China yazindua Cruise Ship ya kwanza, 'Adora Magic City.'

China yazindua Cruise Ship ya kwanza, 'Adora Magic City.'

Unajua China ana advantage kubwa sana ya soko lao la ndani kwa mfano wana kampuni nyingi za shipping kama COSCO, YANG MING na zinginezo ambazo hao lazima wanunue meli zinazotengenezwa nchini kwao

In term of orders worldwide Mchina kamzidi South Korea

Na kwa sasa makampuni mengi yanafanya kazi na China kwa sababu makampuni ya China yako more competitive in terms of productivity, production stability, labor and on-time vessel completion

Ndio maana Mchina amekuwa top mwa miaka 13

Usisahau na bei nafuuu [emoji41]
 
Hivi wale wabunifu wetu wa helcopter waliishia wapi? Kwanini wasiwe accelerated ili siku moja wafike huku? Hawa wachina si nao walianza kama wetu?
Wale sio wabunifu, wale ni kama kijana wa mtaani anayeweza piga danadana zaidi ya 200 alafu uje useme akasajiriwe timu ya ligi kuu.
Kama ungekuwa mtumiaji mzuri wa YouTube ungeona demonstrations za watoto wa vyuo na wahuni uko duniani wakitengeneza maroketi madogo kilo kama 50 linapaa makumi ya kilomita na wanapiga kila kitu kwa kompyuta na programu wanazo na calibrations wanafanya. Wakitoka hapo sio eti wanaamini wana uwezo wa kuunda roketi, wala media hazihangaiki nao.
Kuna bwana mmoja yeye anatengeneza mini -engines kwenye channel yake ya YouTube nimesahau jina.

Bongo mtu anachomelea mabati na kuweka mota used ya mashine ya kusaga alafu media na kamera zao wanakuja kusema eti "kaunda helikopta". Hata uweke trilioni moja kwenye mradi, hutoi helikopta pale.

Manufacturing ya vitu vikubwa sio jambo la mtu mmoja, inabidi iwe sera ya nchi na dira ijulikane tunafanya vitu vingapi ambavyo vikiungana ndio vinawezesha industry fulani ikue. Mfano Boeing ndege zao zina components zaidi ya milioni moja, yani ndege moja inahitaji ufanye utafiti, ukague ubora, utoe certificate, ufanye testing, ufanye upgrade, upime resistance sijui uwezo wa mwisho na mambo mengine mengi kwa kila component na hapo una vitu zaidi ya milioni moja vyote upitie process hiyo.

Kwa hali hiyo hakuna uwezekano ndege nzima ikaundwa na Boeing. Landing gear atakuwa labda General Electric, power supply labda awe BAE Systems, kompyuta na mifumo ya mawasiliano labda awe Raytheon na makampuni zaidi ya 100 yanahusika.

Sasa bongo mtu anakwambia anatengeneza gari la umeme ila akionyesha sehemu anakotengenezea ni kama sebule kubwa, sakafu ya nyumbani, vifaa vya kutengenezea gari hamna; sikuona moulding machines, sikuona lathes, sikuona vya kufanya cutting, kupaka rangi ile electropainting, hakuna sehemu ya drawings na design. Mafundi gereji wameshika spana alafu kuna raia kwa akili zao kabisa wanaamini pale kuna gari linatengenezwa. Nitaambiwa nina chuki na "mbona hata Toyota sio kila kitu wanatengeneza wao".
Kama kufanya assembling hapo sawa hata mafundi gereji wanaweza, si huwa wanafungua kila kitu kwenye gari na kukirudisha.

Sasa hivi vitu havifanyiki nchi haina steel industry, vyuo vinakaririsha vitini, shule zinafundisha uchavushaji wa maua na matobo ya panzi kupumulia, umeme ghali na hauaminiki, hakuna investing culture kila mtu anajenga nyumba za kupanga hapo anaona amewekeza, rushwa, hakuna juhudi binafsi za kulinda viwanda vya ndani.
Manufacturing ni ngumu sana usione matajiri wa bongo wanaenda kununua vitenge China waje kuuza wawe mabilionea wakati viwanda vya nguo kibao nchini vimekufa na pamba sio zao tena la kibiashara.
 
Shanghai, China
06/06/2023


Kampuni kubwa ya utengenezaji meli inayoitwa China State Shipbuilding Corporation (CSSC) yenye makao yake Shanghai walizindua meli ya kwanza ya kitalii (Cruise ship) kutengenezwa China, iliyopewa jina la Adora Magic City.

Itakuwa cruise ship ya kwanza duniani kuwa na internet ya 5G

Meli hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 5246 na vyumba vya kulala 2826 itakuwa na
•Restaurants
•Theaters
•Shopping centres
•Water parks (swimming pools)
•Outdoor Cinema
•Casinos
•Gaming lounge
•Luxury-brand boutiques
•Photo Gallery & Shop
•Bar
•Modern gym
•Spa
•Beauty saloon
•Stage for live perfomance
•Multi-Sports Course (for playing volleyball/basketball/tennis
•Themed entertainment for kids in 3 age groups
(i)Age 2-5 yo, 6-8 yo, and 9-11 yo
(ii)Children Club Lounge is for older kids (12-14 yo/video games, movies, parties, planned activities),
(iii)Teen Club for teenagers (15-17 yo/movies, interactive video gaming, karaoke, themed parties, booking teen-only cruise shore excursion).


Mwonekano wa nje;

View attachment 2654911

View attachment 2654912



Baadhi ya picha za mwonekano wa ndani

Hotel
View attachment 2654913


Restaurant
View attachment 2654914

Theatre
View attachment 2654915

Mall
View attachment 2654917

Water park
View attachment 2654952

Sasa ni wakati wa China kuingia katika ushindani na makampuni ya Ulaya na America katika utengenezaji wa cruise ships.

UTENGENEZAJI WA MELI CHINA
Mbali ya meli za abiria pia meli zinazotengenezwa kwa wingi nchini China ni meli za mizigo kama liquefied natural gas (LNG) tankers, oil tankers na container ships.

Baadhi ya rekodi zilizowekwa na China katika utengenezaji wa meli;

●Kwa miaka 13 mfululizo China inashikilia rekodi ya kuongoza uuzaji wa meli duniani.

●China State Shipbuilding Corporation (CSSC) ilisaini mkataba na kampuni ya Ufaransa ya CMA CGM kuitengenezea meli za kubeba kontena kubwa 16 zenye thamani ya 4 billion U.S. dollars. Imekuwa kampuni ya kwanza duniani kupewa oda kubwa kwa wakati mmoja

●Meli kubwa duniani ya kubeba container yenye ukubwa wa viwanja 4 vya mpira wa miguu, iliuzwa kwa kampuni ya Mediterranean Shipping Company (MSC) SA. Ilitengenezwa na kampuni ya Hudong-Zhonghua Shipbuilding Co Ltd, yenye makao yake Shanghai. Imepewa jina la MSC TESSA

View attachment 2654947


●China pekee inachangia 47.3% ya meli za mizigo zinazotengenezwa duniani

●Kampuni za China zinaongoza kwa kuwa na zaidi ya nusu ya oda za meli zote ulimwenguni

According to Voice Of America (VoA): China has 19 modern shipbuilding yards pumping out commercial and naval ships. One of China's shipyards is so large that its capacity surpasses that of all U.S. shipbuilders combined.
afu mtu jinga moja utaliskia wanaijeria wachawi!!!uchawi ndo huu sasa
 
Unajua China ana advantage kubwa sana ya soko lao la ndani kwa mfano wana kampuni nyingi za shipping kama COSCO, YANG MING na zinginezo ambazo hao lazima wanunue meli zinazotengenezwa nchini kwao

In term of orders worldwide Mchina kamzidi South Korea

Na kwa sasa makampuni mengi yanafanya kazi na China kwa sababu makampuni ya China yako more competitive in terms of productivity, production stability, labor and on-time vessel completion

Ndio maana Mchina amekuwa top mwa miaka 13
China akishakuwa na soko la ndani inamtengenezea production capacity kubwa ambayo inatosheleza soko la nje ukizingatia orders zinavyokuwa. Mwaka juzi hivi Serbia walinunua air defense system kutoka kwao nadhani ni HQ-9 kama sisahau, zililetwa mwaka jana wakati ukinunua systems za Marekani au Ulaya inabidi ukae zaidi ya miaka miwili ndio upokee, ukitaka haraka zaidi unalipa hela nyingi zaidi.
Mwaka jana tena Pakistan ikapata delivery yake ya pili ya J-10C fighter jets, wakati wameziagiza ndani ya miaka miwili vilevile. Nigeria ilivyoagiza JF-17 hazikukawia.

Yani ukiwa vitani na una compatibility na silaha za Mchina ambazo zipo in service utapata silaha kwa nguvu kidogo kuliko manufacturers wa nchi nyingine. Kutimiza mahitaji ya wateja wa nchi ya watu bilioni 1.3 itakufanya uone kama ni kucheza ukitengeneza bidhaa za nchi ya watu sijui milioni 60.
 
China akishakuwa na soko la ndani inamtengenezea production capacity kubwa ambayo inatosheleza soko la nje ukizingatia orders zinavyokuwa. Mwaka juzi hivi Serbia walinunua air defense system kutoka kwao nadhani ni HQ-9 kama sisahau, zililetwa mwaka jana wakati ukinunua systems za Marekani au Ulaya inabidi ukae zaidi ya miaka miwili ndio upokee, ukitaka haraka zaidi unalipa hela nyingi zaidi.
Mwaka jana tena Pakistan ikapata delivery yake ya pili ya J-10C fighter jets, wakati wameziagiza ndani ya miaka miwili vilevile. Nigeria ilivyoagiza JF-17 hazikukawia.

Yani ukiwa vitani na una compatibility na silaha za Mchina ambazo zipo in service utapata silaha kwa nguvu kidogo kuliko manufacturers wa nchi nyingine. Kutimiza mahitaji ya wateja wa nchi ya watu bilioni 1.3 itakufanya uone kama ni kucheza ukitengeneza bidhaa za nchi ya watu sijui milioni 60.
Well said
 
Sasa bongo mtu anakwambia anatengeneza gari la umeme ila akionyesha sehemu anakotengenezea ni kama sebule kubwa, sakafu ya nyumbani, vifaa vya kutengenezea gari hamna; sikuona moulding machines, sikuona lathes, sikuona vya kufanya cutting, kupaka rangi ile electropainting, hakuna sehemu ya drawings na design. Mafundi gereji wameshika spana alafu kuna raia kwa akili zao kabisa wanaamini pale kuna gari linatengenezwa. Nitaambiwa nina chuki na "mbona hata Toyota sio kila kitu wanatengeneza wao".
Kama kufanya assembling hapo sawa hata mafundi gereji wanaweza, si huwa wanafungua kila kitu kwenye gari na kukirudisha.
🤣😄
 
Wale sio wabunifu, wale ni kama kijana wa mtaani anayeweza piga danadana zaidi ya 200 alafu uje useme akasajiriwe timu ya ligi kuu.
Kama ungekuwa mtumiaji mzuri wa YouTube ungeona demonstrations za watoto wa vyuo na wahuni uko duniani wakitengeneza maroketi madogo kilo kama 50 linapaa makumi ya kilomita na wanapiga kila kitu kwa kompyuta na programu wanazo na calibrations wanafanya. Wakitoka hapo sio eti wanaamini wana uwezo wa kuunda roketi, wala media hazihangaiki nao.
Kuna bwana mmoja yeye anatengeneza mini -engines kwenye channel yake ya YouTube nimesahau jina.

Bongo mtu anachomelea mabati na kuweka mota used ya mashine ya kusaga alafu media na kamera zao wanakuja kusema eti "kaunda helikopta". Hata uweke trilioni moja kwenye mradi, hutoi helikopta pale.

Manufacturing ya vitu vikubwa sio jambo la mtu mmoja, inabidi iwe sera ya nchi na dira ijulikane tunafanya vitu vingapi ambavyo vikiungana ndio vinawezesha industry fulani ikue. Mfano Boeing ndege zao zina components zaidi ya milioni moja, yani ndege moja inahitaji ufanye utafiti, ukague ubora, utoe certificate, ufanye testing, ufanye upgrade, upime resistance sijui uwezo wa mwisho na mambo mengine mengi kwa kila component na hapo una vitu zaidi ya milioni moja vyote upitie process hiyo.

Kwa hali hiyo hakuna uwezekano ndege nzima ikaundwa na Boeing. Landing gear atakuwa labda General Electric, power supply labda awe BAE Systems, kompyuta na mifumo ya mawasiliano labda awe Raytheon na makampuni zaidi ya 100 yanahusika.

Sasa bongo mtu anakwambia anatengeneza gari la umeme ila akionyesha sehemu anakotengenezea ni kama sebule kubwa, sakafu ya nyumbani, vifaa vya kutengenezea gari hamna; sikuona moulding machines, sikuona lathes, sikuona vya kufanya cutting, kupaka rangi ile electropainting, hakuna sehemu ya drawings na design. Mafundi gereji wameshika spana alafu kuna raia kwa akili zao kabisa wanaamini pale kuna gari linatengenezwa. Nitaambiwa nina chuki na "mbona hata Toyota sio kila kitu wanatengeneza wao".
Kama kufanya assembling hapo sawa hata mafundi gereji wanaweza, si huwa wanafungua kila kitu kwenye gari na kukirudisha.

Sasa hivi vitu havifanyiki nchi haina steel industry, vyuo vinakaririsha vitini, shule zinafundisha uchavushaji wa maua na matobo ya panzi kupumulia, umeme ghali na hauaminiki, hakuna investing culture kila mtu anajenga nyumba za kupanga hapo anaona amewekeza, rushwa, hakuna juhudi binafsi za kulinda viwanda vya ndani.
Manufacturing ni ngumu sana usione matajiri wa bongo wanaenda kununua vitenge China waje kuuza wawe mabilionea wakati viwanda vya nguo kibao nchini vimekufa na pamba sio zao tena la kibiashara.
Duuuu....hiii kichwaa hatari..ckupangaa kucoment.semaa inaonekana uko bright..Africa tuna safari ndefu aiseee
 
Mkuu umechambua vyema, je tukianza utengenezaji hasa vyombo vya uchukuzi kama ndege, tunaweza vipi shindana na kampuni za kigeni hasa soko na tender, hivi Kenya watakubali kununua ndege made in Tz? au hata abiria tu wananchi wa hapa hapa watakubali kupanda ndege ametengeneza mTz mwenzie?
Hatutakiwi kuwaza kwenye kutengeneza ndege kabisa kabisa, hizo ni ndoto za mchana. Boeing ambao ndio giant duniani wanatumia zaidi ya trilioni 6 za Kitanzania kufanya research na development, hapo wana products ambazo tiyari zinakubalika, wana plants tiyari, wana wataalamu na uzoefu, wana contracts na suppliers. Yani wanaweza kaa miaka minne bila kuleta modernization yoyote ya ndege na wakaendelea kuwa sokoni ila bado wanatumia zaidi ya trilioni 6 kwenye utafiti, sembuse sisi tukitaka kuanza na moja tuwekeze kiasi gani.

Sisi tuwaze kutengeneza zana za kilimo, viwepo viwanda vya matrekta, mabomba ya kumwagilia, combine harvesters, cold rooms za kuhifadhi matunda kama parachichi za kule Njombe, silos za kisasa na vitu kama hivyo.
Tukitoka stage hiyo twende kwenye kutengeneza nguo. Kisha viwanda vya kuchakata bidhaa nyingine za kilimo habari za kubeba magunia ya korosho kwenda nje tuache, tubebe maboksi ya korosho zilizokuwa roasted.

Hapo hapo tunaweza elekea kwenye kuunda magari kwenye assembly lines tukichukua licence kutoka kwa manufacturers. Unakuwa mwisho wa kununua daladala nje. Hapo sasa tunaongeza miundombinu ya reli na bandari inaongezwa nyingine hasa Mtwara, tunaelekeza nguvu kwenye nishati inakuwa cheap na uhakika. Hapo ndipo tunaita wawekezaji wakubwa wa kujenga kiwanda cha hata bilioni 500.

Hapo nimefanya kwa ufupi, kuna mlolongo mrefu sana unatakiwa mfano kwenye elimu, sheria, kupambana na rushwa, uhuru wa kibiashara na mengine. Ila kwa akili za kibongo hizi za kujadili mpira asubuhi saa moja inatakiwa roho ngumu ishushwe kutoka mbinguni kujaribu kufanya haya.
 
Back
Top Bottom