Dada Mkubwa tunakupenda na tunakukubali, kama ni wewe, ni wewe tu, hakuna mwingine! Usiruhusu uhuni huu, fuata Katiba na the due process, utabarikiwa

Japo umetoa NB lakini hichi kizazi Cha kusema kwa kuzunguka zunguka na kuficha hata kwa kidogo japo imeeleweka kwa kiasi , Inabidi kiishe au kifutike kabisa.

Kizazi jeuri chakuhoji na kusema pasina na kificho Cha level yoyote ya USiri iwe Stiri, Siri sana au imezuiliwa, Ndio kitainyanyua Tanzania.
Lakini hizi ngonjera za kubembelezana kama Nchi Ni Mali ya mtu Mmoja au ki grupu Cha watu kutaendelea kuwa na Chawa wa umri wote.
 
Kaka yangu Pascal Mayalla unahangaika sana ndugu yangu. Yaani badala ya kuwa straight to the point unazunguka wee ilimradi uonekane haujamkosoa mama.

Lakini ndugu yangu nikukumbushe kwamba wewe ni mkristo, naa maadiko ya kikristo yanatukataza sana kuwa ndumilakuwili ieleweke wazi WEWE NI BARIDI AU JOTO NA SIO VUGUVUGU.

Wewe ulipaswa unyooshe rula (maelezo) kwa huyo dada yako kwamba jambo ulilofanya kwenye ule mkutano wa Dodoma ni UBAKAJI WA DEMOKRASIA NDANI YA CHAMA HIVYO TUBU URUDISHE MCHAKATO HALISI WA KUMPATA MGOMBEA WA CHAMA KWA KUPIGIWA KURA.
 
Poa poa tumekupata. Haya turudi kwenye mada husika, unaizungumziaje ibara ya 100 ya katiba ya CCM?
 
Huyo ni mwanasheria alafu mwandishi nguli ambaye keshapitia misukosuko mingi kutokana na maandiko yake kwahiyo mpe heshima yake usije dhani huyo ni sawa na Zero IQ.
 
Haogopi wapinzani bali anaogopa wadogo zake wa damu.
 
Kaka pascal pole, na hongera kwa hili andiko japo siku ya mkutano mkuu waliuliza kabisa nani hapokei hii taarifa, wajumbe wote hakuna alie jitokeza ila baada ya hili inakuaje wajumbe wa mkutano mkuu mna ona si sheria?

Huenda wapo watu zaidi ya mmoja wanao elewa kifungu na taratibu zilizo kiukwa lakini hiyo nayo ni taasisi na board members wote walikuwepo na ikapitishwa kwa kauli moja naona kama ilikuwa nnje ya kanuni ilitakiwa kupingwa ile siku.

Ila mchezo ulishaisha na ulikuwa wa dakika 90 na kipenga kikapigwa matokeo yamesha tolewa, nadhani ni muda wa kungojea msimu ujao mpya ukianza maana hii ilikuwa kama mapumziko mafupi na kuvunjwa kwa kanuni katikati ya mchezo mlitakiwa kusema muda ule, ila kwa sasa kurudi tena dimbani haiwezekani kaka Pascal.
 
Wala siyo anaomba uteuzi he is just a whistle blower,kuna fukuto.
 
Afande Mafwele yuko standby ujue.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…