Cocacola kubandika majina ya watu bila ruhusa/malipo, Jacline Wolper aomba wanasheria kuingilia kati


Yeye anapelekewa kopo hata haulizi ni la nini? Anapokea tuu. Likimlipukiaje?

Aende zake huko. Ruge angemwekea pesa za Escrow kwenye account yake angeenda kutafuta ushauri huko Insta?

Ushauri akatafute kwa wanasheria siyo insta.
 

Sasa kama sheria siyo professional yao waende kwa wanasheria kutafuta ushauri wa kisheria badala ya kulialia kwenye mitandao.

Kwani Rihanna ni mwanasheria? Mbona hakulialia kwenye mitandao baada ya image yake kutumika bila ridhaa yake?

Yeye alitafuta lawyer kesi ikaenda mahakama akashinda akafidiwa mkwanja wake.

Hivi Wolper anaweza kuunga foleni na watoto yatima kwenye mlango wa mwananaharakati kuomba ushauri au tuseme legal aid?
 
Yeye anapelekewa kopo hata haulizi ni la nini? Anapokea tuu. Likimlipukiaje?

Aende zake huko. Ruge angemwekea pesa za Escrow kwenye account yake angeenda kutafuta ushauri huko Insta?

Ushauri akatafute kwa wanasheria siyo insta.

Suala la pesa za Escrow kuwekewa kwenye account ni tofauti kabisa na zawadi ya kopoz, pia wanasheria wapo insta vilevile inaweza kuwa sehemu mojawapo ya kupata contacts zao wanasheria...
 
Suala la pesa za Escrow kuwekewa kwenye account ni tofauti kabisa na zawadi ya kopoz, pia wanasheria wapo insta

Haya basi tunasubiri tuone kesi yao mahakamani kama wana huo ubavu.

Wasitegemee wanaharakati wawasadie kwa sababu wako bize kuwasaidia the most disadvantaged people in the society na siyo hawa maselebu wanaotamba kuwa wanaishi large.

Mtu unaletewa kopo hata hujiulizi, inawezekana hata maji yaliyokuwa mle ndani keshayanywa halafu ndo anakuja kulalama mitandaoni?

vilevile inaweza kuwa sehemu mojawapo ya kupata contacts zao wanasheria...

Kama wana "heshima kubwa" kama anavyodai hana haja ya kutafuta wanasheria insta.
 

kwahiyo unamaanisha watoto yatima pekee ndio wanastahili kwenda kwa wanaharakati kuomba ushauri!!??, wanasheria wapo kwenye mitandao pia hata humu JF lipo jukwaa la SHERIA ambalo linatoa ushauri kwa watu mbalimbali wenye kuhitaji ushauri au unadhani na JF sio mtandao!!???
 

sawa sawa mkuu kama watakua wanasoma humu watakua wamekuelewa na nadhani ushauri wako wataufanyia kazi...
 
kwahiyo unamaanisha watoto yatima pekee ndio wanastahili kwenda kwa wanaharakati kuomba ushauri!!??,

Nimetumia watoto yatima kama one of the most disadvantaged people in the society.

Sasa unaweza kusema mlalamikaji ni one most disadvantaged people in the society kiasi cha kuhitaji kusaidiwa na wanaharakati?

Kwamba tumfanyie huyu mlalamikaji a "professional work undertaken voluntarily and without payment or at a reduced fee as a public service"? No way!! Alipe.

wanasheria wapo kwenye mitandao pia hata humu JF lipo jukwaa la SHERIA ambalo linatoa ushauri kwa watu mbalimbali wenye kuhitaji ushauri au unadhani na JF sio mtandao!!???

Kama kweli upo serious, kama kweli unahitaji ushauri wa kisheria the best option ni kutafuta mwanasheria na kukushauri professionally.

Yes, kwenye mitandao kuna wanasheria, lakini vipi kama wakimpa ushauri mbaya na yeye aka-act upon to her detriment, ataweza kuja kuwashtaki wanasheria wa mitandaoni for their negligence?

Wafanye kama alivyofanya Rihanna. Watafute mwanasheria awashauri kama wana case. Kama wana kesi waipeleke kampuni ya Coca Cola mahakamani na kudai fidia kwa kutumia "majina" yao bila "ridhaa" yao.

Narudia tena https://www.jamiiforums.com/celebri...ngo-acheni-kulilia;-fanyeni-kama-rihanna.html
 

Kujielewa na kujua thamani yako ni kitu muhim sana maishani. So sad these people don't know their values. This is and wil definetely promote coca cola. Maskin, wanawafanyia kazi bure, coca cola wanaingiza hela kupitia haya matangazo, wao wanachopata ni kuuza sura. So sad, wamefanya matangazo kwa kulipwa soda moja lenye jina lao tu.

Eti "thanx coca I got myn", mwingine "ahsante coca na mimiapa", masikin hata kiswahil chenyewe kuandika shida.

Poor them, wasanii wetu wengi hawajitambui.

Pamoja na kutojitambua kwao, coca cola kwa hili wamefanya uhuni mkubwa. Wametumia udhaifu wao wa kutojitambua kuwanyonya, wamewafanyisha matangazo ya bidhaa yao ya coca cola bila kuwalipa. Huu ni wiz wa mchana kweupe. Kuwashtaki itakuwa ngumu coz wengi hawajasajil majina yao km brand, but coca cola wanatakiwa waambiwe walichofanya wamekosea na ni unyonyaji mkubwa. Somebody must tell them.
 
sawa sawa mkuu kama watakua wanasoma humu watakua wamekuelewa na nadhani ushauri wako wataufanyia kazi...

Alitakiwa awe ameshashariwa na mwanasheria au PR wake kwanza kabla ya kukimbilia Inta kuandika aliyoandika.

Kuuza CD feki ni kosa na la jinai. Lakini kampuni kutumia jina lake bila ridhaa yake ni suala la madai.

Ajaribu kwenye kuripoti polisi kuwa Coca Cola wametumia jina lake bila ridhaa yake aone kama watamsadia.
 
Mkimaliza kubishana mniambie niwapatie coca zenye id zenu
 
kwanza unajichanganya sijazungumzia kwamba waliopewa zawadi ni wasanii tu la hasha, waliopewa zawadi ni watu wenye majina maarufu katika jamii ambayo ni target ya kutangaza katika soko bidhaa hii,

Sasa nilipojichanganya ni wapi? Unaweza kunionyesha?

halafu pia sijaona watu wa kawaida wakisema wamepewa zawadi za kopo kama walivyofanya hao super stars!!!

Kwa vile tu wewe hujaona hiyo haina maana kuwa hakuna. Usichanganye mambo.
 

Ushauri ni nzuri sana ...lakini matusi ya nn ndugu? Naamini hajui na anahitaji msaada wa kueleweshwa bila jazba....
 

CC to Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:

- For sure ametumwa kuandika kitu asichokijua amelipokea kopo amelipiga picha na kulitundika Instagram halafu anasema hakutaka, kweli akili ni mali sana kabla hawajamletea wamempigia simu wakamwambia wana kopo lenye jina lake wanagependa kumletea akakubali bila ya kumuwekea bunduki kwa mbali, wakamfuata akawasubiri akalipokea akalipiga picha nalo akaweka Instagram leo analia hakutaka, hahahahahahahahaha hawa ndio wasanii wa yule jamaa yenu wa Njiro, hahahahahahahahaha

Le Mutuz
 

we ulilipwa sh ngapi? au na wewe umetumika tu
 

Ni kweli kabisa inabidi hawe na intellectual property lasivyo anajiaangaisha tu,hopeless elimu inahitajika kwa hawa watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…