CRDB bank inafilisika?

CRDB bank inafilisika?

Na makampuni ya simu yanawashikisha adabu mdogo mdogo...maana sasa hivi CRDB nao wana vibanda vya kuweka na kutoa pesa....na wanatoa Passo...

Nilikuwa nacheka siku moja na mume wangu baada ya kusikia tangazo...nkasema sasa hii benki au kampuni ya simu...na bado...wameamua ku join TIGO na M-Pesa

Mdada kwa hilo hauko sawa kabisa, siku hizi naona Kama natembea na akaunti mkononi vile. Nilikuwa Mpanda ndanindani niliweza kupata pesa kupitia Tigopesa. Niliamisha toka akaunti kwenda Tigopesa. Nawapa hongera sana hawa jamaa maana nilikuwa nimebanwa sina kitu kabisa.
 
Unaposema benki inakufa napata wasi wasi kidogo.kama miezi 2 iliyopita niliend Burundi! mie ni mteja wa benki kama tatu na nilibeba kadi zangu!baada ya kufika na kujaribu kadi zangu zote ziligoma na kwa bahati nzuri kati ya hizo benki tatu,ni benki ya crdb inakitengo cha huduma kwa wateja na nilipopiga 0755 19 77 00 muda wa sa mbili usiku,simu ilipokelewa mara moja na nilihudimiwa kwa haraka.Niliambiwa kadi yangu nimekosea kuweka namba ya siri na imefungwa kwa usalama wangu.kadi ilifunguliwa,nikapata huduma na kikubwa nilipata maelekezo tawi la benki ya crdb lilipo maeneo ya Burundi na nilifanikiwa kupata huduma kama nipo Tanzania.nilifurahi sana kupata huduma zao nchini Burundi na nilijivunia kuwa mtanzania ugenini!sasa unaposema benki inakufa unanipa wasiwasi!changamoto ndogo ndogo zipo na titaendelea kuziwasilisha sehemu usika ili wazifanyie kazi.Big up crdb bank,benki ya kizawa nchini na nje ya Tanzania!naomba ujipange na utupe mbadala wa Benki inayokufa nasi tukajionee!
 
Mdada kwa hilo hauko sawa kabisa, siku hizi naona Kama natembea na akaunti mkononi vile. Nilikuwa Mpanda ndanindani niliweza kupata pesa kupitia Tigopesa. Niliamisha toka akaunti kwenda Tigopesa. Nawapa hongera sana hawa jamaa maana nilikuwa nimebanwa sina kitu kabisa.

Sasa unampongeza Tigopesa au Bank...mbona tunaongea same language??????
 
sasa kwa sisi tunaotaka kujiunga katika share itakuwaje mweee ngoja nifuatilie habari hii kama ni kweli
 
Sasa unampongeza Tigopesa au Bank...mbona tunaongea same language??????

Soma vizuri utanielewa. Past few days nilikuwa Mpanda nilikwama sina pesa but huduma yao ya Simbanking iliniokoa maana niliamisha kwenda Tigopesa nikapata mzigo. Tena naona wamefanya safi sana kuwa na mawakala Coz sasa nitatoa kwa hao. Safi CRDB banki kwa kwenda extra mile to deliver.
 
Lengo la Benki ya Ulaya kuikopesha Benki ya CRDB ni kwa ajili wa wajasiliamari na sio kuwa benki haina uwezo wa kuwakopesha. Hili ni jambo la kawaida kabisa kwani hata African Devt Bank hupokesha benki nyingi hapa nchini ili nazo zitoe mikopo kwa wateja. Acha kukurupuka!
Hiyo NBC yako unayoishabikia ndio mabingwa wa kupika, jiulize katika kipindi cha miaka kumi iliyopita benki yako imeshabadili na kufukuza Ma CEo wangapi? If all is well as you potray?.Tufanye kazi jamani tuache siasa kwenye mambo ya msingi.

Makamba tutabishana kweli juu ya hili mkopo ni mkopo tu hakuna alie kurupuka hapa, nilifikiri ungesema mkopo hamkuchukua hapo ungekuwa umekosea na juu ya ma CEO kufukuzwa sii kweli maana hakuna mahali popote iliwahi kuandikwa hao viongozi wa juu wamefukuzwa note CEO NA VIONGOZI WENGINE WA BANK WANAFANYA KAZI KWA MIKATABA HIVYO NILAZIMA UWE UNAJUWA HILO
 
Profit yao ni million 100? Naona hesabu hujui kabisa ingia kwenye mtando wao uone walipata Trillion ngapi faida kwa mwaka! Jile79


Safi kabisa....Sasa km hiyo figure yako ni sahihi mi niingie kufanya nini mtandaoni tena? Hesabu najua kidogo acha kinivua nguo mwanakwetu
 
Back
Top Bottom