Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

Wafungiwe tu kama watangazaji wenyewe kina Mwijaku unategemea nn?[emoji13][emoji13]
 
Hivi yale magazeti pendwa ya chama na musiba hayakuonekana kama yamekosea kurusha habari hizo hizo zilizorushwa na Clouds?

Sababu clouds walisoma magazeti yaliyoandika hivyo lakini mwisho wa siku Clouds ndio imewajibishwa, ebu tusubiri labda uhuru na jamvi nao watachukuliwa hatua
 
Upo sahihi sana kiongozi
 
Hata kama wanakubali kuwa wanasesere wa CCM wasifikiri ccm ina rafiki ccm inachotaka ni kututawala kwa mabavu na kutukandamiza
Waambie wamuulize Mbatia.
Maana walimvuta kaingia 18 akaanza kutamba ana kwenda kuwa KUB. sasa hata viti maalum hajui kama atapewa.
 
Hawa wanaofungia vyombo vya habari wangetafakari kwanza wanapoteza ajira za watanzania wangapi? Au hao walishatengeneza ajira ngapi? Au hao hawaoni hii changamoto ya ajira?

Wakati mwingine watanzania tunakatishana tamaa wenyewe, hili suala la kutangaza matokeo kabla ya tume ni suala la kupewa onyo tu ingetosha kuliko kutukosesha habari wiki nzima.

Wajue pia kuna vipindi vya kuwasaidia watu kama njia panda, je wanajua kua wameharibia watu kusaidiwa?
 
Hahahahah waandishi wa habari huu mwaka wenu hadi mkome..

Lissu njoo utukomboe baba tulipofikia inatosha.
 
Nasikilizaga Power breakfast mara nyingi asubuhi Clouds FM ila sijawahi kuona affiliation ya kipindi na CCM, kina Masoud huwa wanaongea indirect. Clouds 360 pale Clouds tv ndio wazee wa kujipendekeza

Na hii habari ya kupita bila kupingwa si iliandikwa hadi kwenye magazeti? Je na wao wamefungiwa?
 
Naomba kuelimishwa nanyi wabobevu wa sheria, hivi katika shauri hili nani ni MLALAMIKAJI na nani ni MLALAMIKIWA? Je hizo pande mbili zimekutanishwa na TCRA (Mamlaka) kabla ya kutoa hukumu?

Naomba kuelimishwa kidogo.


Ahsante
 
[emoji106] [emoji106]
 
kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…