Consession na lease agreements zinapoandaliwa muda huu, watendaji serikalini wakumbuke maana ya usiri kazini (confidentiality)

Consession na lease agreements zinapoandaliwa muda huu, watendaji serikalini wakumbuke maana ya usiri kazini (confidentiality)

Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.
Ni Watumishi wasio na Maadili ya kazi ndio huvujisha,Hawa wakibainika wafinywe mazima maana sheria ya usalama wa Taifa na kutunza Siri za miaka 20 hazitoshi wanaweza tumia ujanja ujanja kukwepa kifungo.
 
Ni Watumishi wasio na Maadili ya kazi ndio huvujisha,Hawa wakibainika wafinywe mazima maana sheria ya usalama wa Taifa na kutunza Siri za miaka 20 hazitoshi wanaweza tumia ujanja ujanja kukwepa kifungo.
Siasa za kuutafuta urais zimeanza mapema. Hata yale maneno aliyoyasema RC Chalamila kule Kagera kuhusu mtendaji mmoja wa serikali kwenda huko nje kutafuta pesa kwa ajili ya kampeni za 2025 yana ukweli. Hakusema kufurahisha baraza tu.
 
Huu mkataba wa TPA umeandikwa kwa kutegemea uzoefu mbovu wa kampuni hii na mataifa mbalimbali. Hakuna aliyekurupuka kufikia hatua ya kuandaa hii mikataba.

Unayo haki ya kutilia wasiwasi juu ya uwezo wa wataalam wetu lakini hakiwezi kuwa kigezo cha kupuuza uzoefu na elimu walizonazo kwenye sekta husika.
Hawa wataalamu ndio akina professor Ossoro wamefika kwenye mahakama zinazofuata sheria na sio maagizo ya serikali, wameishia kuongea mambo ya aibu. Lakini wakati walipokuwa wanatengeneza hizo taratibu walikuwa wanalazimisha tuwaone ni watu makini sana.

Inshort hakuna lolote jipya unatuambia maana tunajua uwezo duni walionao hao wanajifanya wataalamu wetu. Na ushahidi wa uwezo wao duni tunao kwenye mikataba mingi.
 
Siasa za kuutafuta urais zimeanza mapema. Hata yale maneno aliyoyasema RC Chalamila kule Kagera kuhusu mtendaji mmoja wa serikali kwenda huko nje kutafuta pesa kwa ajili ya kampeni za 2025 yana ukweli. Hakusema kufurahisha baraza tu.
Hiyo ndio namna urais unatafutwa siku hizi, kisha wakifika hata wakati wa uchaguzi wanaishia kupora uchaguzi. Halafu watu hao wanaotafuta madaraka kwa mbinu chafu, wakiingia madarakani ndio mnalazimisha tuwaone ni watu makini. Ila nyie chawa mna vituko vya hatari.
 
Hawa wataalamu ndio akina professor Ossoro wamefika kwenye mahakama zinazofuata sheria na sio maagizo ya serikali, wameishia kuongea mambo ya aibu. Lakini wakati walipokuwa wanatengeneza hizo taratibu walikuwa wanalazimisha tuwaone ni watu makini sana.

Inshort hakuna lolote jipya unatuambia maana tunajua uwezo duni walionao hao wanajifanya wataalamu wetu. Na ushahidi wa uwezo wao duni tunao kwenye mikataba mingi.
Una haki ya kuwa na maoni hayo kwa uzoefu halisi wa taifa hili. Nakuhakikishia tu kuwa suala la DP World limeshughulikiwa na mikono salama sana mpaka dakika hii.
 
Hiyo ndio namna urais unatafutwa siku hizi, kisha wakifika hata wakati wa uchaguzi wanaishia kupora uchaguzi. Halafu watu hao wanaotafuta madaraka kwa mbinu chafu, wakiingia madarakani ndio mnalazimisha tuwaone ni watu makini. Ila nyie chawa mna vituko vya hatari.
Kuniita chawa ni kunitukana, kwa sababu hunijui. Mpaka unakuwa na mawazo ya kuporwa uchaguzi maana yake umetengeneza mazingira ya kuibiwa, hilo ni tatizo lako binafsi sio la kitaifa.

Kumbuka hao hao wanaodaiwa kuiba kura ndio wanaotandaza umeme nchi nzima umefika. Ndio wanaojenga SGR na inakaribia kumalizika. Wanafanya mengi sana na kupata uhalali wa kuongoza nchi hata kama kuna baadhi ya matukio ya wizi wa kura.

Huo wizi hauwezi kuwa ni doa kwenye uongozi wao ambao upo karibu na shida za watu na unaziishi kila siku.
 
Huu mkataba wa TPA umeandikwa kwa kutegemea uzoefu mbovu wa kampuni hii na mataifa mbalimbali. Hakuna aliyekurupuka kufikia hatua ya kuandaa hii mikataba.

Unayo haki ya kutilia wasiwasi juu ya uwezo wa wataalam wetu lakini hakiwezi kuwa kigezo cha kupuuza uzoefu na elimu walizonazo kwenye sekta husika.
Yule Johari na Elimu yake ya kuungaunga ndiyo mtaalamu wa kumuamini!
Aisee,hiyo rushwa aliyotoa DPW imewalevya sana!
Kama tungezingatia weledi basi tulitarajia watu kama Professor Shivji,Jaji Warioba,Tundu Lissu et al wakihusishwa ku-negotiate hiyo mikataba na siyo hao Wahuni ambao wanaifanya nchi kuipigia magoti City-state ya Dubai!
 
Mikataba na concession za michongo! Hakuna ushindani ni mwendo wa kupeana RUSHWA na 10% basi.
Mimi ni CCM lakini wenzetu wanaokula hadi kuvembewa hawaoni hata kinachotokea Africa Magharibi!
Wananchi wakishachoka Serikali za kifisadi basi hujichukulia njia wanayojua wao!
Suala la Bandari jinsi lilivyopelekwa na Rais Samia Lina Mazingira ya RUSHWA kubwa sana!
Hakuna mtu mwenye akili anayeweza kumuunga Samia mkono kwenye hili!
Machawa wake waendelee kumdanganya!
 
Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.

Hata wakificha huwa wanaumbuka tu kwenye mahakama za kimataifa na kuliingizia gharama taifa letu,bora wa weke wazi ili vipengele vibovu vijadiliwe wapate kurekebisha.
 
Kosa la kuruhusu mkataba kuvuja na wasiotakiwa kuuona limeshafanyika na gharama ya kujitetea zimekuwa kubwa kwa upande wa serikalini. Mijadala imekuwa ni mingi kutoka kwa watu wa kada mbalimbali juu ya masuala ya kisheria.

Nani alivujisha siri za serikali? Wahusika wanajuana na wameshaiona gharama ya walichokifanya. Serikali imepoteza ule usiri uliokuwepo kuanzia awamu ya Hayati Benjamin Mkapa kurudi awamu ya pili na ya kwanza. Kuwepo kwa watu wanaotumia anwani ya Kigogo 2014 na Kigogo 20014 kumekuwa ni mwiba kwa mipango ya kiserikalini.

Kuzungukana ni kwingi sana kuanzia kwa watendaji wa ikulu yenyewe mpaka huko kwenye mawizara mbalimbali. Makundi ni mengi na yanatafuna ufanisi mzima wa baadhi ya maazimio na miradi ya kiserikali. Aliyeuvujisha huu mkataba wa bandari anaweza kuwa ni mmoja wa wale wenye nia ya kutafuta urais wa mwaka 2025 au 2030 hivyo akadhani kuwa kuichimba serikali ya SSH ni njia ya kujirahisishia kazi ya kwenda ikulu.

Niliuelewa ukimya wa Rais na wasaidizi wake hata pale mbinu za wapinzani wake zilipomtaka afungue mdomo aongelee suala la bandari. Alifahamu mtego wa wapinzani wake na akaamua kuendelea na masuala mengine ya kiserikali kama vile hahusiki na suala zima la bandari. Alijua ni kwa kiasi gani wapigaji wa TPA walikuwa wakiumia mioyo yao kutaka kujua msimamo wa serikali ni upi.

Bahati mbaya sana Mababa Askofu wenye kuheshimika kwenye jamii zetu wakarekodiwa zile video fupi na zikarushwa mitandaoni ilimradi tu kuigawa jamii ya kitanzania. Huko kanisani mapadre wakaanza kuhubiri kuhusu bandari bila ya kuwa na uelewa mpana wa hicho wanachokiongelea mbele ya waumini wao.

Adui pia akawatumia wazee wenye ushawishi na umaarufu ndani ya CCM lengo likiwa kauli yao iwe ndio rejea ya wanajamii wanaofuatilia suala zima. Kwamba Profesa Shivji au Profesa Lipumba akitoa maoni yake kuhusu bandari sisi wengine tulifanya makosa kuwakosoa na kuhoji juu ya maadili mazima ya wao kulikosoa lengo zima la uwekezaji!

Utanganyika na uzanzibari vikaanza kuongelewa kama vile ni hatua njema kabisa kwa mustakabali wa Tanzania. Watu wakasahau kuwa yapo maisha baada ya kuwepo kwa Tanganyika kama nchi mpya, wakasahau kuwa ule umaskini wetu upo pale pale hata baada ya kujitenga na kuwa nchi mbili kamili.

Yote haya yamesababishwa na wale walioshindwa kutunza siri za serikali na wakaamua kuisaliti ofisi inayowalipa mishahara!. Wapo wengi hata hawakutaka kujiuliza hiyo bandari imekuwa ni yetu tangu siku bendera inapandishwa pale uwanja wa Taifa iweje leo eti ndio iuzwe!

Mbegu ya ubaguzi iliyotaka kupandikizwa miongoni mwa watanzania imeshindwa rasmi kule Mbeya baada ya hukumu iliyotolewa na majaji juu ya suala zima la uwekezaji bandarini. Mbegu ya wao na sisi imepoteza kabisa mashiko baada ya DP World kuruhusiwa kisheria kufanya uwekezaji katika bandari yetu.

Ombi maalum kwa wanasheria wanaoandaa mikataba ya kibiashara muda huu katika sehemu fulani ya dunia, ni kutorudia kosa kama lililoufanya mchakato mzima wa uwekezaji kuchukua muda na kuzusha maneno mengi kutoka kwa wanasheria uchwara wa mitandaoni.

Nadhani ni wazoefu kiasi cha kufahamu maana ya kutunza siri haswa katika suala nyeti na lenye maadui wengi kama hili la uwekezaji pale TPA. Wamejifungia wakiumiza vichwa vyao ili waje na vifungu vyenye maslahi kwa wafanyabiashara wazalendo.

Iwapo biashara nzima ya uwekezaji itakwenda kuharibika mbele ya safari na Tanzania ikalazimika kulipa mabilioni ya pesa basi wao wakiwa ni wanasheria wa taifa hawataweza kukwepa lawama zozote zile zitakazoibuka, ni muda wa kuwa makini kadri wawezavyo wakati wa uandishi wa vifungu vyote vitakavyokuwemo katika hiyo mikataba miwili muhimu iliyobakia.

Uwekezaji huu ukikaa sawa na kuzaa faida kwa upande wa TRA watakumbukwa na majina yao yataingizwa kwenye zile kurasa maalum za mashujaa wa Taifa, wakishindwa kuweka uzalendo mbele na weledi wao ukaliangusha taifa maana yake majina yao yatakwenda kupoteza kabisa heshima ambayo wameipata mpaka muda huu.
Upumbavu NAO Ni kipaji.
 
Yule Johari na Elimu yake ya kuungaunga ndiyo mtaalamu wa kumuamini!
Aisee,hiyo rushwa aliyotoa DPW imewalevya sana!
Kama tungezingatia weledi basi tulitarajia watu kama Professor Shivji,Jaji Warioba,Tundu Lissu et al wakihusishwa ku-negotiate hiyo mikataba na siyo hao Wahuni ambao wanaifanya nchi kuipigia magoti City-state ya Dubai!
Kama hao unaowaamini wewe wanawakilishwa na mawazo ya Wakili Mwabukusi basi mmeshindwa vibaya na hili la kushindwa mliambiwa siku nyingi kabla ya hukumu.

Mnaleta ujuaji wa kutaka kuandama nchi nzima, mtaumia sana.
 
Hata wakificha huwa wanaumbuka tu kwenye mahakama za kimataifa na kuliingizia gharama taifa letu,bora wa weke wazi ili vipengele vibovu vijadiliwe wapate kurekebisha.
Kule mahakamani ilikuwa ni sehemu sahihi ya kujenga uhalali wa hoja za wanaopinga uwekezaji lakini kushindwa kwao mbele ya sheria ni kielelezo cha ukosefu wa hoja za maana zenye haki ya kujadiliwa.
 
Yule Johari na Elimu yake ya kuungaunga ndiyo mtaalamu wa kumuamini!
Aisee,hiyo rushwa aliyotoa DPW imewalevya sana!
Kama tungezingatia weledi basi tulitarajia watu kama Professor Shivji,Jaji Warioba,Tundu Lissu et al wakihusishwa ku-negotiate hiyo mikataba na siyo hao Wahuni ambao wanaifanya nchi kuipigia magoti City-state ya Dubai!
Johari aliwashinda wanasheria wa Malawi kwenye suala zima la haki ya kumiliki Ziwa Nyasa, amefanya mengi ya maana.

Johari amekuwa kwenye timu za serikali za majadiliano mengi ya kisheria na wenye elimu na uelewa wanaujua mchango wake.

Usitishwe na hayo majina ya kina Shivji na Lissu hao ni maarufu tu lakini yapo mengi yenye kuwazidi vimo.
 
Hili gazeti ulioleta hapa halina maana yoyote, maana hata mkataba wa gas kuna waliokuja na porojo kama zako. Leo hii tunaambiwa gas sio yetu!
Ati anadai wanaochakata HGA wakikosea walaumiwe. Kweli? Yaani waingize nchi kwenye crisis afu itoshe mulaumiwa badala ya kunyongwa? Anyway, sikujua kama kuna timu inaendelea na HGA huko hadi baada ya kuhabarishwa na huyu mdau stevin Joel. Kumbe ndo maana humu siku hizi akina The Boss Na faiza foxy wameadimika hapa JF kumbe wanacharaza HGA kati ya Tz na Dubai? Kweli nchi inachezewa.
 
Was

Wasimamizi wa hayo matumaini ya mafanikio ndio hawa hawa wa Tz wa kukosa ufanisi kila nyanja au watakuwa malaika toka mbinguni 🤔.Tunayo mifano hai hata siku ya zamani,akina RAHCo, Netgroup solutions,ubinafsishaji viwanda vya Baba wa taifa.Tena leo wapo binadamu wanasema mikataba huu iwe siri,mbona tutauzwa wote bila kujua🤔
Changamoto ni kwamba watumishi wengi wa serikali hawana ownership ya fikra zao, hii Ina maana wanaazima akili za wanasiasa katika kuamua kitaalamu.
Bahati mbaya siasa zaweza kumpa madaraka mtu ambaye ana uwezo mdogo sana wa fikra na hivyo wataalamu kutumia uwezo huohuo.
Ni watumishi wachache sana, hata wanasiasa kwenye serikali, hayati Magufuli akiwa mfano wa kuigwa, wenye uthubutu wa kutumia akili zao kwa uwazi katika kuamua. Wengi wakiwa na madaraka makubwa hutumia vyombo vya dola ambavyo navyo huongozwa na watu wa aina hiyo hiyo ya kuazima fikra katika kutekeleza majukumu yake ya siku kwa siku.
Wageni wengi wanajua utamaduni huu na hivyo kutumia kufanya lobbying na kufanikisha wizi wao dhidi ya taifa letu kiulaini.
Kinachotakiwa ni kila raia na watumishi wa uma kutumia akili zao kwa mantiki katika nafasi zao kwa maslahi mapana ya taifa ambapo maslahi yao binafsi yapo ndani.
 
Ati anadai wanaochakata HGA wakikosea walaumiwe. Kweli? Yaani waingize nchi kwenye crisis afu itoshe mulaumiwa badala ya kunyongwa? Anyway, sikujua kama kuna timu inaendelea na HGA huko hadi baada ya kuhabarishwa na huyu mdau stevin Joel. Kumbe ndo maana humu siku hizi akina The Boss Na faiza foxy wameadimika hapa JF kumbe wanacharaza HGA kati ya Tz na Dubai? Kweli nchi inachezewa.
Uelewa wetu mdogo unatufanya tuamini kwamba nchi inachezewa ukweli ni kwamba nchi inakwenda kuwafagia wapigaji wa pale TPA ili pesa halali na nyingi iweze kuingia kwenye uchumi mkuu.

Ili mzigo mwingi unaotoka DRC na Rwanda uweze kusafiri kwenda nje ya nchi kwa haraka zaidi na tusipoteze soko la ushoroba huu.

Mungu aliyeiumba Tanzania na kuiweka hapa ilipo kijiografia alishamaliza wajibu wake siku nyingi inabakia wajibu wetu wa kiserikali wa kuitumia faida hiyo ili igeuke kuwa pesa nyingi.
 
Back
Top Bottom