CHINESE CUISINE: Nini ule ukienda kwenye mgahawa wa kichina...

CHINESE CUISINE: Nini ule ukienda kwenye mgahawa wa kichina...

Jamani nyoka aliyeokwa sijamuona hapo sijui hii menu inaitwaje nataka nijaribu
 
干煎黄鱼 (Gan Jian Huang Yu) - Pan Fried Yellow Fish

Ni samaki aliyekaangwa na wakati mwingine huwekwa viungo vyenye kumfanya awe na ladha nzuri mdomoni.


3254577175_05b7ca0163_o.jpg

Huyu samaki hata kwa sura anavutia,tatizo ni huo wali usio na ladha sijui utapita kooni!!
Ahsante best,endeleaaa
 
Jamani nyoka aliyeokwa sijamuona hapo sijui hii menu inaitwaje nataka nijaribu

Mkuu dhumuni langu kubwa sio kuweka kila aina ya chakula cha kichina bali ni vyakula vile tu ambavyo 'raw material' yake hata kwetu zipo lakini utofauti ni upishi tu.

Wapo Watanzania wengi wanaopenda kujaribu kula vyakula vya Kichina lakini hawana mwanga ni vyakula gani waagize kwenye migahawa.

Wapo pia Watanzania wanaokwenda kibiashara huko China lakini pia wakifika huko huishia kula mikate na wali mkavu wakiwa na wasiwasi wa kulishwa mbwa na misosi mingine isiyo jadi yetu.

Kwa mantiki hiyo ndio maana hujaona vyakula kama nyoka, ng'e, viwazi, konokono & co...lakini kwa kuwa umependa kujua Nyoka aliyeokwa huitwaje basi jina la chakula hicho huitwa 烤蛇 (kao she) bahati mbaya namna ya kutamka 'she' siwezi ambatanisha sauti hapa ila haitamkwi kama ilivyoandikwa.
 
...tatizo ni huo wali usio na ladha sijui utapita kooni!!

Ni kweli kwa mtu yoyote aliyezoea kula wali upikwao na Mtanzania basi mtu huyo kwa mara ya kwanza atapata tabu sana kula Wali wa Kichina 'Steamed Rice' ambao haujamwagiwa mboga.
 
Kusema kweli wachina MashAllah.

Apa kwetu zenji kuna Restaurant yao inaitwa Pagoda. Ama nkiwa na uchenji wa maana sijinyimi. Bata wao watam ajabu, na prawns na kaa. Na soup zao.

Ila iyo iwe kwa hapa tz yetu. Ukienda kwao ni kheri uagize mboga mboga mana mara unalishwa chura au nyoka au mbwa. Lols
 
酱汁排骨 (Jiang Zhi Pai Gu) - Braised Ribs with Sauce

Chakula hiki huwa ni mbavu za kitimoto ambazo zimemwagiwa sauce mahususi kwa ajili ya kitimoto ambayo huwekwa kidogo tu.

Wakati mwingine chakula hiki huwekwa na vipande vya vitunguu maji vilivyokaangwa na soya sauce au sour vinegarsauce.


yuan_6725058c75ac798bca91d2b39c2042ed.jpg
 
Kusema kweli wachina MashAllah.

Apa kwetu zenji kuna Restaurant yao inaitwa Pagoda. Ama nkiwa na uchenji wa maana sijinyimi. Bata wao watam ajabu, na prawns na kaa. Na soup zao.

Hahaha aisee umenikumbusha maana hapo Pagoda (Stone Town) karibu Dhow Hotel nimeshakula sana chakula cha kichina...mara nyingi nikienda Zenji hula hapo na wakati mwingine hupiga stori za hapa na pale ni yule mzee wa kichina mmiliki wa hiyo hoteli

Ila iyo iwe kwa hapa tz yetu. Ukienda kwao ni kheri uagize mboga mboga mana mara unalishwa chura au nyoka au mbwa. Lols

Huwezi kulishwa chura, nyoka au mbwa kwa kuwa vyakula hivyo ni gharama...

Wakati pekee ambao unaweza kulishwa hivyo vyakula ni kama umeenda mgahawani na marafiki wa Kichina halafu wasikueleze kilichopo mezani.
 
小白菜 (Xiao Bai Cai) - Chinese cabbage

Hii ni mboga ya majani ambayo hupatikana Mashariki ya Mbali na ni moja ya mboga za majani maarufu huko.

Mapishi yake kwa kawaida hutumia mvuke au huchemshwa pasipo kutokosa na huwekwa vitunguu saumu na chumvi tu.


2397_650x450_63d276393c.jpg
 
小白菜 (Xiao Bai Cai) - Chinese cabbage

Hii ni mboga ya majani ambayo hupatikana Mashariki ya Mbali na ni moja ya mboga za majani maarufu huko.

Mapishi yake kwa kawaida hutumia mvuke au huchemshwa pasipo kutokosa na huwekwa vitunguu saumu na chumvi tu.


2397_650x450_63d276393c.jpg

Ahsante swahiba kwa uzi huu,mi napenda cuisines za mataifa tofauti kama hawa wachina,wathailand,waitaliano,wahindi na nigerians.....sasa je hii cabbage inapatikana kwenye supermarket zetu upande wa groceries?vingine vinapikika nyumbani...
 
回锅肉 (huíguōròu) - Twice Cooked Pork

Hii ni nyama ya kitimoto hivyo kwa wale ndugu zangu msiotumia hii bidhaa inabidi kutoagiza hii.

Ni chakula chenye asili ya Jimbo la Sichuan na kawaida huwa haina vikorombwezo vingi zaidi huwa na majani ya kabichi ambayo huwekwa sour vinegar ili kuleta ladha ya uchachu na wakati mwingine huambatana na pilipili hoho na pilipili za kawaida.


201203151331794297.jpg
Hapa naona gari la KORIE liliangukia kwa bahati mbaya,ukipiga mfululizo unakaribisha Cholesterol,BP,SHELL na Caltex lol
 
ahsante best jamani kuna siku nlipewa offer huko uchinani nikaona sehemu imeandikwa steak nikaagiza ikaja ni nyeusiii afu ina rojorojo nzito ladha hakuna afu ile rohjorojo naieleweki ile kuweka mdomoni tu nikataka kutapika ikabidi niende toi ila wenyeji wangu wakaelewa ikabidi niagize mishkaki.Vyakula vya kichina vizuri ila ukiingia chaka lazima utapike minnapenda makorokoro yao wanayoungia tu mweee huwa yanatamamisha wikiendi hii na mie nimepanga kupika nyama ya ngombe na kujaribu kuweka na wine nione test yake best eti wine gani nidondoshee au hata hata spirit konyagi itanoga?
 
Mkuu mimi nina visa na chakula chenye mafuta mengi...kwa orodha uliyotoa naona havinifai...Je. kuna menu nyingine yenye vyakula visivyo na mafuta mengi ?
 
Hapa naona gari la KORIE liliangukia kwa bahati mbaya,ukipiga mfululizo unakaribisha Cholesterol,BP,SHELL na Caltex lol

Mafuta ya hawa jamaa ni salama kwa afya otherwise kwa wingi wa Wachina duniani basi huenda lingekuwa ni taifa la watu wanene kuliko wote duniani.

Most of fried chinese cuisine huwa zinatiririsha mafuta kama hivyo when served.
 
Mkuu mimi nina visa na chakula chenye mafuta mengi...kwa orodha uliyotoa naona havinifai...

Jaribu kuisoma post yangu hapo juu nilipomjibu Ennie.

Je. kuna menu nyingine yenye vyakula visivyo na mafuta mengi ?

Zipo nyingi tu mkuu ila nyingi zake nahisi Wabongo wengi si ajabu kuwashinda kula.

Kuna soup, tambi za kichina, vegs n.k
 
Mafuta ya hawa jamaa ni salama kwa afya otherwise kwa wingi wa Wachina duniani basi huenda lingekuwa ni taifa la watu wanene kuliko wote duniani.

Most of fried chinese cuisine huwa zinatiririsha mafuta kama hivyo when served.
Endelea kutoa darasa best labda uoga wa kukaribia misosi yao utatutoka wengine
 
Mkuu mimi nina visa na chakula chenye mafuta mengi...kwa orodha uliyotoa naona havinifai...Je. kuna menu nyingine yenye vyakula visivyo na mafuta mengi ?

清蒸鱼 (Qing zheng yu)
Huyu ni samaki ambaye yuko steamed na viungo, mtamu balaa. Hakuna mimafuta wala nini na aina ya samaki inayotumika zaidi hapa ni samaki asiye na miba midogo midogo, yaani hapo ni wewe na chop stick yako ukimaliza upandemmoja unageuza upande wa pili unaendelea
6597184115866988996.jpg
 

Attachments

  • 6597184115866988996.jpg
    6597184115866988996.jpg
    18.5 KB · Views: 144
Mafuta ya hawa jamaa ni salama kwa afya otherwise kwa wingi wa Wachina duniani basi huenda lingekuwa ni taifa la watu wanene kuliko wote duniani.

Most of fried chinese cuisine huwa zinatiririsha mafuta kama hivyo when served.

Kweli mkuu, vyakula mara nyingi huwekwa mafuta kwenye hatua za mwisho za upishi mafuta yanatiririka tofauti na deep frying, halafu kula na chop stick kunasaidia sana pia yaani chakula kinaweza kuwa kimepikwa na mafuta mengi lakini chop stick ina pick mboga tu mchuzi wa mafuta unabaki kwenye sahani. Na mboga kwa kawaida huwa marinated kabla ya kupika kwa hiyo utamu wa mapishi maranyingi upo kwenye mboga sio mchuzi. Pia wali wana kula separately kwa kawaida kibakuli cha wali kinaletwa mwisho kabisa baada ya kukomba mboga zote. Sasa ukimwagia "mchuzi" kwenye wali kama huku kwetu halafu ukala kila kitu na kijiko, utajikuta unabwia mimafuta ambayo hukutakiwa ule. Asante mkubwa kwa menu: 'gong bao ji ding' na 'tang cu pai gu' are my favorites!
 
清蒸鱼 (Qing zheng yu)
Huyu ni samaki ambaye yuko steamed na viungo, mtamu balaa. Hakuna mimafuta wala nini na aina ya samaki inayotumika zaidi hapa ni samaki asiye na miba midogo midogo, yaani hapo ni wewe na chop stick yako ukimaliza upandemmoja unageuza upande wa pili unaendelea
6597184115866988996.jpg

huyu samaki anaitwa chewa ... yes ni mtamu sana
 
Back
Top Bottom