Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Mkuu, sijataka kuanzisha mjadala katika hili ndiyo maana sijazungumza kwa kina. Kama hujasikia, dunia haiko kwenye giza bado. Unaweza kujitafutia taarifa mwenyewe.
Weka chanzo cha ulipoyatiwa ukiyoandika au u muongo na mzushi tu hauna kingine.

Uongo uuzuwe wewe halafu mimi nikakutafutie ushahidi?

Fikra za kijinga hizo.
 
Allah/ Mwenyezi Mungu alivyoleta manabii na mitume ni kwa ajili ya Kuonya na Kubashiri sio kuleta maombi watu wasife, na lau kifo kingekuwa na auheni basi wangelipewa hao mitume na manabii umri mrefu hadi leo wangekuwepo ili waendelee kutubashiria na kutuonya.

Hivyo kuwepo kwa viongozi au waumini si ishara ya kuzuia yale atakayo Allah yatendeke. Sisi ni kuendelea kumuomba na kumtumainia yeye (kwa maana dua na ibada zinapunguza au kuondosha mabalaa na mitihani) na kuchukua asbabu (ushauri kutoka kwa mamlaka na wataalamu wa afya) tu ndio wajibu wetu.
 
Weka chanzo cha ulipoyatiwa ukiyoandika au u muongo na mzushi tu hauna kingine.

Uongo uuzuwe wewe halafu mimi nikakutafutie ushahidi?

Fikra za kijinga hizo.
Sawa, mimi nina fikra za kijinga. Hivyo siwezi kusema lolote mbele yako ewe mwenye fikra za kisomi na werevu.
 
Naamini Mungu yupo lakini hainizuii kuhoji

Mimi sio mtumwa wa dini kama wewe
That is the difference between me and you



Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa mie mtumwa ila wewe utakuwa mjinga,kwa sababu huyo Mungu haonekani wala hakuna njia ya kuwasiliana nae kwa kuweza kumuhoji. Sasa huko kuhoji unamuhoji nani? Au mwenzetu unaonanae huyo Mungu ndio maana unajisifu kuhoji?

Kwa sababu kama unaamini Mungu(mtumwa wa Mungu) na hauamini dini(sio mtumwa wa dini) basi huko kuhoji kwako inatakiwa umuhoji Mungu mwenyewe na sio kuhoji dini halafu unajisifu kuhoji.

Unajitia misifa ambayo mwenyewe unajiona una akili sana upo huru kumbe ni ujinga,huwa unanifurahishaga kweli.

Ushawahi kumhoji Mungu hata jambo moja tu?
 
Kwahiyo umetaja spiderman kwa sababu spiderman ni kitu cha kufikirika ?

Sasa nani alikwambia kuwa Mungu ni kitu cha kufikirika tu kama spiderman? Mfanano hapo ni upi?

Mungu ni hadithi zilizo nje ya uhalisia na ndio maana uwepo wake hauthibitishiki nje ya masimulizi yakufikirika

The same goes with Spiderman

It's Scars
 
Teh...ukishashiba ugali wa matembele lazima uwe na mentality za dizaini hii, kuna magonjwa hatari ya tauni yamewahi kuangamiza mamilioni ya watu huko nyuma achana na hii korona, watu waliomba na Mungu akaingilia kati. Najua kwa akili yako fupi utafikiri yalitokomea tu by chance..
 
Unauliza nitawaamini vp wakati nakuelezea hapa kuwa wanatibu hilo tatizo na mtu anapona kabisa na hawapelekwi hospitali,mie sikulazimishi wewe uamini kuwa sababu ya hilo tatizo kuwa ni majini bali nakuelezea tiba ya hilo tatizo ambayo ni kweli na watu hupona. Sasa wewe ukiamini kuwa ni tatizo la magonjwa ya akili ni sawa tu ila kuhusu tiba ni kwa dua hutibu hilo tatizo na ndiyo point yetu hapa.
Unajuaje kua wanapona na sio kwamba ni script iliyochezwa na padre/sheikh ili kuwateka watu kiakili?

It's Scars
 
Viongozi wengi wa dini wa zama hizi ndo wanaofanya Mungu atukanwe kwa wayatendayo na uongo wao,
Lkn nafsini mwangu iwe iwavyo,corona iwepo isiwepo,dini ziwepo zisiwepo naamini Mungu yupo maana binafsi nilishayaona matendo yake kwenye maisha yangu,
Binafsi huwa natamani Mungu awaumbue viongozi wachumia tumbo wa dini za sasa wanaofanya atukanwe,
Waafrika tujifunze kuomba wenyewe,kumuambia Mungu haja zetu wenyewe,tusitegemee hawa matapeli waliopotoka,
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?

Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?

Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.

Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?

Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.

Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.

Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.

Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but i ain't laughing?

Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.

Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?

Kwanini mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?

Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?

Hivi kweli mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?

Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?

====

Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nadhani kwa vizazi viliyopita Mungu/Allah alikuwa anasikiliza maombi ya wanadamu na kuyafanyia kazi haraka.

ila kwa kizazi hiki cha wachungaji wanzinzi(kama gwajima), matepeli(kama wale mashehe wa instagram),Mungu kaamua kula pozi kidogo ili tunyoke.

Mungu kazia hapohapo ili hawa manabii na wachungaji feki wa kizazi hiki wapate kuumbuka.
 
Teh...ukishashiba ugali wa matembele lazima uwe na mentality za dizaini hii, kuna magonjwa hatari ya tauni yamewahi kuangamiza mamilioni ya watu huko nyuma achana na hii korona, watu waliomba na Mungu akaingilia kati. Najua kwa akili yako fupi utafikiri yalitokomea tu by chance..
Kwa hiyo hilo gonjwa la town mungu alilileta kisha akasubiri aombwe ndio aliondoe?, usiniambie hakujua lilipotoka hadi likaua watu wakamuomba ndio akaliondoa.

Mungu hawezi kuzuia gonjwa kabla halijaua watu wake ama hua hajui linapotokea anakija kushtuliwa na maombi?😀😀.

Ukimwi, kansa bado maombi hayajamfikia ili ayaondoe kama alivyoondoa town au hajui kama yapo?

Tuendelee kuomba mkuu.
 
Asante mkuu,
Mm kwa uwazi kabisa huwa nasema hawa watu ni chanzo cha uvivu,upofu,ujinga na umaskini wetu,
Wanafanya watu mateka wao,kwa faida za matumbo yao,
Ndugu Mungu ni Baba yetu,kwa nini sasa umtumie jirani yako kukuombea kwa Baba yako,
Mungu hawezi sikia maombi ya hawa maana wamechanganya Maombi na njaa kwa pamoja,
Hapo hakuna cha mtume wala nabii nacho kiona hapo kuna wawekezaji tu walio wekeza kwenye dini

Mitume na manabii haya ni majina ya kijasiliamali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunawaamini wanasayansi,madaktari n.k halafu wewe unasema hizi sio zama za kuamini? Au wewe huamini wanasayansi na madaktari?
Mi sifungamani na imani

Wewe kama unawaamini wanasayansi mimi niko kinyume kwa kuikubali sayansi na wanasayansi kupitia tafiti zake ambazo zinathibitishika

It's Scars
 
Tusipime nguvu ya Mungu kupitia hawa wachumia tumbo wanaojiita mitume na manabii wa sasa,
Nguvu ya Mungu ipo lkn tatizo tunadhani wanachosema hawa wachumia tumbo ndo nguvu ya Mungu,
Mungu hawezi jibu haya maigizo yanayoitwa maombi kwake yanayofanywa na watu ambao azma yao ya kwanza ni umaarufu na pesa,Mungu hashirikishwi na nia ovu za kitapeli za hawa matapeli,
Virusi vya corona vimekuja kuthibitisha wazi kua maombi hayana msaada wowote kwenye maisha ya binadamu na wala dini haiwezi kuwaokoa binadamu na janga lolote la asili hivyo kuabudu na kufanya maombi ni kazi bure.

Juzi niliona Italy wakitembeza msalaba na sanamu la maria mama wa yesu angani ili kuwaokoa, kilichofuatia ni vifo vingi zaidi vya watu.

Jana niliona video clip Gwajima akisihi watu kunawa mikono, nikajiuliza ameshindwa kuombea watu hili gonjwa lipite au mungu wake anachagua magonjwa ya kuponya na ya kuacha yaue watu maana mara nyingine hua wanadai wanaombea na kuponya ukimwi, kansa, nk, je corona mungu haiwezi?

Corona imevamia Italy hadi vatcan imeua mapadri, viongozi wakubwa wa kidini vatcan(petro alipojenga kanisa-mwamba)wanakufa kwa corona, mwamba unaenda kuanguka, siku corona ikimvaa papa ndio tutajua hatujui.

Haya mambo ya dini, maombi na sala ni ya watu, hayawezi kumsaidia binadamu kwa chochote. Mungu anaeshindwa kuzuia majanga na magonjwa ataweezaje kuyaondoa kwa maombi ya binadamu kama yeye na malaika wameshindwa kuzuia kabla?

Tuendelee kuomba ndugu zangu[emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tujifunze kumuomba Mungu straight sisi wenyewe,turekebishe MAHUSIANO BINAFSI SISI NA MUNGU siyo kupitia majizi haya
nadhani kwa vizazi viliyopita Mungu/Allah alikuwa anasikiliza maombi ya wanadamu na kuyafanyia kazi haraka.

ila kwa kizazi hiki cha wachungaji wanzinzi(kama gwajima), matepeli(kama wale mashehe wa instagram),Mungu kaamua kula pozi kidogo ili tunyoke.

Mungu kazia hapohapo ili hawa manabii na wachungaji feki wa kizazi hiki wapate kuumbuka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Imani katika Mungu Mwenyezi haifanyi kazi kama unavyofikiri, wacha Mungu hawana kinga ya kuugua na kufa ila wana kinga ya kufa kifo cha milele. Maana yake wanaweza kufa katika mwili lakini wanaishi milele katika roho. Ila shetani na mawakala zake wanasubiriwa na adhabu ya kifo cha milele
 
Back
Top Bottom