Uchaguzi 2020 CUF yatangaza kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wowote

Uchaguzi 2020 CUF yatangaza kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wowote

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
ED7FB922-DB81-4BBD-9F71-CF7F5F801FCE.jpeg


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Prof Ibrahim Lipumba, ametangaza kuwa kutokana na uchaguzi mkuu ulivyoendeshwa nchini, chama hicho hakitashiriki uchaguzi wowote na badala yake kitajikita katika harakati za kudai katiba mpya, ili kupatikana kwa Tume huru ya Uchaguzi.

“CUF tunawaomba Watanzania wote wapenda haki kuungana na sisi katika ibaada siku ya Alhamis, ambapo tutafunga kwa kutokula mchana na tufanye dua na maombi kila mmoja kwa imani yake ili kuomba hukumu ya haki kutokana na kile kilichofanyika”- Prof. Lipumba.
 
Huwa inatokea pale timu pinzani zinapokutana na wachezaji wakali lazima wapoteane kabisa.

Hongera Magufuli, Hongera Mwinyi, Hongera CCM
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Bado na Mbatia naye aliye ahidiwa kuwa chama chake kitakuwa chama kikuu cha upinzani atajitokeza hadharani kulia maumivu. Wakimalizika wote wanaingia ccm wenyewe kwa wenyewe kulana mikia ili kumfurahisha bwana mkubwa
 
Profesa alikosa hata watu 10 wa kumsikiliza kwenye kampeni zake, alafu leo analia? Hata aliposimama sokoni au stendi, watu walikuwa wanampa kisogo. Na aliulizwa na waandishi, mbona watu wamemsusa?, akaleta kiswahili swahili cha kujidanganya mwenyewe.
 
Back
Top Bottom