Consession na lease agreements zinapoandaliwa muda huu, watendaji serikalini wakumbuke maana ya usiri kazini (confidentiality)

Consession na lease agreements zinapoandaliwa muda huu, watendaji serikalini wakumbuke maana ya usiri kazini (confidentiality)

Steven Joel Ntamusano

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
5,203
Reaction score
3,913
Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.
 
Aliyevujisha hiyo siri anahitaji pongezi na ikiwezekana wtz tumchangie chochote tulichonacho ili kumfanya uzalendo wake uwe maradufu.pamoja na kuwa serikali imeshinda hii kesi iliyoamuliwa na hizi mahakama zetu kibogoyo,Ni mpumbavu na punguani pekee anayeweza kuuona huu mkataba wa kishenzi na wa milele kati bandari na dp world kuwa ni mzuri.
 
Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.
Hili gazeti ulioleta hapa halina maana yoyote, maana hata mkataba wa gas kuna waliokuja na porojo kama zako. Leo hii tunaambiwa gas sio yetu!
 
Hili gazeti ulioleta hapa halina maana yoyote, maana hata mkataba wa gas kuna waliokuja na porojo kama zako. Leo hii tunaambiwa gas sio yetu!
Walioandika na kusaini mkataba wa gas sio hawa wa mkataba wa DP World, usipende sana kukariri masuala yanayofanywa na serikali mengine yanajumuisha utaalam wa kina.
 
Aliyevujisha hiyo siri anahitaji pongezi na ikiwezekana wtz tumchangie chochote tulichonacho ili kumfanya uzalendo wake uwe maradufu.pamoja na kuwa serikali imeshinda hii kesi iliyoamuliwa na hizi mahakama zetu kibogoyo,Ni mpumbavu na punguani pekee anayeweza kuuona huu mkataba wa kishenzi na wa milele kati bandari na dp world kuwa ni mzuri.
Litakuwa fundisho kwa wenye dhamana wengine huko serikalini, wameona namna serikali ilivyohenyeshwa mitandaoni kwa suala lenye kutakiwa kuwa ni la siri.
 
Kwanini siri,kama raia sitakiwi kujua linaloendelea kwenye taifa langu🤔
Mkataba una mambo mengi ya kitaalam kuhusu kampuni husika na upande wa serikali.

Kuna teknolojia mpya ambayo labda kampuni haitaki mshindani wake wa kibiashara azifahamu.

Kuna faida za kiuwekezaji anazoweza kuipa nchi moja na akainyima nchi nyingine na yote hayo huandikwa kwenye kurasa za mikataba.

Dunia nzima wawekezaji hupenda usiri kwani unaambatana na ubunifu wao wa kiutendaji unaowafanya wakaendelea kuwa juu kwa maana ya makampuni yao kuendelea kupata tender mbalimbali.
 
Was
Mkataba una mambo mengi ya kitaalam kuhusu kampuni husika na upande wa serikali.

Kuna teknolojia mpya ambayo labda kampuni haitaki mshindani wake wa kibiashara azifahamu.

Kuna faida za kiuwekezaji anazoweza kuipa nchi moja na akainyima nchi nyingine na yote hayo huandikwa kwenye kurasa za mikataba.

Dunia nzima wawekezaji hupenda usiri kwani unaambatana na ubunifu wao wa kiutendaji unaowafanya wakaendelea kuwa juu kwa maana ya makampuni yao kuendelea kupata tender mbalimbali.
Wasimamizi wa hayo matumaini ya mafanikio ndio hawa hawa wa Tz wa kukosa ufanisi kila nyanja au watakuwa malaika toka mbinguni 🤔.Tunayo mifano hai hata siku ya zamani,akina RAHCo, Netgroup solutions,ubinafsishaji viwanda vya Baba wa taifa.Tena leo wapo binadamu wanasema mikataba huu iwe siri,mbona tutauzwa wote bila kujua🤔
 
Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.
Porojo nyiingi
 
Was

Wasimamizi wa hayo matumaini ya mafanikio ndio hawa hawa wa Tz wa kukosa ufanisi kila nyanja au watakuwa malaika toka mbinguni 🤔.Tunayo mifano hai hata siku ya zamani,akina RAHCo, Netgroup solutions,ubinafsishaji viwanda vya Baba wa taifa.Tena leo wapo binadamu wanasema mikataba huu iwe siri,mbona tutauzwa wote bila kujua🤔
Usiri wa mkataba ni taratibu iliyopo dunia nzima. Huwezi kutumia uzembe na ufisadi miaka ya nyuma kama kigezo cha kuanika siri za makampuni makubwa ambao ni wateja wetu tunaofanya nao biashara.

Hata sisi tunaodai kutaka kujua kinachoandikwa kwenye hiyo mikataba wengi wetu hatuna elimu zenye kuweza kuboresha chochote kwenye hizo biashara kubwa zinazofanyika kati ya serikali na makampuni makubwa ya kigeni.
 
Nipe tofauti yake, au hao haikuwa serikali?
Huu mkataba wa TPA umeandikwa kwa kutegemea uzoefu mbovu wa kampuni hii na mataifa mbalimbali. Hakuna aliyekurupuka kufikia hatua ya kuandaa hii mikataba.

Unayo haki ya kutilia wasiwasi juu ya uwezo wa wataalam wetu lakini hakiwezi kuwa kigezo cha kupuuza uzoefu na elimu walizonazo kwenye sekta husika.
 
Back
Top Bottom