Chuma Ulete: Ni kweli ipo? Ipi dawa ya kuidhibiti?

Chuma Ulete: Ni kweli ipo? Ipi dawa ya kuidhibiti?

Ili kutengeneza chuma ulete , mchawi huchukua njugu mawe nyeusi na kuimeza nzima nzima bila kuitafuna halafu anainya na kuichukua tena. Baada ya hapo atachukua mti unaitwa Kilinda Mgunda, anaunguza pamoja na hiyo njugu mawe nyeusi aliyo imeza na kuitoa kwa njia ya haja kubwa. Vinachomwa kisha vinasagwa na kuwa unga unga. Anachanjwa kwenye pembe zote za mwili wake na kupakwa hiyo ndumba halafu ndumba nyingine inawekwa kwenye chungu kisha inapikwa pamoja sarafu halafu anatumia kuoga
Baada ya hapo ataenda kuwaalika majini wa chuma ulete ulete. Jinsi majini wa chuma ulete wanavyo alikwa. Kinachukuliwa kipande cha ngozi ya hayawani wa mwituni, ngozi ya kinyonga iliyo kaushwa, pamoja na pangaa ya mti. Pangaa ya mti ni mti ulio ota juu ya mti mwingine.
Vitu vyote hivi vinachomwa pamoja na njugu mawe na kisha kusagwa na kufungwa kwenye kitambaa chekundu pamoja na jinni halafu vinaenda kufungwa kichawi kwenye mti mkubwa kwa muda wa siku tatu usiku na mchana.
Baada ya hapo, ndumba hiyo itatolewa mahali hapo na kwenda kuwekwa kichawi katika eneo la sokoni vinapo uzwa vitu.
Baada ya siku tatu ndumba hiyo inachukuliwa inaenda kuzikwa kaburini kwa muda wa siku tatu.
Siku ya saba, ndumba hiyo inachukuliwa na kupelekwa kwenye chumba maalumu, kwa ajili ya kupikwa kichawi. Basi baada ya hapo, hiyo chuma ulete itakuwa inafuata amri ya mtu huyo na kumpatia chochote anacho kitaka.
wewe una maghorofa mangapi
 
Duh kweli namba zinasomeka mpaka watu wameamua kuja na mawazo mbadala jinsi ya kutafuta hela baada ya kuzikosa kwa tochi.
 
Ushindwe ktk jina la Yesu,juzi tu ujue kuna jamaa kafa na nyoka wake,acheni kuendekeza ushirikina yani wafanye kazi wengine ule mwingine inahusuu?? Asiefanya kazi na asile
Mzembe huyo
 
Ili kutengeneza chuma ulete , mchawi huchukua njugu mawe nyeusi na kuimeza nzima nzima bila kuitafuna halafu anainya na kuichukua tena. Baada ya hapo atachukua mti unaitwa Kilinda Mgunda, anaunguza pamoja na hiyo njugu mawe nyeusi aliyo imeza na kuitoa kwa njia ya haja kubwa. Vinachomwa kisha vinasagwa na kuwa unga unga. Anachanjwa kwenye pembe zote za mwili wake na kupakwa hiyo ndumba halafu ndumba nyingine inawekwa kwenye chungu kisha inapikwa pamoja sarafu halafu anatumia kuoga
Baada ya hapo ataenda kuwaalika majini wa chuma ulete ulete. Jinsi majini wa chuma ulete wanavyo alikwa. Kinachukuliwa kipande cha ngozi ya hayawani wa mwituni, ngozi ya kinyonga iliyo kaushwa, pamoja na pangaa ya mti. Pangaa ya mti ni mti ulio ota juu ya mti mwingine.
Vitu vyote hivi vinachomwa pamoja na njugu mawe na kisha kusagwa na kufungwa kwenye kitambaa chekundu pamoja na jinni halafu vinaenda kufungwa kichawi kwenye mti mkubwa kwa muda wa siku tatu usiku na mchana.
Baada ya hapo, ndumba hiyo itatolewa mahali hapo na kwenda kuwekwa kichawi katika eneo la sokoni vinapo uzwa vitu.
Baada ya siku tatu ndumba hiyo inachukuliwa inaenda kuzikwa kaburini kwa muda wa siku tatu.
Siku ya saba, ndumba hiyo inachukuliwa na kupelekwa kwenye chumba maalumu, kwa ajili ya kupikwa kichawi. Basi baada ya hapo, hiyo chuma ulete itakuwa inafuata amri ya mtu huyo na kumpatia chochote anacho kitaka.
Process ndefu hivyo!!
 
A,aleykum warahmatullah wabarakatu Naam wapendwa leo tunamzungumzia jini aitwae Ghull .Jini Ghull ni mionhoni mwa zile aina 660 za majini. Jini Ghull ni jini ambae ana vituko na madhara makubwa kwa binadam.

Washirikina wote dunian huwa hawafanyi kazi zao za kichawi pasipo kushirikiana na huyu jini nikiwa na maana huyu jini ndiye mwalimu wa wachawi suratu baqara2:202 mara nyingi jini huyu hupenda kujibadili katika umbo la paka mweusi au Nyoka ndipo unapokuta unamuona nyoka au paka mara akakupotea hapo hapo na usijue kaenda wapi.

Unaweza kukutana na paka njiani akakuvimbia ili usipite na la kumfanya usiwe nalo kias cha kwamba mwili ukakusisimka na kutoa vipele vya baridi.Kuna mgonjwa ambae aliwahu kufika ofisini kwangu na kueleza kwamba maradhi yalimfika baada tu ya kusikia mlio wa paka dirishani kwake alianza kuumwa na kichwa kutetemeka kwa mwili na alivyokwenda hospital hakuonekana na tatizo lolote lakini yeye mwenyewe na nduguze wanamuona mgonjwa sasa tatizo hilo ni miongoni mwa matatizo yanayosababishwa na huyo jini Ghulli.

Watu wengi sana wanajua kwamba jini chuma ulete kazi yake ni kuiba pesa tu lakini ni jini ambae ana kazi nyingi sana sana

BAADHI YA KAZI ZA JINI GHULL (CHUMA ULETE)

(1)Humsababishia mtu kupoteza pesa pasipo sababu au pesa kutumika pasipo matumiz ya kueleweka

(2)Husababisha maradhi yasiyoeleweka yani kutoonekana katika vipimo vya kisayansi maradhi hayo

(3)Kumfanya mtu augue mara kwa mara

(4)Kuiba mimba mwanamama anaweza kubeba mimba lakin baada ya muda mimba ikapotea pasipo sababu za msingi

DALILI ZA MTU MWENYE JINI GHULI

1Kuota ana safiri safiri

2 Kuota yupo katika vikao si sehem ya ofisi

3 Kuota ana pika pika vyakula

4Kuota anafukia makaburi au anazika

5Kuota unafanya kazi nzito na ukiamka asubuh umechoka

6Kuota unafukuzwa na wanyama wakali au kundi la maadui kisha ukapaa

7Kuharibu mimba ya 8-9

8Kuwa na kawaida ya kujifungua watoto waliokufa tumboni

9 Mwanaume kutokukomaa kwa mbegu za uzazi

10 Kupotelewa na vitu pasipo sababu

Hizo ni baadhi ya dalili somo lijalo WACHAWI WANAMPATAJE JINI GHULL NA KUFANYA NAE KAZI? Lakini pia tutaangalia mikataba yake na wachawi wanayokubaliana katika kazi

e977a52eeaecc7a6b0ca17f69d1e2f9d.jpg
 
A,aleykum warahmatullah wabarakatu tukiwa tunaendelea na somo letu la kumfahan jini Chuma ulete na teyar tumeshaona dalili za jini huyo na baadhi ya kazi zake embu keo tuendelee kujua anapatikana vipi na mikataba wanayoingia na binadam

Namna jini huyu anavyopatikana kwanza ieleweke kwamba majini in viumbe kwamaana hiyo jini atengenezwi na binadam Bali kuna njia ambazo unaweza kuzitumia katika kuwaita majini na ukashirikiana nao katika shughuli zako (WAJUZI WANAJUA)

Sasa jini huyu Chuma ulete wanachokifanya washirikina huchukua mchanganyiko wa vitu 9 (KABUN)Mchanganyiko wa vitu hivyo huwa wanaita Kabun nitavitaja baadhi ya vitu hivyo vichache

1Chungu au chupa
2Ngozi ya mjusi aitwae sorokoto
3Kitambaa cheusi

Hivyo ni baadhi ya vitu kuvitaja vyote si vyema sababu watu wengine wanaweza kujaribu na ikaleta madhara baada ya kuchukua vitu hivyo vyote kisha uweka katika chungu hiko kitambaa cheusi hufungwa juu ya hiko chungu na kukipeleka makbara (makaburini) na huchagua kaburi mojawapo na kukifukia.Hapo hutegemea mchawi anamtaka Chuma ulete wa ukubwa gani hivyo chungu hiko hukaa kwa idadi ya masiku lakini huanza na siku 11, 21, 23 huchukua masiku ya witiri.Baada ya siku hizo kukamilika mchawi anakwenda kukifukua chungu hicho ifahamike Luna maneno hapa lazima ayaseme na hata katika kukifukia kuna maneno lazma ayaseme ni maneno ya kujikufurisha kwa ALLAH
Baada ya kukifukua chungu hicho hutokea paka mweusi baada ya hapo hutokea him a mtoto anayeweza kuongea au Mzee hapo jini anakuwa teyari ameshafika na mikataba inafanywa.Unaweza ukaona mzaha lakini ukweli wa mambo uko hivyo

MIKATABA

Mikataba ambayo wanaingia baina ya huyu jini na mchawi.Mwanadam ambae anafikia hatua hii maana yake teyari alikwishaingia au kujiunga uchawini zamani na kuna mikataba pia ambayo mtu anapojiunga na uchawi huingia katika hiyo mikataba nitaiekezea katika somo lijalo Leo tuangalie mikataba ya Chuma ulete na binadam

1Chuma ulete hutaka kujua ataishi wapi
Hapa mchawi huchagua sehem ya huyo jini atakapoishi kama Njia panda,Makaburini,Nyumbani au mashuleni

2 Chuma ulete hutaka kujua nini atakula
Sote tunajua chakula kikubwa cha majini ni damu na haijalishi ya kiumbe gani hivyo mchawi humwambia nitakuchinjia ng'ombe, Mbuzi,Njiwa,Kuku n.k

3Muda wa huyo jini kupata chakula chake

Hapa mchawi huchagua kila mwisho wa wiki, Mwezi,Mwaka na jini hula pale pale anapoishi kama ulichagua Nyumban basi iitakubid uchinje kutokana na ule muda mliokubaliana na hapa ndipo unaweza kumkuta mtu kila ifikapo masiku hayo lazma achinje ingawa si kila anayechinja bas yupo katika mkataba huo hapana wengine hupenda tu kuchinja na kutoa swadaka ya haki kabisa kuwapa mboga masikini n.k MNIELEWE JAMANI kuna wale ambao huchKIASI
jini huyo akakae njia panda hawa Mara nyingi huwaambia majini hao watakula kitakachomwagika hapo BASI JINI HUYO HUTENGENEZA AJALI

4 JINI HUYU CHUMA ULETE ANAPOMLETEA MCHAWI PESA SHARTI LAKE HUTAKA MCHAWI HUYO ATUMIE SIKU HIYO HIYO PESA HIZO TENA SI KWA KUJENGA AU KUSOMWSHEA BALI ANUNULIE UCHAWI

5 JINI HUYO UWA HAIBI PESA ZOTE BALI HUIBA KWA KUPUNGUZA KIASI NA KUACHA KIASI.

Inshaallah hiyo ni baadhi ya mikataba tutakuja kuangalia MIKATABA NA VIAPO ANAVOVIFANYA MCHAWI ANAPOTAKA KUINGIA KATIKA UCHAWI NA HII VIAPO UWA VINAENDA KWA VYEO

INSHAALLAH

eb8edbdf0852dc0476ed29b544441a53.jpg
 
Mmmhh si mchezo na viapo vya jini ambaye atachukua sura yangu yani niwe kama na pacha fake inakuwaje?
 
Hivi kwa nini ukitaka pesa yako isibebwe na chuma ulete lazima uichane kidogo kule kwenye pembe ya pesa?
 
Hivi kwa nini ukitaka pesa yako isibebwe na chuma ulete lazima uichane kidogo kule kwenye pembe ya pesa?
Ww dogo ni pimbi sana. Yaani ww ndio ulikuwa unajifanya unamjua shetani zaid??ndezi sanaa we dogo na utakula jeuri yako
 
Back
Top Bottom