Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

Ni jambo jema!
Safi sana,hii ndio faida na mshahara wa kushabikia utawala unaovunja Sheria wazi wazi,

kipindi kile cha issue ya Mbowe walikuwa wanashadadia sana kila siku kumuhoji Ndugai na wajinga wenzake wa CCM. Na lissu aliwaambia kuwa kwa utawala huu kila mtu ataguswa kwa wakati wake.
 
Kilaba fungia na haya magazeti mawili
Gazeti la TISS na Bagaile Mulaga Musiba Majura na gazeti pendwa la CCM. Haliwezi fungiwa aisee.

Clouds walirusha pingamiz la Lisu Twitter halafu yule mom Rose Majinge mke wa ndugu yake Kusaga alogombea Urais kura za maoni Chadema pia anawaponza clouds
 
Leo Tarehe 27 August,Clouds FM radio na Clouds TV wamekatika ghafla Hewani mida ya saa8 mchana hivi mpaka saiv...Lakini kuna Sauti ya George Bantu inaskika mala kwa mala kama Tangazo au Jingle ikisema..

"Clouds FM radio inachukua fursa hii kuomba radhi wasikilizaji wake na Watanzania kwa ujumla kwa kukiuka kanuni na taratibu za maudhui ya Uchaguzi wa mwaka 2020,Clouds FM radio inaahidi kujikita kwenye weledi zaidi katika siku za Usoni"
@NgarenaroBoy.
 
Nyie hamjagundua plan

Lissu ataanza kampeni DSM

Vyombo hivi vya habari sasa hivi kwenye kipindi rasmi cha kampeni ni vigumu kuvidhibiti kutotangaza habari za wapizani 100%, yaani wataanza kutupia tupia, na hilo watawala hawalitaki!

Kwa hiyo plan ni ifungie Cloud Media ambayo inasikilizwa na wananchi wengi zaidi kuliko vyombo vingine ili kupisha kimbunga cha Dar, maana CHADEMA wamejiandaa kufungulia kampeni Dar

Sasa Dar ikikubali kwa Lissu, ni rahisi mikoa mingine kuitika!

Kwa hiyo watawala wanataka siku CCM wakiwa Dar, Cloud Media itakuwa imeshakuwa huru kurusha mikutano ya CCM na hivyo kuwapa CCM coverage kubwa.

Eleweni hii michezo ya kisiasa inavyochezwa nyie
 
Kosa nikutangaza matokeo bila tume kutangaza hafu mda wa rufaa ulikuwa bado kuisha. Hapo wamefanya kosa.
Kwani wao si walitangaza kile kilichotangazwa na wasimamizi wa uchaguzi?

Mbona tume wao walitangaza kumpitisha Magufuli wakati muda wa pingamizi ulikuwa bado ?
 
Eleweni nyie ndugu zangu, CCM haiwezi kuingia mgogoro na vyombo vya habari kizembe zembe namna hii! Haswa kipindi hiki cha kampeni.

Hapo kuna mchezo mnachezewa, na mchezo wenyewe umesukwa kiakili ili msing'amue.

Huo mchezo ni wa blackmail kwa vyombo vya habari kuwa ni lazima viendelee kuwa vitiifu, vya kutoa ushirikiano mzuri kwa chama tawala kipindi hiki cha kampeni. Lakini pia kudeal na Chadema

Plot niliyoing'amua ni hii ifuatayo:

Kwa kuwa Lissu ataanzia kampeni DSM kesho ama keshokutwa, na atafanya mikutano Dar siku tatu mfululizo.

Vyombo hivi vya habari sasa hivi kwenye kipindi rasmi cha kampeni ni vigumu kuvidhibiti kutotangaza habari za wapizani 100%, yaani wataanza kutupia tupia, na hilo watawala hawalitaki! Na hata kama havitaki kuzungumzia kampeni za upinzani bado vitapata pressure kutoka kwa umma kuwa kwa nini havirushi taarifa za upinzani?- Vinaogopa kudharauliwa na watu

Kwa hiyo plan ni ifungie Cloud Media ambayo inasikilizwa na wananchi wengi zaidi kuliko vyombo vingine kwa wiki nzima ili kupisha kimbunga cha Dar ili kuzuia uwezekano wowote wa clods media kurusha mikutano au habari za mikutano hiyo ya Lissu. Kumbuka CHADEMA wamejiandaa kufungulia kampeni Dar. Na nina wasiwasi viongozi wa clouds ambao ni makada wa CCM huenda wametoa ushirikiano mzuri kwenye kuwezesha hili.

Sasa Dar ikikubali kwa Lissu, ni rahisi mikoa mingine kuitika!

Kwa hiyo watawala wanataka siku CCM wakiwa Dar, Cloud Media itakuwa imeshakuwa huru kurusha mikutano ya CCM na hivyo kuwapa CCM coverage kubwa.
 
Tanzania Communication Regulatory Authority( TCRA) imeagiza Clouds TV na Redio kusitisha matangazo yao kwa muda wa siku saba kuanzia kesho 28 Agosti hadi 3 Septemba 2020 kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji na kanuni ndogo za utangazaji za uchaguzi. Pia, wametakiwa kuomba radhi siku nzima leo.

TCRA Wameyasema hayo Wakati wakiongea na Wanahabari na kudai kwamba, Clouds Media Walitangaza Takwimu za Wagombea waliopita bila kupingwa kinyume na Sheria ya Uchaguzi inavyotaka na kwamba Tume ya Uchaguzi ilikuwa haijawatangaza.

Hivi karibuni Tume ya Uchaguzi ilalamikia baadhi ya vyombo vya habari kutangaza majina ya Waliopita bila kupingwa.
Kazi kwao
 
Back
Top Bottom