Chongolo Mgeni Rasmi kikao cha Wakuu wa Shule za umoja wa wazazi Tanzania

Chongolo Mgeni Rasmi kikao cha Wakuu wa Shule za umoja wa wazazi Tanzania

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
CHONGOLO MGENI RASMI KIKAO CHA WAKUU WA SHULE ZA UMOJA WA WAZAZI TANZANIA- ASUBUHI HII.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo, Leo Ijumaa tarehe 15 Julai, 2022 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kikao cha Wakuu wa Shule za Umoja wa Wazazi Tanzania.

Kikao hicho kinatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma kuanzia saa nne asubuhi.

IMG-20220714-WA0032.jpg
IMG-20220714-WA0031.jpg

#Chongolokazini
#Kaziinaendelea
 
Awaambie ukweli hao wakuu wa shule na baadhi ya makada wenzake wa ccm, shule zinakufa kwa sababu ya upigaji uliopitiliza.

Leo shule ya sekondari Meta kule Mbeya imekufa kwa sababu ya ufisadi! Mbalizi nayo iko mahututi! Walimu hawalipiwi mishahara! Sangu Sekondari haisikiki tena! Achana na shule nyingine! Zote ziko hoi bin taaban! Kisa tu ubadhirifu uliopitiliza.

Yaani ccm na ufisadi/wizi kama pete na kidole vile.
 
NA NYINGINE ZIMEKUFA KABISA HAZINA WANAFUNZI YAMEBAKI MAJENGO TU YANI HATA KUKODISHA TU INASHINDIKANA
KAMA TUMESHINDWA TUTAFUTE MUWEKEZAJI
 
Awaambie ukweli hao wakuu wa shule na baadhi ya makada wenzake wa ccm, shule zinakufa kwa sababu ya upigaji uliopitiliza.

Leo shule ya sekondari Meta kule Mbeya imekufa kwa sababu ya ufisadi! Mbalizi nayo iko mahututi! Walimu hawalipiwi mishahara! Sangu Sekondari haisikiki tena! Achana na shule nyingine! Zote ziko hoi bin taaban! Kisa tu ubadhirifu uliopitiliza.

Yaani ccm na ufisadi/wizi kama pete na kidole vile.
Katibu mkuu amekusikia.

CCM ni sikivu
 
CHONGOLO MGENI RASMI KIKAO CHA WAKUU WA SHULE ZA UMOJA WA WAZAZI TANZANIA- ASUBUHI HII.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo, Leo Ijumaa tarehe 15 Julai, 2022 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kikao cha Wakuu wa Shule za Umoja wa Wazazi Tanzania.

Kikao hicho kinatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma kuanzia saa nne asubuhi.


#Chongolokazini
#Kaziinaendelea
JIWE na sanaa zake zote kwa hizi shule hakufua dafu. Shule za kata ndo zimeua hizi shule maana hazina tena maajabu.
 
Sijwahi kuona kwingine duniani chama cha siasa kinamiliki na kuendesha shule.
 
Sijwahi kuona kwingine duniani chama cha siasa kinamiliki na kuendesha shule.
Chama cha wapigaji hicho! Kimejimilikisha pia maeneo ya wazi na kujenga vibanda vya biashara, majengo ya serikali, viwanja vya michezo, nk.

Hela zote zinazopatikana kwenye hiyo miradi, kabla ya kufika sehemu husika, zinapigwa kwanza na wajanja. Magufuli alijaribu kuunda tume iliyoongozwa na Dr. Bashiru Ali kuchunguza alichokiita 'mali za chama'!! Ila mpaka leo taarifa zake hazijulikani zilipo.
 
CHONGOLO MGENI RASMI KIKAO CHA WAKUU WA SHULE ZA UMOJA WA WAZAZI TANZANIA- ASUBUHI HII.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo, Leo Ijumaa tarehe 15 Julai, 2022 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kikao cha Wakuu wa Shule za Umoja wa Wazazi Tanzania.

Kikao hicho kinatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma kuanzia saa nne asubuhi.


#Chongolokazini
#Kaziinaendelea
Tukumbushane.

Agenda kuu Kwa sasa nchini ni Katiba Mpya.

Rasimu ya Judge Warioba irudi mezani, mjadala uanzie hapo.

Amen
 
Back
Top Bottom