Chonde chonde wana Mbeya msikubali kutumika, msishiriki hayo maandamano haramu

Chonde chonde wana Mbeya msikubali kutumika, msishiriki hayo maandamano haramu

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Ndugu zangu wana Mbeya, mimi ni miongoni mwa wapingaji wakuu wa mkataba wa uwekezaji bandarini, hususani ile IGA. Huo mwingine bado hatujui kama ni mzuri au tumepigwa.

Lakini, kuna njia sahihi na njia isiyo sahihi ya kupinga jambo. Njia sahihi ni kama ile aliyoitumia Lissu kwa kuelezea mapungufu ya mkataba ule kwenye mikutano halali ya hadhara.

Njia nyingine sahihi ni ile waliyotumia Mwabukusi na Mpaula ya kwenda mahakamani. Na wengine pia kama TLS , wadau wa hapa JF, wabunge kule bungeni, TEC pamoja na wananzuoni wengine kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Kwakuwa serikali imeamua kupuuzia ‘concern’ za hao wote, basi njia pekee sahihi iliyosalia ni sanduku la kura katika uchaguzi ulio huru na wa haki. Kwamba, nguvu ielekezwe kwenye kidai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya kwa njia halali na kisha sote tutayatoa maoni yetu kupitia sanduku la kura.

Kuna kipindi mkoa wa Mbeya ni kama ulisuswa na serikali kutokana na tabia za watu wake kupenda ‘ligi’ kwenye kila jambo. Wakati wa JPM na hata sasa walau mambo yameanza kwenda vizuri.

Kwahiyo naomba niwasihi ndugu zangu, msitumike kifanya uhalifu wa maandamano yasiyo na kibali ili tu kupaisha ndoto za kisiasa za Mwabukusi na Mpaula.

Bandari sio mali ya Mbeyapeke yake bali Tanzania yote. Kama wenzenu hawaandamani nanyi hamna haja ya kufanya hivyo. Msijifanye mna uchungu saaana hadi mkaanza kuvunja sheria na kujiharibia bure.

Naamini hakuna atakaye andamana, lakini ni muhimu kukumbushana wajibu wetu kama wananchi wapenda maendeleo na amani.
 
Ndugu zangu wana Mbeya, mimi ni miongoni mwa wapingaji wakuu wa mkataba wa uwekezaji bandarini, hususani ile IGA. Huo mwingine bado hatujui kama ni mzuri au tumepigwa.
a, lakini ni muhimu kukumbushana wajibu wetu kama wananchi wapenda maendeleo na amani.
We mwanaume wa Dar tulia tukuonyeshe kwamba Sisi siyo sawa na nyie. Kesho mtatuelewa!
 
We mwanaume wa Dar tulia tukuonyeshe kwamba Sisi siyo sawa na nyie.Kesho mtatuelewa!
Mimi mwanaume wa Mbeya, nafahamu vema hasara ya maandamano yasiyo halali. Wengi mnaochochea hui ujinga hampo Mbeya.

Narudia tena, wana Mbeya msiwasikilize wahalifu hawa. Mheshimiwa Rais SSH amewaheahimu sana Mbeya na kuwapendelea. Ukibebwa bebeka. Waachieni Mpaula na Mwabukusi maandamano yao.
 
Maandamano sio haramu. Yako kwa mujibu wa katiba.
IGA ni haramu na batili.
Katiba mpya ni takwa la msingi.
Wana Loliondo, na Ngorongoro wana haki ya kuishi maeneo yao asilia.

Tume huru ya uchaguzi ni takwa letu wananchi
 
Mimi mwanaume wa Mbeya, nafahamu vema hasara ya maandamano yasiyo halali. Wengi mnaochochea hui ujinga hampo Mbeya.

Narudia tena, wana Mbeya msiwasikilize wahalifu hawa. Mheshimiwa Rais SSH amewaheahimu sana Mbeya na kuwapendelea. Ukibebwa bebeka. Waachieni Mpaula na Mwabukusi maandamano yao.
Kawabeba kivip nna mashak na uwezo wako wa kufikiria, ndo maana tunasema elimu ya Tanzania Ni mbov kwasabu ya watu kama wee
 
Maandamano sio haramu. Yako kwa mujibu wa katiba.
IGA ni haramu na batili.
Katiba mpya ni takwa la msingi.
Wana Loliondo, na Ngorongoro wana haki ya kuishi maeneo yao asilia.

Tume huru ya uchaguzi ni takwa letu wananchi
Kwa mujibu wa sheria zetu maandamano halali yanahitaji kibali. Hayo ya Mpaula na Mwabukusi hayana. Hivyo ni haramu.

Nakuunga mkono, tume huru ni takwa letu wananchi, na ndio itakayotupa njia sahihi ya kuiwajibisha serikali pale inapofanya yasiyotakiwa.
 
Bado sijapata jibu sahihi, kwa nini CCM inaogopa maandamano namna hii?

mtu anaandamana mwenyewe, njaa yake, jua lake, mvua yake na hata silaha yoyote mkononi mwake hana- sasa wewe kitakupunguzia nini ukimwacha aandamanee kisha asepe zake ?
 
Kwa mujibu wa sheria zetu maandamano halali yanahitaji kibali. Hayo ya Mpaula na Mwabukusi hayana. Hivyo ni haramu.

Nakuunga mkono, tume huru ni takwa letu wananchi, na ndio itakayotupa njia sahihi ya kuiwajibisha serikali pale inapofanya yasiyotakiwa.
Wacha sisi wana Ilemi, Simike, Nzovwe, Iwambi, Ituha, Jacaranda, Nonde, Nzovwe, Ikuto, Iyela, Ilolo nk tuingie road, nyie wa Dar endeleeni na mishe zenu za KFC, Mlimani City, Slipway, Bongoyo, nk kuleni bata. Wana Mbeya tutaliheshimisha taifa
 
Bado sijapata jibu sahihi, kwa nini CCM inaogopa maandamano namna hii?

mtu anaandamana mwenyewe, njaa yake, jua lake, mvua yake na hata silaha yoyote mkononi mwake hana- sasa wewe kitakupunguzia nini ukimwacha aandamanee kisha asepe zake ?
Watu wenye nia ovu huwa wanatumia maandamano kifanya vitendo vya kihalifu. Ndio sababu unahitaji kibali ili vyombo vya dola vijipange.
 
Hatuogopi. Idadi ya wana Mbeya ni kubwa sana ikilinganishwa na idadi ya askari wote nchini.
Polisi na jeshi waje Mbeya kesho, Mafiat kujifunza mauaji ya kimbari. Watatukuta tumejàa tele.
Uzuri Wana mbeya Wana ghala la chakula
Hawana njaa
Huwa wanakula wanashiba😂🤣
Wana shibe na nguvu
Sio wanaume wa buguruni wanaoshindia miguu ya kuku na maji ya kandoro🤣😂
 
Back
Top Bottom