Coronavirus, Tanzania: Shule zote kuanzia za Awali, Msingi na Sekondari zafungwa. Mikusanyiko ikiwemo ya Kisiasa yasitishwa

Coronavirus, Tanzania: Shule zote kuanzia za Awali, Msingi na Sekondari zafungwa. Mikusanyiko ikiwemo ya Kisiasa yasitishwa

Wafunge na safari za ndani kwa ndani(mkoa - mkoa) ya tz kwa muda pia.
 
Hapo wazazi tuliokuwa tunadaiwa ada tu nasema afadhali tupumue Kaz kwa wamiliki washule walivyokuwa wanasubir tumalizie ada kabla ya mid term.

Kaz imebaki kwenye nyumba za kupanga Sasa naomba serikali itoe tamko hakuna kutoka wala kusafiri ili tupate sababu ya kuendelea kuishi mpaka tutakapopata pesa zao

Hahaaaa ,wew jamaa wewe ni nouma khaa 🙄🙄.
 
Kichekesho pale bandarini wanakagua wasafiri kutoka Zanzibar lakini pale Ubungo mambo shagalabagala wakati kuna mabasi yanatoka nje ya nchi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unataka wakose fedha za watalii?
Hakuna watalii saivi, kila nchi ipo katika hali ya tahadhari, ni kheri mara mia tukose fedha ya watalii wachache waliobaki kuliko ugonjwa uingie mtaani na vijijini, watu si tu watakufa kwa Corona bali watakufa kwa njaa kutokana na kulazimishwa kukaa ndani kama ugonjwa umesambaa.
 
Mbona vyuo vikuu havijafungwa?

Mbona wageni bado wanaruhusiwa kuingia, wakivileta je?

Hili katazo halikidhi haja ya kuzuia korona
 
GODZILLA,

Absolutely on point!

Halafu, kwa jinsi makazi yetu yalivyo, hususan huku mijini, ni vigumu sana hata kwa total lockdown kufanya kazi.

Huku Mwananyamala Kisiwani watu tunaishi kama dagaa walio kwenye tenga.

Uzuri, kama ulivyosema, huu ugonjwa siyo lethal kivile.

Na si ajabu wengi tunao lakini hata hatujui tunao.
 
Hii ya kufungwa shule madogo wa primary sipimi furaha yao... Yaani ni noma wanatamani korona isiishe [emoji81][emoji81]
Natamani nimtafte sister angu

Anipe story za dogo [emoji23][emoji23]

Anyway mwanafunzi atabaki kuwa mwanafunzi

Hata ningekua mm ningefurahi

Enzi hzo iyunga tech tunataka kuchoma shule dah [emoji28][emoji28][emoji28]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi sana hii tahadhali.nashauri pia kwenye usafiri wa gari abiria wasisimame wakae levo siti mana wakisimama kugusana ni rahisi,hili mnalionaje wadau? mabaa nayo yafungwe watu wakilewa wanagusana hovyo huko
Kwenye daladala kama ni ivyo inabidi nauli iongezeke,mfano kama kutoka tabata hadi muhimbili nauli iwe elfu Tano,je mtaweza.....ama kama vile serikali inataka kuweka level seat basi watoe mafuta bure kwa kila daladala
 
Mbona Mhs. wazari kaacha misikiti na makanisa au hawa watalindwa na Mungu mwenyewe
 
Back
Top Bottom