Mkuu tatizo kama hilo nilipata mwaka 2008 nilipata ajali ya pikipiki kati ya meno haya mawili ya mbele, moja lilikatika kipande kwa upande mmoja, siku lilipo katika hadi ile nerve ilikuwa exposed, sikwenda hospital likapona ila sasa kumbe kupitia ile nerve likaanza kuoza, likajenga tundu katikati, likaendelea mwaka huu likaanza kupasuka, maana limeoza ndani, kutokana na vhakula kuwa kinaingia, nikaamua kwenda hospitali, nilienda hospitali moja ipo maeneo ya posta nikaambiwa hapo nitoe niwekewe jino jipya kwa tsh 800000/= mbali na matibabu na vitu kama ivo. Nikasepa.
Nikaenda Regency, wakanambia jino 250000/= ni lazima ning'oe kisha nikae na pengo mpka lipone alafu kwa miezi kama sita nitapewa jino la bandia la kuvaa na kutoa kisha baada ya hapo nichonge permanent kama nitapenda na ila permanent ni kama laki 400k hivi.
Nikaondoka nikaenda hospital nyingine kariakoo ki dispensary kidogo hivi, Dr akasafisha lile tundu, akanichoma sindano, akanipiga pamba ndani, kisha akanambia niendr baada ya siku tatu atoe ile pamba, ang'oe jino, achukue kipimo anichongee la bandia la kudumu, bei yake tsh 70 elfu kufanyiwa kila kitu, nikaodoka
Nilipofika home sikuridhika maana kila hospital nilipita nikakuta maelezo mapya, kesho yake nikaelekea msasani kuna kio hospital cha meno pale, nilipofika nikamkuta yank mdogo tu nilipomuonesha jino, kwanza akanikaliza akaleta vitabu vya meno akaanza kunipa shule, jinsi jino lilivyo na linavyo athiriwa na kwa kuangalia jino langu nini kinaonekana, akanipiga x ray.. Akaona root yake ilivo
Baada ya hapo akatoa pamba niliowekewa k. Koo, aksema hapa hujafanya kitu, akasafisha jino lile tundu akafungia dawa, akajengea jino la cement akanipa vidonge akaniambia kanywe dose ikiisha uje. Siku iyo iyo akachukua kipimo cha jino.
Baada ya wiki nikarudi, akafumua ile cement nikafanyiwa root canal treatment, akasugua lile jino bila kung'oa mpk likabaki usawa wa fisi, akapachika jino jipya la kudumu la bandia, akanambia anisafishe kinywa, akasafisha jino moja moja.
Tulikaa masaa 6 akinishughulikia, akamaliza akanipa dawa na mouth wash, nikaondoka akanichaji kwa kila kitu tangu siku ya kwanza tsh 140000/= lak na arobaini tu. Nikashangaa. Nikawa mpya kinywani mpk leo
Yule jamaa ndie my best dentist nilieona anachukua muda wake mwingi kwa mteja kuelimisha na kumhudumia, amekuwa kama rafiki saizi na huwa nikija dar hapo ananiomba nipite anicheki meno
Unaweza ku-pm contacts zake na wapi yupo huyu dr.