Uchaguzi 2020 Corona virus: Uchaguzi 2020 kuahirishwa?

Uchaguzi 2020 Corona virus: Uchaguzi 2020 kuahirishwa?

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,206
Reaction score
18,549
Kwanza tuombe Mungu hii homa isitufikie.

Pili Ulaya wameshaanza kuzungumzia baadhi ya match kuchezwa bila mashabiki kwa hofu ya kuambukizwa hii homa.

Kwa jinsi ninavyoona kitakuwa kisingizio valid kwa serikali kubakia madarakani na kuchelewesha uchaguzi.

Au uchaguzi utafanyika bila campaign.

Haya yote yatategemea maambukizi yamefikia wapi.

----
Pendekezo: Kutokana na mlipuko wa Corona, uchaguzi mkuu 2020 uahirishwe.

Salamu ndugu Watanzania wenzangu, poleni na hekaheka za kujiokoa na balaa hili, afya zetu imara ndio kipaombele chetu namba moja.

Mwaka huu agenda kuu kitaifa ni uchaguzi mkuu, pamoja na mambo mengine, naomba tujikite kwenye hili kwa uzito wake.

Uchaguzi mkuu ni mchakato ambao huchukua muda mrefu hadi kukamilika, kuanzia maandalizi ya awali kabisa [mtu binafsi], na hata kitaasisi kama vyama vya siasa, hadi kufikia kupiga kura Oktoba 25 ambapo ni kilele kwa mwaka huu.

Katika kipindi hiki chote, wahusika [wagombea] huzunguka huku na kule na hutumia namna mbalimbali kujiandaa ikiwemo kutafuta wadhamini au hata wataalamu [waganga] ili kujiweka sawa.

Hii inaweza kuhusisha watu kwa makundi kutoka ndani na nje ya nchi, pamoja na mlipuko wa balaa hili, lakini mgombea kwa maslahi yake binafsi hashindwi kusafiri [hata ikibidi kwa siri] kwenda maeneo hatarishi ilimradi tu kutimiza azma yake.

Hii inaweza kuwa sehemu ya kuwezesha maambukizi na kusambaa kwa ugonjwa huu, hapo bado vikao vya ndani vya chama na baadae mikutano ya hadhara ili kunadi sera [kampeni] ambayo hukusanya watu wengi [mafuriko] kusikiliza na kuchambua sera.

Kwa hali ilivyo sasa nchini na duniani kote, hatuwezi kujua hili janga litakuwa na madhara kiasi gani, hivyo tunawajibika kuchukua kila aina ya tahadhari ili kujilinda na kulinda afya za wengine.

Tunapozuia watu kujumuika na hata kusafiri, hatupaswi kubeza madhara ya uchaguzi, ambao kwa vyovyote vile ni lazima utahusisha ziara na mikusanyiko ya watu.

Kwa hayo machache, pamoja na maoni yenu yenye nia njema na kuboresha hoja hii, napendekeza uchaguzi mkuu uahirishwe hadi hapo hali itapoonekana kutengemaa.

Tulinde AFYA zetu, tuwalinde wenzetu, maendeleo hayana VYAMA.
 
Tutatengeneza app za simu au mfumo kama wa m-pesa, au kuangalia namba yako ya nida watu watavote, kampeni tutachagua vituo viwili vya tv watu watamwaga sera zao hapo.

Kisha kwenye kujumuisha matokeo, upinzani utaita wadukuzi kutoka urusi wafanye kama kwa Trump, huku chama tawala wakijidhatiti na wataalamu kutoka Israel.

Hatimaye mshindi atatangazwa UCHAGUZI LAZIMA
 
Tabutupu,
Haiwezi kuathiri na kikubwa kama hapa kwetu ni jambo la kuomba mungu isije sababu kwakweli ule ugonjwa hauna utani.
 
Corona virus ni tishio kwa ustawi wa binadamu kila sehemu.Kuna uwezekano mkubwa wa kufuta michezo ya Olimpic huko Japan.
 
Ukimwi umekolea sana siku hivi, je umeona watu wamepu gua guesthouse? Uchaguzi ni kama kawaida.
 
Tabutupu,
Mda wote mnawaza Corona tu, nani kakwambia corona inaenea kila mahali, huyo kirusi ni kiumbe kama wewe ili aishi anategemea hali joto, anaenea nchi za baridi kipindi cha baridi kali lkn kwenye maeneo yenye joto hawezi kuishi. Kwa hiyo achana na hayo mawazo yako.
 
Yanini kuitabiria nchi matatizo,mada haina logic hii yafaa kufutiliwa mbali
 
Corona haichagui wala haibagui,inaweza anzia jumba jeupe,tena wakiwa kwenye kikao cha baraza la wakubwa.Wakiugua wote na wakatangulia,uchaguzi hautafanyika?
Iwe kweli basi
 
Back
Top Bottom