Corona Virus: Tanzania yathibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza, ni raia wa Tanzania, aliwasili kutoka Ubelgiji

Corona Virus: Tanzania yathibitisha kuwa na mgonjwa wa kwanza, ni raia wa Tanzania, aliwasili kutoka Ubelgiji

Tusilalamike Sana tuombe mungu tu afanye rehema zake ila korona ingeingia tu TZ ila kinachosikitisha umeingia kizembe wangeweka sheria ndege zinazotoka sehem kumeathiriwa Zaid watu wote wanawekwa karantin siku 15 wanapimwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ngoma ilishatinga kitambo!
Inawezekana vipi kuwa mgonjwa tarehe 15 kapita uwanja wa ndege akiwa hana dalili yoyote na tarehe 16 ithibitishwe ana corona?!!!
Huyo mwanamke iweje atoke matembezi majuu atue saa 10 jioni KIA na kuishia hotelini badala ya kufikia kwake??!! Au alikuwa anasubiria saibaba ya saa nne yenye bei nafuu ili aendelee na safari?
Danganyeni wadanganyika, serikali ya kiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu Ni Mwema Wakati Wote
Asimame Atuokoe Na Na Hii Kadhia
Hili Ni Bhalaa Zaidi Ya Nzige Na Madumadu
 
Kwa hiyo huo muunganiko hauuoni mpaka ithibitishwe na Serikali sio !?.

Hauoni upo uwezekano wa maambukizi zaidi hasa kutokana na Tabia ya huu Ugonjwa !?
Uwezekano siyo uhalisia bwashee....... Tusubiri taarifa ya wataalamu!
 
Mkuu kilichotokea kwa mgonjwa wa kwanza kugundulika Tanzania ndio kimetokea kwa nchi zote duniani zilizopata wagonjwa wa Corona Virus.
Tatizo pale uwanja wa ndege hawapimi vipimo vingi vya kimaabara.
Nadhani wana angalia joto, muonekano n.k.

Sasa dalili za nje zinazo pimika au kuonekana kirahisi zinatokea siku zaidi ya 4 tangu mtu apate maambukizi.
Zikishatokea wakaenda kupima maabara sampuli kutoka mwilini mwake ndio ugonjwa unaothibitika kirahisi.

Wakisema wapime damu na mate au mkojo au machozi kabla mgonjwa hajaruhusiwa kutoka uwanja wa ndege basi kutakuwa na vurugu kubwa na foleni kama hospital au kambiya magonjwa ya mlipuko, hata wzima watapatia maambukizi hapo hapo uwanja wa ndege.

Jambo la msingi kama tuko tayari kujitenga na dunia inabidi wasiruhusu ndege na mabasi yote ya kutoka nje ya nchi.
Ndo mana nikashauri wageni wawekwe kambi, hadi siku kumi na nne, au wazuie watu kuingia nchini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ki ukweli hatupo mahali salama!

Mtu anaingia nchini 15 anapimwa Kwenye uwanja wanagundua hana homa, baadae mgonjwa akiwa mgonjwa akiwa pekeake anaanza kujisikia vibaya anaamua mwenyewe kwenda hospital Ndo anapimwa anakutwa na virusi vya corona.

Je, ni kwamba virusi vya Corona havionekani hadi muathirika aanze kuona dalili?

Kama Ndo hivyo ni wangapi wameingia nchini wenye virusi vya corona tunasubiri hadi waanze kupata maumivu Ndo tujue kua huyu ni mgonjwa wa corona?

Kuna udhaifu mkubwa sana Kwenye hatua zinazochukuliwa kutoka na maelezo ya jinsi mgonjwa huyu amejulikana.

Ina maana tuna watu wengi wenye virusi vya corona nchini lakini tunasubiri hadi waanze kupata maumivu Ndo tuwajue.

Kwa nini serikali inavyoona haiwezi kuwajua wenye virusi vya corona kabla dalili hazijaanza kuonekana wasizuie wageni kuingia nchini au wakawa wanawekwa karantini kwa muda hadi watakapo jiridhisha?
bwana yule hanampango na afya za watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dada wa Tanga hayupo serious, ningekuwa president ningemfukuza kazi.hakuchukua tahadhari ya kutosha, just shouting at what she doesn’t know
 
Zaburi 91:10
 

Attachments

  • IMG-20200316-WA0052.jpg
    IMG-20200316-WA0052.jpg
    42.8 KB · Views: 1
Mwananchi, Ndugu yangu, upo sahihi kabisa.

Hiki ulichoandika ndicho kilichonifanya niandike kwamba waliokuwa wameshafuatilia ABCs za huu mlipuko, walishajua kuwa ni inevitable.

Ndio maana kila nchi ikisharipoti mtu/watu wa kwanza, kinachofuata ni kusambaa tu.

Ndio maana pia, hata viongozi na watu mashuhuri wameshindwa kuukwepa.

kuanzia leo hii kuelekea miezi kadhaa mbele, tutakuwa na wakati mgumu.

Sent using LF Electromagnetic Waves
 
So hapa kuna connections alizifanya na baadhi ya watu hapo hapo airport,aliyemkagua passport kama aliishika naye aliwazoa virus Mungu jaalia labda alikuwa amevaa vifaa kinga,tax driver aliyempakia kutoka uwanja wa ndege to lodge naye ana hatihati akawa alivizoa na wote wapo mtaani hawazijui hali zao wapo wanafurahi na jamaa zao tu.......

Mungu atunusuru Watanzania tuna mtihani mkubwa sana kuliko hawa wanasiasa wanavyofikiri.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Mkuu kilichotokea kwa mgonjwa wa kwanza kugundulika Tanzania ndio kimetokea kwa nchi zote duniani zilizopata wagonjwa wa Corona Virus.
Tatizo pale uwanja wa ndege hawapimi vipimo vingi vya kimaabara.
Nadhani wana angalia joto, muonekano n.k.

Sasa dalili za nje zinazo pimika au kuonekana kirahisi zinatokea siku zaidi ya 4 tangu mtu apate maambukizi.
Zikishatokea wakaenda kupima maabara sampuli kutoka mwilini mwake ndio ugonjwa unaothibitika kirahisi.

Wakisema wapime damu na mate au mkojo au machozi kabla mgonjwa hajaruhusiwa kutoka uwanja wa ndege basi kutakuwa na vurugu kubwa na foleni kama hospital au kambiya magonjwa ya mlipuko, hata wzima watapatia maambukizi hapo hapo uwanja wa ndege.

Jambo la msingi kama tuko tayari kujitenga na dunia inabidi wasiruhusu ndege na mabasi yote ya kutoka nje ya nchi.
Safi sana umechambua vizuri na kitaalam
 
Pepe Hotel Arusha Imezingirwa hakuna mtu Kutoka Wala kuingia. Mgonjwa alilala hapo.
 
Back
Top Bottom