Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

We uhuru jr Una uhuru wa kumuita chizi mwenzako kisa mungu, lakini hauna uhuru kuthibitisha uwepo wake?

It's Scars
Sijamwita chizi kwa sababu sababu ya Mungu,mbona wewe hauamini Mungu na sijakwita chizi? Mara zote sie tunaoamini Mungu huwa tunaitwa machizi na majina ya kila aina kisa tu tunaamini Mungu na huyo jamaa ni mmoja wenye kuongea maneno mabovu kwa sie wenye kuamini Mungu na hujiona ana akili sana kisa tu haamini Mungu.

Sasa nashangaa kaja na sababu ya kichizi kueleza et kwanini watu wanaamini Mungu,mtu mwenye akili timamu hawezi kuja na sababu kama hiyo aliyokuja kutueleza hapa.

Wewe ndio hauna uhuru wa kuthibitisha kutokuwepo kwa huyo Mungu,na kwa sababu umeambiwa kisichokuwepo hakithibitishiki.
 
Sidhani kama umeelewa,sijazungumzia kufanyika maovu kwa kivuli cha dini bali nazungumzia mtu binafsi kufanya maovu na hali ya kuwa anaamini dini na imani ya uwepo wa Mungu.
 
Hizo nukuu unahakika gani kwamba zimesema ukweli?

Maana hata Mimi pia naweza kukupa nukuu kuonesha uhodari wa spiderman katika kukwea magorofa utakubali?

Sasa tutajuaje kua ulichokinukuu ni kweli na sio porojo za waarabu?

It's Scars

Usipate shida Qur'an yenyewe inakupa jibu...

Qur'an 2:

23. Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya mfano wake, na muwaite mashahidi wenu badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema kweli. 23


24. Na mkitofanya - na wala hamtofanya kamwe - basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe walio andaliwa hao wanao kanusha. 24



Haya tunasubiri utimize hiyo "challenge". Miaka zaidi ya 1400 imetolewa , mpaka.leo hajatokea hata mmoja aliyeweza, jaribu bahati yako tRNA washirikishe na makafiri wenzako wote.


Hahaha unaongelea "spider"? Kuna sura nzima ndani ya Qur'an inabeba jina Hilo, imeshushwa zaidi ya miaka 1400 nyuma. Kwi kwi kwi teh teh teh, wewe ndio leo unamjuwa? Ulilala usingizi mzito sana.
 
Unajuaje kua habari za mungu sio za kufikirika kama ilivyo spiderman?

Unaweza kuthibitisha?

It's Scars
Hapa umeniamsha Ndugu yangu
Mimi nakuthibitishia
35:3. Enyi watu! Kumbukeni neema za Mwenyezi Mungu juu yenu. Ati yupo muumba mwengine asiye kuwa Mwenyezi Mungu anaye kupeni riziki kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Hapana mungu ila Yeye tu. Basi wapi mnako geuzwa?

5. Enyi watu! Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli. Basi yasikudanganyeni maisha ya dunia, wala mdanganyifu asikudanganyeni juu ya Mwenyezi Mungu.

9. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye zituma Pepo ziyatimue mawingu, nasi tukayafikisha kwenye nchi iliyo kufa (mvua ikanyesha), tukaifufua ardhi( kwa mvua hiyo) baada ya kufa kwake. Ndivyo kama hivyo kutakavyo kuwa kufufuliwa (siku ya mwisho, Na Je ni nani anayeweza kuyafanya hayo asie kuwa Mungu?).

11. Na Mwenyezi Mungu amekuumbeni kutokana na udongo. Kisha kwa tone la manii. Kisha akakufanyeni mwanamume na mwanamke. Na mwanamke yeyote hachukui mimba, wala hazai, ila kwa ilimu yake. Na wala hapewi umri mwenye umri mrefu, wala hapunguziwi katika umri wake, ila yamo hayo katika Kitabu (cha Mungu). Hakika hayo ni mepesi kwa Mwenyezi Mungu. (je ni nani mwengine ayafanyaye hayo asiekuwa Mungu ikiwa unamjuwa)?

34:38. Na wanao jitahidi kuzipinga Ishara zetu, wakaona watashinda, hao watahudhurishwa kwenye adhabu ( hapa duniani kabla ya kufa na siku ya kiama).
Hebu kiri ukweli huu kama kuna yeyote anaye yamiliki haya

huu ndio ushahidi wangu, nipe wa kwako basi
 
Elimu ya mungu ni pana sana ,
Alishajuwa utakvyo kuwa na utakachokichagua,
na kwa kuwa ameahidi kuwa hatomlazimisha mtu katika kutii,
Ila akijitahidi atamsaidia,
Naakipotoka ,shetani yupo anamgoja kumsaidia,
Na akipenda mwenyewe Anaweza kukuokowa kwenye janga hilo na kukuongoza.
Justice ya Mungu si kama vile tuhukumuvyo sisi.
YEYE NI MUNGU MUUMBA KILA KITU NI CHAKE, HUFANYA APENDAVYO.
 
Naona unamtetea Mungu kwa matusi [emoji23][emoji23]
. Mkuu utaenda motoni taratibu [emoji23][emoji120]
Sent using Jamii Forums mobile app
 
majuzi niliona clip moja ya tapeli mmoja anaejiita nabii akiapa corona kamwe haiwezi kuja Tz! kama kawaida niliona wanaomshabikia wakishangilia kwa nguvu sana! kweli wajinga kamwe hawawezi kuisha ktk ulimwengu huu!
Ni wakati wa hawa wanaojiita 'manabii' kutumia mafuta , vitambaa, maji na udongo wao wa upako kuondoa korona! Ni wakati wa hawa wanaosali huko kutambua utapeli na usanii wanaofanyiwa na watu hawa.
 
Tatizo sio hao manabii bali ni watu wenyewe,hao watu kwenye siasa huko nako wanasiasa wanawadanganya sana hadi unashangaa.
 
Asante mwalimu kwa kunielimisha ila usichoke kunifundisha hii elimu pana ya Mungu. Umesema kuwa Mungu "Alishajua utakavyokuwa na utakachokichagua" je kajua kwavile kamuumba makusudi ili binadamu awe vile? Au kuna kipengele cha makubaliano baina ya binadamu na Mungu wakati wa kuumbwa, binadamu mwenyewe achague aumbwe mtu wa aina gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una maswali ya kitoto sana Mwanadamu aliumbwa ili atumie akili na sio miujiza, tafsiri mbaya za wafanyabiashara wa kidini zisikufanye umdhihaki Mungu kiasi hiko
 

Naona umeshindwa kujibu umekimbilia personal attacks 😂
Hata nilichoandika umeshindwa kukielewa, ukizaliwa kwenye familia ya kiislamu una 99% ya kuishia kua muislamu, same for dini nyingine zote, unazaliwa unalishwa uongo unashika toka utotoni kufikia ukubwani inakua ngumu sana kutoka. Its very simple. Sasa wewe endelea kutukana utakufa na umasikini wako haha, poor in mind na poor mfukoni, pole sana. Nimekublock just in case so usipoteze muda kunijibu maana hata notifications sitoziona, sina muda na stupid people mimi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…