BOB MARLEY ALIVYO UAWA NA MAREKANI .
NA, Noel Shao.
Wakala wa CIA anakiri kuhusika moja kwa kwa juu ya kifo cha Mwana muziki wa reggae Bob Marley.
Mkurugenzi wa CIA, Bill Oxley, amefanya mfululizo wa maajabu tangu alipofikishwa kwenye Hospitali ya Mercy huko Maine Jumatatu ya wiki hii na kuambiwa kuwa ana wiki chache za kuishi. Anasema alifanya mauaji 17 kwa serikali kwa ajili ya Amerika kati ya 1974 na 1985, ikiwa ni pamoja na kumuua mwana muziki Bob Marley.
Oxley, ambaye alifanya kazi na CIA kwa miaka 29, anasema mara nyingi alitumiwa na CIA , na kuua watu ambao ni tishio kwa malengo ya shirika hilo.
Alifundishwa kama sniper na markman, (Muuwaji Mkuu). Wakala huyu ana uzoefu mkubwa na mbinu zaidi zisizo za kawaida za kuwadhuru watu, kwa kutumia vitu mbalimbali km sumu, mabomu, na saratani.
Mauaji mengi alifanya kati ya mwaka 1974 - 1985, wakati ana hudumu ktk shiriki hilo, anasema alikuwa sehemu ya kiini cha uendeshaji cha wanachama watatu ambao ulifanya mauaji ya kisiasa nchini kote na mara kwa mara katika nchi za kigeni.
Waathirika wao wengi walikuwa wanaharakati wa kisiasa, waandishi wa habari, na viongozi mbalimbali, lakini pia anakiri kuua wanasayansi wachache, watafiti wa matibabu, wasanii na wanamuziki ambao wana mawazo makubwa na ushawishi, hasa walio kuwa ni tishio kwa maslahi ya Marekani."
Anasema hakuwa na tatizo la kumuuawa Bob Marley, kwa sababu "nilikuwa mwaminifu , niliamini CIA, na sikuwa na shaka ya motisha ya shirika hilo. Nimekuwa nimeelewa kwamba wakati mwingine dhabihu zinapaswa kufanywa kwa manufaa zaidi. "
Lakini Oxley anakiri kwamba Bob Marley bado ni wa pekee kati ya waathirika wake alisha wahi kuwaua, kwa sababu yeye ndiye aliyeathirika.
"Wengine ilikuwa kawaida. Bob Marley alikuwa Bob Marley.
Anasema "nilikuwa hisia zilizochanganywa" kuhusu kifo cha Bob Marley. Kwa upande mmoja, Marley alikuwa "Mtu mzuri, roho nzuri" na "zawadi kubwa za kisanii" ambazo hazikustahili kupunguzwa maisha yake. Lakini kwa mujibu wa Oxley, Bob Marley pia aliweka malengo ya CIA katika hatari na kutishia kuwepo kwa Marekani.
Alifanikiwa kuunda mapinduzi yaliyotumia muziki kama chombo cha nguvu zaidi kuliko risasi na mabomu. Bob Marley mwaka wa 1976 alikuwa tishio kubwa sana kimataifa na nguvu kubwa zilizofichwa kutekeleza mpango wao wa utaratibu mpya wa dunia.
Bob Marley alikuwa na mafanikio mno, na maarufu sana, pia mwenye ushawishi mkubwa.
Rastaman wa Jamaika ambaye alianza kutumia fedha na umaarufu ili kusaidia watu duniani kote ambazo zilikuwa na hatari za moja kwa moja na CIA.
"Ili kuwa mwaminifu, alisaini hati yake ya kifo chake . (to be honest, He signed his own death warrant)
"Si kama sisi hatukumuonya. Tuliwatuma watu wachache nyumbani kwake huko Kingston, mara kadhaa.
Alisema pia waliratibu jaribu la kumpiga risasi katika makazi ya Marley ambayo ilimuacha mwimbaji huyo na majeraha ya mkono na kifua. "anasema pamoja na juhudi hizo za kumpelekea ujumbe . Hakuwasikiliza wala kuacha alicho kuwa anafanya. "
Siku kadhaa baada ya kutoka hospitali, Bob Marley alisafiri kwenda ktk milima na alitumia muda mrefu kujiandaa kwa tamasha kubwa la muziki.
Kulingana na Oxley, alitumia sifa za vyombo vya habari ili kumpata Bob Marley wakati wa akiwa ktk makazi yake huko milimani. Alijitambulisha kama mpiga picha maarufu anayefanya kazi na New York Times, na akampa Bob Marley zawadi.
"Nilimpa jozi ya Converse All Stars. Ukubwa wa size 10, alipokuwa akijaribu kwenye kiatu sahihi, alilia 'OUUCH.'
"Hapo ndipo. Uhai wake ulpoifika mwisho pale pale . Msumari katika kiatu ulikuwa una virusi vya saratani/kansa na bakteria. Kimsumari kilimchoma ngozi yake" Nilichofanya, nilikuwa muuguzi mzuri. "
"Kulikuwa na mfululizo wa mauaji ya juu ulio kuwa utamaduni Marekani mwishoni mwa miaka ya sitini, na mapema miaka ya sabini. Wakati huo na Bob Marley alikuwa target, na ulikuwa utaratibu wa siku zote. Kwa Bob Hakuna risasi zaidi na kelele zilizopigwa. "
Oxley anasema aliendelea kuwasiliana kwa ukaribu na Marley wakati wa miaka ya mwisho ya maisha yake hasa akiwa Hospitalini, akihakikisha kuwa ushauri wa matibabu aliokuwa akipokea huko Paris, London na Marekani ungemuua kwa haraka kuliko kumponya." Na hatimaye, alikufa kutokana na kansa Mei 1981. Akiwa na umri wa miaka 36 tu.
Anasema, "wakati wa mwisho Bob alinyoa rasta zake, na kabla ya kufa alikonda sana na uzito wake ulikuwa umeshuka mno.
"Alikuwa dhaifu sana, Alikuwa amepungua mno. Kansa ilikuwa imefanya kazi yake . "
"Siku aliyokufa huko Miami ilikuwa siku ya majuto na mbaya kwa wakati wote katika historia ya kazi yangu. Nilihisi vibaya sana. Kwa muda mrefu sikuwa na furaha kwa kifo chake.
" Lakini hatimaye nilitambua ni kazi ambayo lazima ifanyike, kwa ajili yataifa la Amerika. "
[HASHTAG]#Nimeitafsiri[/HASHTAG] kutoka kwenye mtandao.
Nini Maoni Yako?
Ndimi, Noel Shao [HASHTAG]#mjenziWaTanzaniaMpya[/HASHTAG]
O