COVID-19: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atangaza ongezeko la Wagonjwa Wapya 196. Visa vyafikia 480

Mkuu, tujionee huruma basi, ikiwa hivyo utapata wapi sasa wakukupigia Kura mkuu, mambo yasiyofaa kuwekwa kwenye siasa za kijinga ni kuombea vifo viongezeke sio Tu vifo hata maambukizi pia
CCM wanataka watanzania wafe kwa wingi wapate kisingizio cha kuahirisha uchaguzi mkuu na pia wapate pesa nyingi toka WHO
 
Mambo bado mabichi kabisa....watu bado wanaishi kimazoea.....uchumi unadorora....kipato cha kila mmoja kiko hatarini.....mkuu ametulia mahali na barakoa mpaka kwenye 071........TANZANIA unakwenda wapi wewe....ukienda Karakoo, Feri huwezi jua kama kuna hili gonjwa.........bado tumesimamia misimamo yetu ya KIBURI.......for how long?? hatujui....MUNGU TUNAOMBA WEPESI KTK HILI.....
 
Sasa hizo takwimu ulizo nazo wewe kwanini usiweke hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mitaani bado watu wanakaa vijiweni vibarazani mikusanyiko ni mikubwa watoto wanacheza pamoja licha ya mashule kufungwa
 
Sasa hapo umeandika nini?

Yani ulichoandika ni ujinga mtupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wagonjwa tunajua wako wengi sana, maana hata mimi hapa nina dalili zote za corona lkn bado sijaenda kupima ili waniingize kwenye data zao.

Swali la msingi ni kuna vifo vingapi mpaka sasa?
Unforgetable
Rafiki yangu kanipigia simu kuwa amepoteza sense of smell na ana mafua ambayo hajawahi pata na ikifika usiku kifua kinamuuma na pia pua zinakuwa nzito kupitisha hewa kama vile ametoka ku dive kwenye kina kirefu cha maji, bila kusahau kichwa kuuma na uchovu wa mwili kiujumla. Kwa maelezo yake anasema tonsels alishapona tangia juzi.

Alichoshauriwa na dada angu ambaye ni daktari by profession afanye mazoezi hata ya kutembea pale anapojisikia uchovu na kutaka kupumzika na kujifukiza mkararusi, malimao, mchaichai na tangawizi maramoja kwa siku kwa dakika 10. Pia ale machungwa yasiyopungua 15 kwasiku then baada ya siku tatu tuangalie.

Kama hali itakuwa tofauti aende hospitali. Leo ni siku ya kwanza tangia auzingatie huo ushauri na ameamka wa afya njema tofauti na jana
 
Angalau wametangaza hata kama ni uongo,Japokuwa alipaswa atuambie hao wagonjwa waliopatikana ni miongoni mwa watu wangapi waliopimwa,karantini kuna watu wangapi,na walioruhusiwa ni wangapi. Nimejisemea tu maana siyo lazima wafanye kadiri ya matakwa haya. Tuendelee kuchukua tahadhari,Kama una uwezo wa kubaki nyumbani,fanya hivyo hasa kwa Dar maana hali siyo nzuri.
 
Ningekua mimi ndie nina maamuzi ya kuliende hili,nisingetangaza kifo wala maambukizi,jitihada zingekuwa katika kuwaelimisha watu kuhusu huu ugonjwa.Hakuna tija katika kutangaa vifo wala idadi ya wagonjwa.Kuna malaria yanaua,kuna magonjwa mengine yanaua kila kukicha,kwanini tulazimike kuagaza corona_
 
Huu ni muongozo kutoka WHO na sio matakwa ya mtu/nchi binafsi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…