China yailaani Tume ye Umoja wa Ulaya kwa kutaka siri za kibiashara katika uchunguzi wa magari ya umeme

China yailaani Tume ye Umoja wa Ulaya kwa kutaka siri za kibiashara katika uchunguzi wa magari ya umeme

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
1720422400369.png


Wizara ya Biashara ya China hivi karibuni imelaani vikali uchunguzi unaofanywa na Tume ya Umoja wa Ulaya kuhusu uchunguzi wa kampuni zinazotengeneza magari ya umeme, ambapo Umoja wa Ulaya unataka kiasi kikubwa cha taarifa zinazohusiana na siri za kibiashara za viwanda hivyo. Wizara hiyo imerejea ahadi yake ya kuchukua hatua zote zinazotakiwa kulinda haki na maslahi ya kampuni za China.



Watengenezaji wa magari nchini China wametaka hatua kali za kujibu kitendo hicho cha Tume ya Umoja wa Ulaya zichukuliwe, ikiwa ni pamoja na kuongeza kwa muda kiwango cha ushuru kwa magari yanayoagizwa kutoka nje yenye injini kubwa, huku viwanda husika vya ndani vikiomba ama kupanga kuomba uchunguzi ufanyike kwa baadhi ya bidhaa zinazoto9ka kwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, ikiwemo maziwa. Pia, maofisa wa China wameahidi kuchukua hatua zote zinazotakiwa kutetea haki na maslahi ya wafanyabiashara wa China.

Wakati huohuo, utafiti uliofanywa hivi karibuni umeonyesha kuwa, imani ya wafanyabiashara wa China kwa soko la Umoja wa Ulaya imepungua kwa kasi kufuatia uchunguzi wa Umoja huo dhidi ya magari ya umeme ya China na pia ushuru mkubwa unaotozwa kwa magari hayo. Hatua hiyo ya Umoja wa Ulaya imedhoofisa sana ushirikiano kati ya China na Umoja wa Ulaya, na itatoa pigo kubwa kwa uchumi wa Umoja wa Ulaya ambao unakabiliwa na changamoto nyingi.

Akijibu swali kuhusu mkutano wa ndani kati ya watengenezaji magari wakubwa wa China na Umoja wa Ulaya, ambapo kampuni husika zilisema Umoja huo unadai siri za ndani za kibiashara, Msemaji wa Wizara ya Biashara ya China He Yadong amesema, Tume ya Umoja wa Ulaya imetaka kupewa taarifa nyingi kuhusu uzalishani na operesheni, mipango ya maendeleo, mchakato wa kiufundi, mfumo wa bidhaa na taarifa nyingine kutoka kwa kampuni za China zinazotengeneza magari ya umeme na betri. Amesema aina, muundo na wingi wa taarifa zilizokusanywa na Tume hiyo hazikutarajiwa na haziendani na uchunguzi huo unaofanyika. Pia amelaani adhabu ya ushuru iliyotolewa na Tume hiyo kwa madai kwamba kampuni za China hazikutoa ushirikiano, hatua iliyowashangaza na kuwasikitisha wamiliki wa kampuni wa China.



Bw. He amesisitiza kuwa, hatua ya Tume ya Umoja wa Ulaya imekosa msingi wowote wa uhalali na kisheria, inakiuka kanuni za Shirika la Biashara Duniani (WTO), inavuruga ushindani wa usawa na kudhoofisha mageuzi ya kijani duniani na ushirikiao wa wazi.

Juni 18, kampuni kubwa za China na Ulaya zinazotengeneza magari zilifanya mkutano wa ndani, ambapo watengenezaji wa magari wa China na mashirikisho ya sekta hiyo yalipinga uamuzi wa Umoja wa Ulaya dhidi ya magari ya umeme ya China, na kuitaka serikali ya China kuchukua hatua za kujibu, ikiwa ni pamoja na kuongeza kiwango cha ushuru kwa magari yanayoagizwa yenye injini kubwa.

Cha ajabu ni kwamba, watengenezaji wa magari wa Ulaya waliohudhuria mkutano huo pia walipinga hatua ya Tume ya Umoja wa Ulaya ya kuongeza ushuru wa ziara kwa magari ya umeme yanayotengenezwa nchini China, na kueleza matarajio yao kwamba China na Umoja wa Ulaya zitaanza majadiliano haraka iwezekanavyo ili kuepuka mvutano zaidi wa kibiashara kati ya pande hizo mbili.

Kuhusu kama Wizara ya Biashara ya China itaanza kufanya uchunguzi kwa bidhaa za maziwa zinazotoka katika nchi za Ulaya, Bw. He amesema Wizara hiyo imepokea maombi yaliyotolewa na viwanda husika, ambavyo vina haki ya kuomba kufanyika kwa uchunguzi huo chini ya sheria za China na kanuni za WTO.

Wakati huohuo, utafiti uliochapishwa na Shirikisho la Wafanyabiashara wa China katika Umoja wa Ulaya (CCCEU) umeonyesha kuwa, asilimia 82 ya kampuni zilizofanyiwa uchunguzi zimesema uchunguzi huo wa Umoja wa Ulaya umesababisha kushuka kwa uaminifu kwa uwekezaji barani Ulaya, huku zaidi ya asilimia 70 zikisema kuwa uchunguzi wa Tume ya Umoja wa Ulaya umekuwa na athari hasi kwa mauzi barani Ulaya.
 
Kila mtu abaki na soko lake kwa sasa , ulaya wana hela ila wako wachache,,,, mchina level ya kati ila watu anao wengi, hata akipiga biashara ndani ya nchi yake ana soko kubwa.......ila hao wa ulaya kampuni zikikosa na masoko ya nje hali ngumu
 
  • Thanks
Reactions: DPN
Kila mtu abaki na soko lake kwa sasa , ulaya wana hela ila wako wachache,,,, mchina level ya kati ila watu anao wengi, hata akipiga biashara ndani ya nchi yake ana soko kubwa.......ila hao wa ulaya kampuni zikikosa na masoko ya nje hali ngumu
shida wachina hawanunui vitu luxuries wanapenda maisha local si ajab kumkut mchina anachoma hat mahind wanavaa vtu vya bei ndogo wapi economy sana wazungu wanapenda vitu vizur high quality vitu vya thaman mchina kama muha tu so hat hayo madude wanatengeneza ila wanalenga soko la nje si ndan mchina aknua sim leo au gar anatumia pk fund aseme alifai mzungu ikitok model mpya anachukua ya juu..hat mfano fenicha mzungu miaka mi2 crismas atabadil fenicha zote nyingine atauza sel atie vtu vpya mzungu mtu wa kwenda na wakat sana ndiomana ki soko mchina anategemea europe na africa
 
shida wachina hawanunui vitu luxuries wanapenda maisha local si ajab kumkut mchina anachoma hat mahind wanavaa vtu vya bei ndogo wapi economy sana wazungu wanapenda vitu vizur high quality vitu vya thaman mchina kama muha tu so hat hayo madude wanatengeneza ila wanalenga soko la nje si ndan mchina aknua sim leo au gar anatumia pk fund aseme alifai mzungu ikitok model mpya anachukua ya juu..hat mfano fenicha mzungu miaka mi2 crismas atabadil fenicha zote nyingine atauza sel atie vtu vpya mzungu mtu wa kwenda na wakat sana ndiomana ki soko mchina anategemea europe na africa
Mchina anao wote,,,matajiri mabilionea anao na masikini anao,, ingekua hivyo apple asingekua anakomalia soko la china maana bidhaa zake ni luxury ila sasa China ni moja kati ya soko lake kubwa na hata kwa sasa apple imeshuka tokana na wachina kuanza kuhamia huawei kwa sababu za kizalendo kabisa,,,,Mchina ana soko la ndani na la nje na ndo maana la nje anaweza kuli manipulate anavyotaka maana hata akikosea step soko la ndani bado litampa faida,,,,Ulaya na marekani walikua wanashangaa jamaa anawezaje kuuza gari za umeme za quality kubwa kabisa zinazolingana au hata kuzidi za kwao na bado akawa anauza kwa bei ndogo kuliko hizo za ulaya na faida anapiga, ndo maana wanataka wacheki wana siri gani maana kwao hio ishu ni ngumu na hawawezi kushindana nae
Screenshot_20240708-110033_Samsung Internet.jpg
 
  • Thanks
Reactions: DPN
Mchina anao wote,,,matajiri mabilionea anao na masikini anao,, ingekua hivyo apple asingekua anakomalia soko la china maana bidhaa zake ni luxury ila sasa China ni moja kati ya soko lake kubwa na hata kwa sasa apple imeshuka tokana na wachina kuanza kuhamia huawei kwa sababu za kizalendo kabisa,,,,Mchina ana soko la ndani na la nje na ndo maana la nje anaweza kuli manipulate anavyotaka maana hata akikosea step soko la ndani bado litampa faida,,,,Ulaya na marekani walikua wanashangaa jamaa anawezaje kuuza gari za umeme za quality kubwa kabisa zinazolingana au hata kuzidi za kwao na bado akawa anauza kwa bei ndogo kuliko hizo za ulaya na faida anapiga, ndo maana wanataka wacheki wana siri gani maana kwao hio ishu ni ngumu na hawawezi kushindana naeView attachment 3036459
we uelewa wako mdogo sana kua billionaire ni mbinu kuu ya ku make uwez kua na matumiz ya ovyo ovyo ukawa tajir labda mali za kurith ingia google msach steve job mtazame nguo mavaz anayovaa mtazame mwenye fb mark zurbeg mtazame jack maa ntazame jef bezos sana wanachojal makaz na security alaf mabilionair wanalipa kod ila awachangii sn mapato km watu wa hal ya chin bahresa anapofngua kiwanda aleng matajir anafnya biashara ndg ndg maji pip unga mafuta mchele icecrm anqleng watu wa lika la chin ndio wanunuaj hat hayo magar ya umeme izo sim na ulivotaj mirad ya matajir wanalenga sis wa daraj la chin...apple asembling in california then inafanywa china ajir china ni center of world kwenye kusafirisha dunia nzima china kuna cheap labour china ni rahis kupata material kutokan nathaman ya usd na yeni ya china china unapat eneo kubwa ukakod ukafanyia kaz kutokan na thaman ya saraf ni tafaut kupat eneo ilo marekan na posho utayolipa wachina si saw na posho utayolipa mmarekan ndoman wazungu weng wanafngua viwanda china nirahis kusafrisha asume unaagiza bidhaa tok marekan kwa dhl na unasafirisha bidhaa toka china kuptia gsm au tosh gharama ni sawa? skujib tena km unafikra utakua umeelew vzur
 
we uelewa wako mdogo sana kua billionaire ni mbinu kuu ya ku make uwez kua na matumiz ya ovyo ovyo ukawa tajir labda mali za kurith ingia google msach steve job mtazame nguo mavaz anayovaa mtazame mwenye fb mark zurbeg mtazame jack maa ntazame jef bezos sana wanachojal makaz na security alaf mabilionair wanalipa kod ila awachangii sn mapato km watu wa hal ya chin bahresa anapofngua kiwanda aleng matajir anafnya biashara ndg ndg maji pip unga mafuta mchele icecrm anqleng watu wa lika la chin ndio wanunuaj hat hayo magar ya umeme izo sim na ulivotaj mirad ya matajir wanalenga sis wa daraj la chin...apple asembling in california then inafanywa china ajir china ni center of world kwenye kusafirisha dunia nzima china kuna cheap labour china ni rahis kupata material kutokan nathaman ya usd na yeni ya china china unapat eneo kubwa ukakod ukafanyia kaz kutokan na thaman ya saraf ni tafaut kupat eneo ilo marekan na posho utayolipa wachina si saw na posho utayolipa mmarekan ndoman wazungu weng wanafngua viwanda china nirahis kusafrisha asume unaagiza bidhaa tok marekan kwa dhl na unasafirisha bidhaa toka china kuptia gsm au tosh gharama ni sawa? skujib tena km unafikra utakua umeelew vzur
Kwa hiyo ww ndo umeona umepost kitu cha maaana hapo .mbona mwenzako ameamdika vizuri tu kwa weledi.. na katoa mfano wa apple iliyona wanunuzi wengi kutoka china
 
  • Thanks
Reactions: DPN
Back
Top Bottom