FikraPevu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2010
- 304
- 236
‘Chloroform’ ni dawa isiyo na rangi na yenye harufu nzuri yenye jina la ‘IUPAC’ lijulikanalo kitaalamu kama ‘Trichloromethane’ na ina fomula ya CHCl3. Chloroform inaweza kukufanya usinzie hata kama itatumiwa kwa dozi ndogo.
Chloroform ni kimiminika chepesi na chenye harufu nzuri ambacho kimekuwa kikitumika kwa miaka mingi kama dawa za ya usingizi wakati wa upasuaji (surgery). Kutokana na kuwa na nguvu hiyo kimepewa sifa ya kufanya mtu alegee au kuzimia kabisa hata pale kinapotumika kwa kiwango kidogo.
Chloroform kama dawa ya usingizi
Chloroform ilitumiwa kwa mara ya kwanza kama dawa ya usingizi mwaka 1847 na mtaalamu wa masuala ya uzazi aitwaye James Young Simpson; yeye aliitumia kwa watu wawili kama njia ya burudani.
Siku chache baadaye, ilitumiwa kwenye ufanisi wa afya ya meno huko Edinburgh na haikuonesha madhara yoyote. Baadaye umaarufu wake kama dawa ya usingizi ulikua kwa kiwango kikubwa na kuvuka mipaka, kiasi kwamba iliweza kutumiwa kwenye uzalishaji wa watoto wawili wa mwisho wa Malkia Victoria katika miaka ya 1850.
Lakini baadaye umaarufu wake ulianza kupungua baada ya kupatikana kwa dawa zingine nzuri zaidi na zenye madhara kidogo zaidi ya Chloroform.
Choloform inavyofanya kazi
Chloroform huathiri mfumo mzima wa fahamu na kuathiri ini pamoja na figo na kwa kiwango kikubwa huweza kuathiri mfumo wa hewa na kusababisha mtu kulala muda mrefu hata miaka (coma). Utumiaji kidogo wa dawa hii hufanya mtu kulegea au kuzimia kabisa na ikitumika kwa kiwango kikubwa huweza kusababisha kifo kwa yule aliyepewa.
Madhara ya Chloroform kwa binadamu
Madhara ya Chloroform kwenye mwili wa mwanadamu hutegemea kipimo cha dozi na njia iliyotumika kuisambaza.
Kwa mujibu wa Idara ya Huduma za Afya ya taasisi ya Wisconsin wanasema, “Mara tu au muda mfupi baada ya mtu kuvuta kiwango cha 100 ppm (100,000 ppbv) ya Chloroform katika hewa, mtu huyo huanza kuhisi uchovu, kizunguzungu na kuumwa kichwa.”
Hata hivyo watu wengi tunachanganya Chloroform na kimiminika kinachowekwa kwenye kitambaa kinachotumika kuwazimisha watu kwenye filamu, lakini madhara ya Chloroform ni makubwa zaidi na yasipodhibitiwa haraka huweza kusababisha kifo.
Madhara ya Choloroform kwa binadamu huongezeka sambamba na kiwango cha dozi yake. Wakati kiwango kidogo kinasababisha kutojielewa, kadiri dozi inavyoongezeka huweza kukufanya uzimie kabisa au usisikie mguso wowote. Kwa kiwango kikubwa zaidi huweza kusababisha upumuaji wa shida, misuli ya mwili kutulia kabisa, misuli ya kifua kupooza na mwishowe kupelekea kifo.
Inachukua muda gani kwa Chloroform kukuzimisha?
Wakati Chloroform iliyowekwa kwenye kitambaa huweza kukuzimisha kabisa, lakini huchukua muda mrefu zaidi ya vile inavyoonekana kwenye filamu nyingi (Huwezi kuzimia ghafla tu baada ya kuinusa). Inaweza kuchukua angalau dakika 5 mpaka mtu kuzima kabisa.
Chloroform ni kimiminika chepesi na chenye harufu nzuri ambacho kimekuwa kikitumika kwa miaka mingi kama dawa za ya usingizi wakati wa upasuaji (surgery). Kutokana na kuwa na nguvu hiyo kimepewa sifa ya kufanya mtu alegee au kuzimia kabisa hata pale kinapotumika kwa kiwango kidogo.
Chloroform kama dawa ya usingizi
Chloroform ilitumiwa kwa mara ya kwanza kama dawa ya usingizi mwaka 1847 na mtaalamu wa masuala ya uzazi aitwaye James Young Simpson; yeye aliitumia kwa watu wawili kama njia ya burudani.
Siku chache baadaye, ilitumiwa kwenye ufanisi wa afya ya meno huko Edinburgh na haikuonesha madhara yoyote. Baadaye umaarufu wake kama dawa ya usingizi ulikua kwa kiwango kikubwa na kuvuka mipaka, kiasi kwamba iliweza kutumiwa kwenye uzalishaji wa watoto wawili wa mwisho wa Malkia Victoria katika miaka ya 1850.
Lakini baadaye umaarufu wake ulianza kupungua baada ya kupatikana kwa dawa zingine nzuri zaidi na zenye madhara kidogo zaidi ya Chloroform.
Choloform inavyofanya kazi
Chloroform huathiri mfumo mzima wa fahamu na kuathiri ini pamoja na figo na kwa kiwango kikubwa huweza kuathiri mfumo wa hewa na kusababisha mtu kulala muda mrefu hata miaka (coma). Utumiaji kidogo wa dawa hii hufanya mtu kulegea au kuzimia kabisa na ikitumika kwa kiwango kikubwa huweza kusababisha kifo kwa yule aliyepewa.
Madhara ya Chloroform kwa binadamu
Madhara ya Chloroform kwenye mwili wa mwanadamu hutegemea kipimo cha dozi na njia iliyotumika kuisambaza.
Kwa mujibu wa Idara ya Huduma za Afya ya taasisi ya Wisconsin wanasema, “Mara tu au muda mfupi baada ya mtu kuvuta kiwango cha 100 ppm (100,000 ppbv) ya Chloroform katika hewa, mtu huyo huanza kuhisi uchovu, kizunguzungu na kuumwa kichwa.”
Hata hivyo watu wengi tunachanganya Chloroform na kimiminika kinachowekwa kwenye kitambaa kinachotumika kuwazimisha watu kwenye filamu, lakini madhara ya Chloroform ni makubwa zaidi na yasipodhibitiwa haraka huweza kusababisha kifo.
Madhara ya Choloroform kwa binadamu huongezeka sambamba na kiwango cha dozi yake. Wakati kiwango kidogo kinasababisha kutojielewa, kadiri dozi inavyoongezeka huweza kukufanya uzimie kabisa au usisikie mguso wowote. Kwa kiwango kikubwa zaidi huweza kusababisha upumuaji wa shida, misuli ya mwili kutulia kabisa, misuli ya kifua kupooza na mwishowe kupelekea kifo.
Inachukua muda gani kwa Chloroform kukuzimisha?
Wakati Chloroform iliyowekwa kwenye kitambaa huweza kukuzimisha kabisa, lakini huchukua muda mrefu zaidi ya vile inavyoonekana kwenye filamu nyingi (Huwezi kuzimia ghafla tu baada ya kuinusa). Inaweza kuchukua angalau dakika 5 mpaka mtu kuzima kabisa.