na architects bora eti ndio wanao design majengo ya china!!!! Hahahaha!!! Nimekuuliza sasa hiyo Great Wall iliyojengwa 2000 years ago nani ali design?
Great Wall of China uliochukua miaka zaidi ya 2000 kuujenga ukakamilika has nothing to do with 21st century architectural needs and technology!

Kama tunazungumzia nyanja ambazo zinagusa wananchi wa pande zote moja kwa moja (kwa mujibu wa maneno yako mwenyewe), tunapaswa kuzingatia wakati uliopo sasa na mahitaji ya sasa ya watu wa hizo nchi mbili.

Great Wall of China imebaki kama sehemu ya utalii tu. Dhumuni la ujenzi wa huo ukuta lililokuwepo miaka hiyo halipo tena hivi sasa, ndio maana nimesema it has nothing to do with 21st century architectural needs and technology.

Again, unatumia mzani usio sahihi kulinganisha hizo nchi mbili. Kwamba USA nayo ilipaswa kuwa na Great Wall of USA miaka 2000 iliyopita ili kuonesha uwezo wake wa kimiundombinu wa sasa hivi? Wrong!

Uwezo wa USA katika miundombinu za kisasa unajionesha katika baadhi ya miradi mikubwa iliyopo China na duniani kote hivi sasa. Nimesema na nimeleta facts hapa za kutosha.

Katika majengo 10 marefu zaidi duniani, Marekani imehusika kwenye usanifu wa majengo takribani 6. Majengo yote ya China yaliyopo kwenye hiyo list yanaihusisha Marekani katika architectural design.

List hii hapa; architects wa hayo majengo wametajwa humo:
 
Hata ukienda Marekani kuna majengo mengi tu yamesanifiwa na makampuni ya nje ya Marekani
Mjadala ni kati ya Marekani na China. Marekani imehusika zaidi kwenye uundwaji wa miundombinu za kisasa za China kuliko ambavyo China imehusika kwenye miundombinu za Marekani.
 
Swali moja tu kwako Venus Star kati ya China na makao makuu ya dunia, USA, unaenda wapi?
 
Wakuu hivi picha ya mnyama inayowakilisha nchi Huwa inaakisi nchi ilivyo? Kama tai,nyoka ,twiga nk
 
Hiyo kampuni inadeal na architecture wala sio mipango miji.

China iko katika boom ya ujenzi kukuta kampuni za kigeni za usanifu majengo zikifanya kazi ni kawaida

Kama ni hivyo mbona kuna kampuni za China zinafanya ujenzi Marekani.

Kwa mfano kuna inayoitwa China Construction America inajenga majengo marefu, hotel, barabara, na madaraja n.k huko USA

Na hata headquarters yake iko Washington. Soma hiyo link hapo uone na projects wanazofanya na walizofanya Marekani

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…