Chukua tahadhari kabla haujanunua hisa za makampuni haya

Chukua tahadhari kabla haujanunua hisa za makampuni haya

greater than

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2018
Posts
1,653
Reaction score
3,060
Soko la hisa la Dar es Salaam lina makampuni 26 yaliyo jiorodhesha. Katika hayo kuna makampuni yanayofanya vibaya na yale yanayo chechemea.

Tuangalie orodha ya makampuni yaliyo na hali mbaya na uchukue tahadhari kabla ya kuwekeza.

JATU
Hili lina husika na cloud farming. Naliweka kwenye orodha kwani sijaona hawajachapisha taarifa za fedha kwa mwaka wa pili mfululizo na hata ripoti yao mwaka haipo mitandaoni.

SWALA
Kampuni inayojihusisha na utafiti wa mafuta huko kitalu cha Morogoro.
-Haijawahi tengeneza faida kwani bado haijafanikiwa kupata hayo mafuta.
-Usije nunua hisa huko mana nchi yetu haina historia kupatikana kwa mafuta.

TATEPA
Mara ya mwisho mwisho hii kampuni kuweka taarifa zake za fedha ni mwaka 2020,nimezisaka mpaka .Ilikuwa na hasara ya Billioni 4.Ikiwa na madeni mengi kuliko amana. Na sioni kama Uongozi wa bodi yake kama una hangaika kuiokoa hii kampuni.

PRECISION AIRLINE
Hii kampuni ya ndege nahisi ishajifia,mana hakuna cha maana nilicho kiona kwenye taarifa zake.
Taarifa zake za mwisho ilikuwa ni za 2019 na zilionesha ilipata hasara ya zaidi ya Billion 44.

MUCOBA

Hii Benki ya wakulima Iringa ni ipo hoi kana kwamba hata taarifa zake hazipatikaniki. Wakinga, Wabena, Wapangwa na Wahehe wekezeni kwenye Benki yenu.

ĎCB
Hii Benki ya Halmashauri ya Jiji la Dar Ina zalisha faida kiduchu, haina mawazo ya ukuaji, haitoi gawio, haiwekezi kwenye tafiti, haina mipango mipya.

Chukua tahadhari unapotaka kuwekeza kwenye haya makampuni.

Uchambuzi huu nimefanya kwa kutumia data zilizopo mtandaoni,kusoma ripoti za mwaka na kuhudhuria baadhi ya vikao vya wanalima.

Karibuni mchangie.
 
Mkuu nikinunua hisa za milioni 200 voda gawio naweza pata kiasi gani kwa mwaka? Kwa mtazamo wako, kununua hisa za milioni 200 na kununua kiwanja cha biashara chenye thamani hiyo ni upi uwekezaji bora?
Gharama ya hisa 1 ya voda = 550
mtaji wako ni 200,000,000

Idadi ya hisa utakazopata = mtaji wako /gharama ya hisa 1
=200,000,000/550
=363,636
so kwa hiyo hela utapata hisa 363,363

GAWIO
kwa mwaka wa fedha wa 2023
Bodi ya Vodacom Tanzania imependekeza gawio la Tsh.12 kila hisa 1.
jumla ya gawio= gawio kwa hisa x idadi ya hisa unazo miliki
=12 x 36,3636
=4,363,632
=Utapata tsh 4,363,632 kama sehemu ya faida ya kampuni yako ya Voda kwa mwaka 2023.....

Kwa mwaka 2021 sijaona kama walitoa gawio.
hili ndiyo Gawio lao dogo kulitoa kwa kipindi cha miaka 5,Gawio lao kubwa kutoa lilikuwa Tsh 24,ambapo lingekufanya upate tsh million 8+
 
Kuna hawa TCCIA wamebadili jina kuwa AFRIPRISE sijui wamekuja na mpya gani
Kwa miaka mingi hawakuwa wakitoa gawio
actually TICL/TCCIA/AFRIPRISE walitoa gawio la Tsh 6 kwa mwaka 2020,Tsh 10 kwa mwaka 2021,Tsh 13 kwa mwaka 2022....
Kampuni ya AFRIPRISE imeinunua kampuni hiyo na TCCIA na kuamua kuibadilisha jina...
 
Soko la hisa la Dar es salaam lina makampuni 26 yaliyo jiorodhesha. Katika hayo kuna makampuni yanayofanya vibaya na yale yanayo chechemea .
Tuangalie orodha ya makampuni yaliyo na hali mbaya na uchukue tahadhari kabla ya kuwekeza....

JATU
Hili lina husika na cloud farming...
Naliweka kwenye orodha kwani sijaona hawajachapisha taarifa za fedha kwa mwaka wa pili mfululizo na hata ripoti yao mwaka haipo mitandaoni...

SWALA
Kampuni inayojihusisha na utafiti wa mafuta huko kitalu cha Morogoro.
-Haijawahi tengeneza faida kwani bado haijafanikiwa kupata hayo mafuta.
-Usije nunua hisa huko mana nchi yetu haina historia kupatikana kwa mafuta.

TATEPA
Mara ya mwisho mwisho hii kampuni kuweka taarifa zake za fedha ni mwaka 2020,nimezisaka mpaka .Ilikuwa na hasara ya Billioni 4.Ikiwa na madeni mengi kuliko amana.
Na sioni kama Uongozi wa bodi yake kama una hangaika kuiokoa hii kampuni.

PRECISION AIRLINE
Hii kampuni ya ndege nahisi ishajifia,mana hakuna cha maana nilicho kiona kwenye taarifa zake.
Taarifa zake za mwisho ilikuwa ni za 2019 na zilionesha ilipata hasara ya zaidi ya Billion 44.

MUCOBA
Hii Benki ya wakulima Iringa ni ipo hoi...kanakwamba hata taarifa zake hazipatikaniki...
Wakinga,Wabena,Wapangwa na Wahehe wekezeni kwenye Benki yenu.

ĎCB
Hii Benki ya Halmashauri ya Jiji la Dar.
Ina zalisha faida kiduchu
Haina mawazo ya ukuaji
Haitoi gawio
Haiwekezi kwenye tafiti
Haina mipango mipya.

Chukua tahadhari unapotaka kuwekeza kwenye haya makampuni.

Uchambuzi huu nimefanya kwa kutumia data zilizopo mtandaoni,kusoma ripoti za mwaka na kuhudhuria baadhi ya vikao vya wanalima...

Karibuni mchangie.
Kwamba Hakuna utafiti wowote ulioonyesha Tanzania kuna Mafuta? I never thought of this.
 
Gharama ya hisa 1 ya voda = 550
mtaji wako ni 200,000,000

Idadi ya hisa utakazopata = mtaji wako /gharama ya hisa 1
=200,000,000/550
=363,636
so kwa hiyo hela utapata hisa 363,363

GAWIO
kwa mwaka wa fedha wa 2023
Bodi ya Vodacom Tanzania imependekeza gawio la Tsh.12 kila hisa 1.
jumla ya gawio= gawio kwa hisa x idadi ya hisa unazo miliki
=12 x 36,3636
=4,363,632
=Utapata tsh 4,363,632 kama sehemu ya faida ya kampuni yako ya Voda kwa mwaka 2023.....

Kwa mwaka 2021 sijaona kama walitoa gawio.
hili ndiyo Gawio lao dogo kulitoa kwa kipindi cha miaka 5,Gawio lao kubwa kutoa lilikuwa Tsh 24,ambapo lingekufanya upate tsh million 8+
Milioni 200 kuzalisha milioni 4 kwa mwaka ni hasara na upotevu wa muda.
Mtu mwenye mtaji wa milioni 200 anatakiwa kuipata faida ya milioni 4 ndani ya wiki 1 tu.
 
Milioni 200 kuzalisha milioni 4 kwa mwaka ni hasara na upotevu wa muda.
Mtu mwenye mtaji wa milioni 200 anatakiwa kuipata faida ya milioni 4 ndani ya wiki 1 tu.
kwanini Rostam Azizi alikuwa anamili hisa zaidi ya 15% VOdacom
Kwanini Bakhresa anamiliki hisa katika moja ya makampuni yaliyopo DSE

Watu hawanunui hisa kwasababu ya gawio tu,ila kuna kuzitumia hisa kama....
  • Dhamana katika kuomba mikopo
  • kuongeza thamani ya pesa yake
  • kuondoa uhangaikaji wa kuendesha biashara....
Na gawio laendana na faida ya kampuni husika.
 
Gharama ya hisa 1 ya voda = 550
mtaji wako ni 200,000,000

Idadi ya hisa utakazopata = mtaji wako /gharama ya hisa 1
=200,000,000/550
=363,636
so kwa hiyo hela utapata hisa 363,363

GAWIO
kwa mwaka wa fedha wa 2023
Bodi ya Vodacom Tanzania imependekeza gawio la Tsh.12 kila hisa 1.
jumla ya gawio= gawio kwa hisa x idadi ya hisa unazo miliki
=12 x 36,3636
=4,363,632
=Utapata tsh 4,363,632 kama sehemu ya faida ya kampuni yako ya Voda kwa mwaka 2023.....

Kwa mwaka 2021 sijaona kama walitoa gawio.
hili ndiyo Gawio lao dogo kulitoa kwa kipindi cha miaka 5,Gawio lao kubwa kutoa lilikuwa Tsh 24,ambapo lingekufanya upate tsh million 8+
Biashara kichaa, 200m nipate faida ya 4m kwa mwaka? Hata ukiweka fixed deposit ya 10% hukosi 20m.

Biashara ya hisa bongo ni biashara kichaa.
 
Gharama ya hisa 1 ya voda = 550
mtaji wako ni 200,000,000

Idadi ya hisa utakazopata = mtaji wako /gharama ya hisa 1
=200,000,000/550
=363,636
so kwa hiyo hela utapata hisa 363,363

GAWIO
kwa mwaka wa fedha wa 2023
Bodi ya Vodacom Tanzania imependekeza gawio la Tsh.12 kila hisa 1.
jumla ya gawio= gawio kwa hisa x idadi ya hisa unazo miliki
=12 x 36,3636
=4,363,632
=Utapata tsh 4,363,632 kama sehemu ya faida ya kampuni yako ya Voda kwa mwaka 2023.....

Kwa mwaka 2021 sijaona kama walitoa gawio.
hili ndiyo Gawio lao dogo kulitoa kwa kipindi cha miaka 5,Gawio lao kubwa kutoa lilikuwa Tsh 24,ambapo lingekufanya upate tsh million 8+
Ila hii ya hisa inataka moyo! Yaani milioni 200 upate milioni 4 kwa mwaka, si ujinga huu?
 
Kuna benki ya waalimu MCB -Mwalimu Commercial Bank.

Hii nadhani ndio inayoongoza kwa utapeli kwenye soko la hisa....

Hisa zake hazinunuliki wala kuuzika, mikutano hawafanyi na haijulikani kama wanatengeneza faida au hasara. 😲
 
Biashara kichaa, 200m nipate faida ya 4m kwa mwaka? Hata ukiweka fixed deposit ya 10% hukosi 20m.

Biashara ya hisa bongo ni biashara kichaa.
Aya tutajie hiyo benki inayokupa fixed deposit ya 10%....
Na pili hiyo ndiyo lowest ambayo imepaata kutolewa na Voda within 5 years....
Lakini hapohapo huo mtaji 200M ungekuwa umeshaongezeka thamani kwa zaidi ya coz hisa za Voda zimekuwa zikiongezeka thamani...
 
Back
Top Bottom